Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,339
- 51,882
KATIKA MAISHA YAKO YA SIASA EPUKA MAMBO HAYA;
Kwa Mkono wa Robert Heriel.
Endapo utapenda uongozi na utawala, mpaka ikakubidi kujiingiza kwenye mapito ya kisiasa, basi nakusihi Epuka mambo haya ili uwe na Amani hata siku ujapoondoka duniani.
1. Epuka kumwaga Damu isiyo na hatia.
Fanya utakavyofanya, ruka utakavyoruka, pigana utakavyo pigana lakini kamwe Mkono wako, wala mawazo yako, wala mdomo wako usihusike Kwa vyovyote kumwaga Damu ya mtu asiye na hatia, mtu mwenye haki kamwe usije ukamwaga damu yake.
Hiyo ni laana na ni dhambi kuu.
Kumuua mwenye haki ni jaribio la kutaka kumuua MUNGU. Ni uhaini katika falme za kiroho. Ni jaribio la kutaka kuangusha Dola ya MUNGU.
MUNGU hafi lakini yapo majaribio ya kutaka kumuua. Moja ya majaribio hayo ni kuua wenye haki.
Kama utaweza kumuua mwenye Haki tafsiri yake unauwezo wa kumuua MUNGU sema kinachokushinda na kuwa huna nguvu na uweza wa kumuua MUNGU mwenyewe kutokana na kuwa wewe ni Binadamu.
Huwezi muua mwenye haki alafu Mungu akakusamehe, hiyo asije akakudanganya yeyote Yule. Utake kumuua MUNGU alafu huyo huyo Mungu akusamehe.
Ni kosa la uhaini ambalo hata kibinadamu adhabu yake ni kifo cha uchungu.
Epuka kumwaga Damu isiyo na hatia.
Zipo namna za kudili na wenye Haki, lakini sio kuwaua. Ni hatari kuliko unavyofikiri.
Ukaidi na kiburi chako kisijekikazidi akili yako ukashindwa kuelewa maana ya haya niyasemayo.
2. Epuka kudhulumu Mali za wajane na Yatima.
Katika maisha yako yote, jitahidi Sana nakuomba, pambana uwezavyo, chuma Mali utakavyochuma lakini kamwe usije ukagusa Mali za wajane na Yatima wasiojiweza.
Ni hatari, unagusa kiti cha Enzo hapo, ni Kama unapiga jiwe Ikulu.
Kama ni kudhulumu huwezi kuacha basi dhulumu Kwa akili, wapo watu wa kuwadhulumu lakini sio wajane na mayatima.
Mdhulumu mtu Kama Taikon, yeye mtapambana naye kisabuni, utapewa dhambi lakini jiwe lako halitakuwa limegusa Ikulu, hujapiga panapouma. Ukitaka umpige Mungu panapouma basi wadhulumu Yatima wasiojiweza na Wajane.
Wengine wadhulumu tuu ikiwa ni wajinga wajinga au wazembe wazembe. Lakini Wajane na Yatima achana nao.
Kwa Wadhambi au Majambazi Professional wanajua nazungumzia Jambo gani.
Kudhulumu Yatima na Wajane sio professional na haina tija.
Hata hivyo usijeninukuu vibaya kwamba nimekuruhusu kudhulumu isipokuwa Yatima na Wajane. Hapana. Kudhulumu ni dhambi kubwa, lakini kudhulumu Wajane na Yatima ni kupiga panapouma kwenye kiti cha Enzi.
3. Epuka kuchukua mke/mume wa Mtu mwingine kisa unamamlaka makubwa zaidi yake.
Usichukue mke au mume wa Mtu mwingine kisa juu yake. Hiyo ni hatari kubwa. Unapambana na MUNGU pasipo ya wewe kujua.
Ni kumchukua mke wa Mungu. Kwa maana utakapomchukua mke wa mtu mwingine hatakuwa na chakukufanya isipokuwa kumlilia Mungu.
Ninachojaribu kukieleza hapa ni kuwa; usipambane na MUNGU.
Na mtu anayembana na Mungu ni Yule anayepigana na watu wasio wa level yake.
Yaani wewe ni Heavy weight alafu unataka kupambana na mtu ambaye ni uzito wa Kati.
Kama ni Waziri na unaona unauchu Sana WA ngono, ukashindwa kujizuia mpaka ukaamua kutenda dhambi, basi chukua mke wa Waziri mwenzako, au mbunge au watu wa level yako ili mkiparangana mmalizane wenyewe kesi isimfikie MUNGU.
Ogopa mtu ambaye unapambana naye alafu unajua kabisa hakuwezi ni hatari Sana.
Mtu huyo hupambani naye isipokuwa unapambana na MUNGU.
Kama ni Rais, chukua wake wa Rais wenzako ili mpashane misuli, mpasuane vyema ili mmalizane kabisa. Usitake kumalizana na Mungu hata siku moja.
Katika maisha ogopa kupambana na mtu uliyemzidi uwezo wa kila kitu. Hapo utakuwa unamuonea, na unapambana na MUNGU mkuu.
Kumbuka Mungu ndiye Refa, sasa ukipambana na mtu yeyote uliyemzidi uwezo lazima umchezee Rafu, na hapo utashangaa Refa anaingilia Kati.
Sijui Kama naeleweka.
4. Epuka kuwaamini wanaokuunga Mkono. Ni Kheri uwaamini wasiokuunga mkono.
Kwenye Siasa katika mambo unayopaswa kwenda nayo Kwa umakini ni watu wako wa karibu. Usiwaamini kupitiliza.
Ni Kheri umuamini adui yako ili uwe Salama na utabaki salama tuu kuliko kumuamini mtu wa karibu yako Kisiasa.
Naomba niishie hapa, nashuka kituo kinachofuata.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa DIT, Dar es salaam
Kwa Mkono wa Robert Heriel.
Endapo utapenda uongozi na utawala, mpaka ikakubidi kujiingiza kwenye mapito ya kisiasa, basi nakusihi Epuka mambo haya ili uwe na Amani hata siku ujapoondoka duniani.
1. Epuka kumwaga Damu isiyo na hatia.
Fanya utakavyofanya, ruka utakavyoruka, pigana utakavyo pigana lakini kamwe Mkono wako, wala mawazo yako, wala mdomo wako usihusike Kwa vyovyote kumwaga Damu ya mtu asiye na hatia, mtu mwenye haki kamwe usije ukamwaga damu yake.
Hiyo ni laana na ni dhambi kuu.
Kumuua mwenye haki ni jaribio la kutaka kumuua MUNGU. Ni uhaini katika falme za kiroho. Ni jaribio la kutaka kuangusha Dola ya MUNGU.
MUNGU hafi lakini yapo majaribio ya kutaka kumuua. Moja ya majaribio hayo ni kuua wenye haki.
Kama utaweza kumuua mwenye Haki tafsiri yake unauwezo wa kumuua MUNGU sema kinachokushinda na kuwa huna nguvu na uweza wa kumuua MUNGU mwenyewe kutokana na kuwa wewe ni Binadamu.
Huwezi muua mwenye haki alafu Mungu akakusamehe, hiyo asije akakudanganya yeyote Yule. Utake kumuua MUNGU alafu huyo huyo Mungu akusamehe.
Ni kosa la uhaini ambalo hata kibinadamu adhabu yake ni kifo cha uchungu.
Epuka kumwaga Damu isiyo na hatia.
Zipo namna za kudili na wenye Haki, lakini sio kuwaua. Ni hatari kuliko unavyofikiri.
Ukaidi na kiburi chako kisijekikazidi akili yako ukashindwa kuelewa maana ya haya niyasemayo.
2. Epuka kudhulumu Mali za wajane na Yatima.
Katika maisha yako yote, jitahidi Sana nakuomba, pambana uwezavyo, chuma Mali utakavyochuma lakini kamwe usije ukagusa Mali za wajane na Yatima wasiojiweza.
Ni hatari, unagusa kiti cha Enzo hapo, ni Kama unapiga jiwe Ikulu.
Kama ni kudhulumu huwezi kuacha basi dhulumu Kwa akili, wapo watu wa kuwadhulumu lakini sio wajane na mayatima.
Mdhulumu mtu Kama Taikon, yeye mtapambana naye kisabuni, utapewa dhambi lakini jiwe lako halitakuwa limegusa Ikulu, hujapiga panapouma. Ukitaka umpige Mungu panapouma basi wadhulumu Yatima wasiojiweza na Wajane.
Wengine wadhulumu tuu ikiwa ni wajinga wajinga au wazembe wazembe. Lakini Wajane na Yatima achana nao.
Kwa Wadhambi au Majambazi Professional wanajua nazungumzia Jambo gani.
Kudhulumu Yatima na Wajane sio professional na haina tija.
Hata hivyo usijeninukuu vibaya kwamba nimekuruhusu kudhulumu isipokuwa Yatima na Wajane. Hapana. Kudhulumu ni dhambi kubwa, lakini kudhulumu Wajane na Yatima ni kupiga panapouma kwenye kiti cha Enzi.
3. Epuka kuchukua mke/mume wa Mtu mwingine kisa unamamlaka makubwa zaidi yake.
Usichukue mke au mume wa Mtu mwingine kisa juu yake. Hiyo ni hatari kubwa. Unapambana na MUNGU pasipo ya wewe kujua.
Ni kumchukua mke wa Mungu. Kwa maana utakapomchukua mke wa mtu mwingine hatakuwa na chakukufanya isipokuwa kumlilia Mungu.
Ninachojaribu kukieleza hapa ni kuwa; usipambane na MUNGU.
Na mtu anayembana na Mungu ni Yule anayepigana na watu wasio wa level yake.
Yaani wewe ni Heavy weight alafu unataka kupambana na mtu ambaye ni uzito wa Kati.
Kama ni Waziri na unaona unauchu Sana WA ngono, ukashindwa kujizuia mpaka ukaamua kutenda dhambi, basi chukua mke wa Waziri mwenzako, au mbunge au watu wa level yako ili mkiparangana mmalizane wenyewe kesi isimfikie MUNGU.
Ogopa mtu ambaye unapambana naye alafu unajua kabisa hakuwezi ni hatari Sana.
Mtu huyo hupambani naye isipokuwa unapambana na MUNGU.
Kama ni Rais, chukua wake wa Rais wenzako ili mpashane misuli, mpasuane vyema ili mmalizane kabisa. Usitake kumalizana na Mungu hata siku moja.
Katika maisha ogopa kupambana na mtu uliyemzidi uwezo wa kila kitu. Hapo utakuwa unamuonea, na unapambana na MUNGU mkuu.
Kumbuka Mungu ndiye Refa, sasa ukipambana na mtu yeyote uliyemzidi uwezo lazima umchezee Rafu, na hapo utashangaa Refa anaingilia Kati.
Sijui Kama naeleweka.
4. Epuka kuwaamini wanaokuunga Mkono. Ni Kheri uwaamini wasiokuunga mkono.
Kwenye Siasa katika mambo unayopaswa kwenda nayo Kwa umakini ni watu wako wa karibu. Usiwaamini kupitiliza.
Ni Kheri umuamini adui yako ili uwe Salama na utabaki salama tuu kuliko kumuamini mtu wa karibu yako Kisiasa.
Naomba niishie hapa, nashuka kituo kinachofuata.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa DIT, Dar es salaam