Kanisa katoliki, linaanzia ngazi ya jumuhiya, ambazo ziko chini ya kigango husika katika eneo husika. Kisha ngazi ya parokia ambazo vigango vyote vinareport na mkuu wa parokia ni paroko anae teuliwa na Askofu. Parokia ziko chini ya Jimbo ambapo hapa kuna ngazi mbili tofauti kwa maana ya kwamba kuna majimbo makuu mfano, mwanza & , dar es salaam ambayo hayapokei Askofu mpya Bali yanapokea askofu mzoefu ndo maana baada ya kifo cha Anthony mayalla , mrithi wake alitoka jimbo la dodoma ambaye ni yuda thadei walaichi. Pia kuna majimbo madogo yanayopokea askofu mpya mfano jimbo la bunda & musoma .naposema askofu mpya namaanisha askofu anaeteuliwa kutoka katika katika wadhifa wa upadri.
Majimbo yote yanaongozwa na Maskofu. Kisha kuna level ya ukadinali ambayo pengo ni moja wao katika Afrika . kisha upapa. Nyadhifa zote wanaruhusiwa kistaafu na kuitwa wastafuu isipokuwa level ya upadri ambayo ndo Nadhiri mama . mtu akiiziaki hii basi uonywa na kupewa adhabu ndani ya kanisa ktk eneo husika au kuitwa vaticani. Ikishindikana basi hufukuzwa kabisaaa...rejea dr. Slaa.
Hivyo katoliki ni dola & serikali kama serikali zingine hivyo kupangua huo mpangilio ni ngumu sana. Bado papa ni kiongozi mkuu lakini bado kuna makadinali wanao mwongozi katika kufanya mabadiliko yoyote . rejea mitaguso kadhaaa ndani ya kanisaa katoliki.