Kauli dhidi ya Malawi: JWTZ wamshushua Lowassa!

war is arabic and premitive. Slavery ended long time. You arabs must go back to middle east. Leave tanzania for blacks
 
Nijuavyo mimi amiri jeshi mkuu hutamka au kuagiza jeshi kuingia vitani, lakini hili la Lowassa kusema jeshi letu liko tayari kwa vita haimaanishi kuwa ndio alitangaza vita, mbona katika sikukuu za Uhuru huwa jeshi linatuonesha silaha zake, hii huwa na maana gani kama si kutumbia kuwa wako "FIT", sasa EL amevunja katiba gani hapo, haya basi na mimi natamka "Jeshi letu liko Fit na tuko tayari kwa Vita, hao wa Maravi (Rays of Light) waje tu!
 
Kwani Tanzania ina amiri jeshi wangapi? Maana inatia mashaka kama tangazo kubwa la kuhusu vita linatolewa na kila mtu anayejisikia kusema hivyo.
 
Hivi hamjui Amiri Jeshi Mkuu wa majeshi ya Tanzania ni nani?

Hakuna Mwanajeshi wa chini yake anaeweza kuliongelea taifa kisiasa bila amri na au idhini yake.

Huyo amiri jeshi mkuu wenu alikua Ghana wala hana time na migogoro ya nchi yetu. Hapo ndio mjiulize lowasa angekua rais angeshaongea Rais wetu kimya hata hajasema kitu wakati yule wa malawi tayari kashazungumza ... Sometimes u wonder ka hii nchi ina kiongozi
 
Nijuavyo mimi amiri jeshi mkuu hutamka au kuagiza jeshi kuingia vitani, lakini hili la Lowassa kusema jeshi letu liko tayari kwa vita haimaanishi kuwa ndio alitangaza vita, mbona katika sikukuu za Uhuru huwa jeshi linatuonesha silaha zake, hii huwa na maana gani kama si kutumbia kuwa wako "FIT", sasa EL amevunja katiba gani hapo, haya basi na mimi natamka "Jeshi letu liko Fit na tuko tayari kwa Vita, hao wa Maravi (Rays of Light) waje tu!

Lowasa hakutoa general statement, Alikuwa very specific juu ya Malawi, kwamba Jeshi letu liko imara na Tayari kwa vita dhidi ya Malawi. Alikuwa halipi sifa za juu juu mkuu. Yeye, Sitta na Membe walilielekeza Jeshi letu kwenda vitani.
 
Kwani Sitta naye ana mamlaka gani na JWTZ? Mbona na yeye alipokuwa anakaimu nafasi ya pinda aliyasema kama hayo ya EL?

Kasema SITTA kasema MEMBE imeonekana sawa,lkn LOWASA imekua nongwa,kule USA nafasi ya LOWASA BUNGENI inashikiliwa na st.JOHN KERY ni mtu mkubwa sana ktk maswala ya ulinzi na usalama ktk nchi.sasa bongo ndivyo sivyo.Mwanamume huyu LOWASA wanamtetema sana.
 
KATIBA ya JMT haimtambui mtu huyu. Niliyasema haya kwenye ile thread ya Mwanakijiji aliokuwa akidadisi uwezo na utayari wetu kwa vita. Lowasa ameishi serikalini kwa muda mrefu. Alipaswa kulifahamu hili. Sio kukurupuka kutamka yale maneno eti kwa kuwa mahasimu wake akina Membe na Sitta wametangulia kuyasema!
Ni heri lowassa kaonyesha njia kuliko huyo jk aliyechoka kaa goal la....sioni sababu gani mnahangaika na Lowassa badala ya ku deal na huyo JK nchi iliyomshinda,mnaongelea ungese tokeeni mwuikomboe nchi yenu msibaki mnakodoa macho na computers zenu, wengine mnatumia id siyo zenu kwa manufaa ya hao wanaowalipa kudiscuss upuuzi humu jamvini, kuanzai asubuhi mpaka jioni mtu anapost topic humu kazi anafanya saa ngap?
 
Ka issue ka Lake Nyasa? Unaona ni kadogo? Na je kikwete alikuwepo bungeni kujibu maswali? Je kiongozi wa Ulinzi wa nchi bungeni kuwahakikishia wananchi kuwa tuna jeshi imara ni kosa? Mbona maboga yanajazana hapa kwa chuki tu?
 
Membe alitoa msimamo wa serikali, ambapo alitaka mazungumzo yaendelee huku Malawi wakifuata makubaliano ya awali ya nchi mbili kusitisha shughuli za utafiti wa mafuta na gas. Kwa uelewa wangu mdogo katika mahuisiano ya kimataifa, nilidhani kabla ya kutangaza vita, SERIKALI inatoa msimamo na ufafanuzi wa jambo husika. Kitu ambacho Membe alishakifanya. Swali nisilolijuwa ni kwamba kamati ya ulinzi ilikwenda kuongeza au kupunguza kitu gani na ina mandate gani katika hili?

Naona bunge linavamia madaraka ya serikali kwasababu mkuu wa kaya bado yuko usingizini. Kamati ya bunge inapokuja na kauli nzito zaidi ya ile ya serikali kila mtu anashangaa kama bunge ndio serikali ya nchi hii. Nchi hii chini ya uongozi wa Jk imekuwa vurugu tupu, na bunge limekuwa ndio mahakama (refer wezi wa rada waliposomewa hukumu bungeni na Chikawe) na serikali (hili la Lowasa kutoa msimamo wa serikali/nchi).


Very unfortunate, now JWTZ are all confused as to who says what, when, and how. I would think the bells would go off when the watchdogs of our land receive mixed chain of command. JK wake up and do/say something about this; a coupe deter is nourished when the soldiers are all mixed up and the government loses power to the legislature.
 
Amiri Jeshi Mkuu DHAIFU hadi hii leo hajatoa tamko lolote kuhusu madai ya Malawi....hahusiki!!!!
 
[QUOTE By kyelatz war is arabic and premitive. Slavery ended long time. You arabs must go back to middle east. Leave tanzania for blacks
=Kilembwe;4421688]He! yamekuwa haya tena?[/QUOTE]

Nami pia yamenishangaza. "Waarab, premitive, slavery" yote haya yameingiaje kwenye mada hii. Tanzania, twendeni tu tutafika na muyatakayo yatakua.
 
Najua kwanini Sitta, Membe na Lowassa ndio wapo mstari wa mbele sana kuongelea hii issue...
 
Mi sioni tatizo kwa Mh. Lowasa kutoa kauli ile kwa nafasi aliyonayo, kwani hakukurupuka lazima amejadili na wajumbe wa kamati yake pamoja na waziri anayehusika lakini pia lazima ametoa kauli hiyo kwa ridhaa ya rais. Hivyo watanzania tunaamini kauli ile ni rais kupitia watendaji wake, sasa napata shida kuelewa kama ni kweli, kwanini Jwtz ihoji kauli hiyo? Kanuni inaruhusu hilo? Kwa kufanya hivyo hawajajihusisha na siasa? Sidhani kama sahihi kuwakosoa wakubwa wao hadharani.
Una hakika na unachokisema?

war is arabic and premitive. Slavery ended long time. You arabs must go back to middle east. Leave tanzania for blacks
Unataka kusema Lowassa, Sitta na Membe ni Waarabu primitive wanaopenda vita na kuendesha utumwa Tanzania?
 
Habari,
Samahani mimi wakati wa vita ya kagera nilikuwa bado sijazaliwa, ila kuna mtu amewahi kunisimulia kuwa ilimchukuwa kama siku 40 Nyerere kutangaza uamuzi wa vita na uganda, aliyenisimulia anasema Nyerere alifanya mfungo kabisa wa siku kadhaa kabla ya kuamua vita.

Nijuavyo mimi ni kuwa Rais ni mtu wa mwisho kabisa kuzungumzia vita na akishazungumza au kuagiza basi lazima kinuke, muda ukifika ataongea tu mwacheni, kwani mnafikiri hajuwi?

Usishangae pengine hata haya mnayoandika hapa yote anayasoma! kuwa rais inataka moyo!. Vita yenyewe ya kazi gani sukari inauzwa kilo 2500? Hiyo ya kagera hadi leo imechangia ufukara wetu, mnapenda vita?
 
Back
Top Bottom