Kauli dhidi ya Malawi: JWTZ wamshushua Lowassa!

KATIBA ya JMT haimtambui mtu huyu. Niliyasema haya kwenye ile thread ya Mwanakijiji aliokuwa akidadisi uwezo na utayari wetu kwa vita. Lowasa ameishi serikalini kwa muda mrefu. Alipaswa kulifahamu hili. Sio kukurupuka kutamka yale maneno eti kwa kuwa mahasimu wake akina Membe na Sitta wametangulia kuyasema!

Wewe una akili sana wewe.
 
Nikiwa naelekea ofisini asubuhi hii Radio Clouds wakiwa wanapitia habari za kwenye magazeti ya leo wamesoma gazeti moja likisema JWTZ limemkanya Edward Lowassa kwa kauli yake aliyotoa hivi karibuni kwamba amethibitishiwa kwamba Jeshi letu liko imara na Tayari kwa vita.
Kwa chanzo chako hicho cha habari, asante na kwaheri.
 
Tusipoangalia utafika wakati Lowassa anaamrisha Jeshi liende vitani na JK anazuia!! Kwa nn Lowasa aongee yale wakati hana mamlaka hayo?? alipata wapi uwezo ule na tena akiwa na baadhia ya makamanda wa JWTZ!! Its shame in our country...
 
Mi sioni tatizo kwa Mh. Lowasa kutoa kauli ile kwa nafasi aliyonayo, kwani hakukurupuka lazima amejadili na wajumbe wa kamati yake pamoja na waziri anayehusika lakini pia lazima ametoa kauli hiyo kwa ridhaa ya rais. Hivyo watanzania tunaamini kauli ile ni rais kupitia watendaji wake, sasa napata shida kuelewa kama ni kweli, kwanini Jwtz ihoji kauli hiyo? Kanuni inaruhusu hilo? Kwa kufanya hivyo hawajajihusisha na siasa? Sidhani kama sahihi kuwakosoa wakubwa wao hadharani.
 
Tusipoangalia utafika wakati Lowassa anaamrisha Jeshi liende vitani na JK anazuia!! Kwa nn Lowasa aongee yale wakati hana mamlaka hayo?? alipata wapi uwezo ule na tena akiwa na baadhia ya makamanda wa JWTZ!! Its shame in our country...

Tatizo la lowasa siku za karibuni amekuwa anafikiria kujipandisha chati ya kisiasa bila kujali kama mazingira yanaruhusu au la? Kama ni kweli alitoa kauli ile akiwa na wanajeshi basi hao wanajeshi wanatakiwa kuchukuliwa hatua za kinidhamu ikibainika kwamba ni wao waliomdokeza kwamba Jeshi liko imara na Tayari kwa vita.
 
Lowasa alisema kama mwenyekiti wa kamati ya bunge ya ulinzi na usalama

Tuna tatizo kubwa sana na uongozi wa bunge letu; hawa wenyeviti wa kamati za bunge sio wasemaji wa bunge!! Msemaji mkuu wa bunge ni Spika , hawa wenyeviti wanatakiwa kureport shuhuli zao kwa Spika na yeye ndiye mwenye mamlaka ya kutoa tamko kwa niaba ya bunge. Uongozi dhaifu wa bunge ndio umewafanya hawa wenyeviti wajitwalie madaraka ambayo si yao!! Nature abhors a vacuum!!!
 
Sasa hapo Lowasa ana kosa gani wakati utayari wao wenye JWTZ Waliuonesha hadharani wakati wa sherehe za miaka 50 ya uhuru.
 
Mi sioni tatizo kwa Mh. Lowasa kutoa kauli ile kwa nafasi aliyonayo, kwani hakukurupuka lazima amejadili na wajumbe wa kamati yake pamoja na waziri anayehusika lakini pia lazima ametoa kauli hiyo kwa ridhaa ya rais. Hivyo watanzania tunaamini kauli ile ni rais kupitia watendaji wake, sasa napata shida kuelewa kama ni kweli, kwanini Jwtz ihoji kauli hiyo? Kanuni inaruhusu hilo? Kwa kufanya hivyo hawajajihusisha na siasa? Sidhani kama sahihi kuwakosoa wakubwa wao hadharani.
Lowasa ni mjanja sana. Aliyatamka yale ndani ya maeneo ya Bunge ambako kuna kinga lukuki. Vinginevyo alipaswa kuwekwa ndani kwa kuvunja KATIBA ya JMT. Tumtume KUB Mbowe amuulize WM Pinda Alhamisi ijayo kwenye maswali ya papokwa papo kama Lowasa, Membe na Sitta walikuwa sahihi kuyatamka yale waliyoyatamka.
 
Wakina Lowasa hawa watatuingiza kwenye vita kwa kujitafutia ujiko wa kisiasa nyie endeleeni kushabikia tu! Bora jeshi limemkanya na next time wamrushe kichurachura ndo watakoma.
 
Bravo Lowasa. Kama mkuu ni dhaifu inalazimu kusaidiwa, maana matamshi magumu dhaifu hawezii! Huu uraisi una wenyewe bwana, dhaifu, dhaifuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu! Mwache LL ateme cheche anaogopa nini sasa na kama kakereka si aseme mwenyewe!

nakuunga mkono mkuu
 
Mbona wamechelewa sana kutoa tamko? Au wanamuogopa lowasa? Jeshi nalo ni dhaifu
 
KATIBA ya JMT haimtambui mtu huyu. Niliyasema haya kwenye ile thread ya Mwanakijiji aliokuwa akidadisi uwezo na utayari wetu kwa vita. Lowasa ameishi serikalini kwa muda mrefu. Alipaswa kulifahamu hili. Sio kukurupuka kutamka yale maneno eti kwa kuwa mahasimu wake akina Membe na Sitta wametangulia kuyasema!

Hali hii ni inaendelea kuonyesha udhaifu wa JK. Ni kweli yawezekana kauli ya EL ilitolewa na mtu asiyestahili, lakini ilitolewa muda muafaka. Ni wazi kuwa imesaidia sana kuleta joto kali Malawi na kuwafanya warudi nyuma!

Hata vyomba vya habari vya Malawi na wananchi wake walipaniki na kufikia kuwaita Watanzania wapenda vita!

Maswali ya kujiuliza, aliyetakiwa kutoa kauli hiyo katika muda muafaka alikuwa wapi? Je, alitoa kauli yoyote?
Kwa nini hakutoa wakati ilikuwa ni muhimu sana kipindi kile? Napata tabu kuelewa kama ipo siku ataelewa kuwa uongozi ni pamoja na kuchukua hatua sahihi katika muda muafaka.

Vyombo vya habari, mna rekodi kubwa ya matukio mbalimbali ambayo Mkulu alilala tu, hatoi kauli mpaka mambo yameharibika. Mfano, Wabunge kujiongezea posho kinyemela! Alikaa kimya mpaka hali ilipokuwa mbaya , akawaruka. Huu si uongozi. Wananchi wanapaswa kukumbushwa matukio haya.Baba hutoka chumbani watoto wanapogombana sebuleni!

El, pamoja na ufisadi umejitahidi kwa hili.

JWTZ, kauli imetulia. Tumewaelewa, ni lugha ya kitu uzima, ya kusema aliyetakiwa kutoa kauli alikuwa kimya as if hajui kinachoendelea!Itamuuma sana hii kulika EL.
 
Lowasa ni mjanja sana. Aliyatamka yale ndani ya maeneo ya Bunge ambako kuna kinga lukuki. Vinginevyo alipaswa kuwekwa ndani kwa kuvunja KATIBA ya JMT. Tumtume KUB Mbowe amuulize WM Pinda Alhamisi ijayo kwenye maswali ya papokwa papo kama Lowasa, Membe na Sitta walikuwa sahihi kuyatamka yale waliyoyatamka.
Wazo zuri sana, walioko karibu na waeshimiwa hawa tunaomba ujumbe huu ufike.
 
Kubali au kataa. Lowasa ndiyo Raisi wa Tz kwa sasa. Ndiyo maana alitoa kauli ya kuwatisha wa Malawi. Jk kawekwa kama sura tu ya kiti cha uraisi, hawa Jk na El hawakukutana street, wanamakubaliano yao ambayo wengine hatuyajui. Kama huamini jiulize, jeuri, ujasiri na nguvu ya El inatoka wapi kama yeye si raisi aliye nyuma ya pazia? Bomu hili litaripuka kabla ya uchaguzi 2015. Hapo ndipo wa Tz wengi tutaujua ukweli kati ya El na Jk.
 
Ni kweli aliyetoa kauli hakustahili. Lakini alitoa kauli muafaka katika muda sahihi. Wamalawi wakapaniki na kurudi nyuma.

Maswali ya kujiuliza, aliyepaswa kutoa kauli alitoa? kwa nini?

Tunaweza kukumbuka matukio mengi ya aina hii, mfano wabunge waliamua kujiongezea posho, alikaa kimya mpaka hali ikawa mbaya ndio akaibuka na kuwaruka! Huu ni uongozi wa aina ya kipekee. Baba hutoka chumbani watoto wanapogombana sebuleni.

EL pamoja na ufisadi wake, kwa hili amesaidia.

JWTZ, kauli yenu iko sawa. Tumeielewa, ni lugha ya kiutu uzima ya kupeleka ujumbe kwa aliyetakiwa kutoa kauli. Itamuuma zaidi JK kuliko EL.
 
Kwa hiyo jeshi linataka kusema halijajiandaa wala haliko tayari kwa vita?

Incase tukivamiwa ndo hapo wataanza mafunzo ya kujiweka tayari kwa vita?

Mume;
Yaani mimi hapa nilipo sasa hivi natetemeka tu! Nimeogopa sana
 
Back
Top Bottom