Katika kila mfumo wa utawala wa nchi kuna kauli hazivumiliki

kmbwembwe

JF-Expert Member
Aug 16, 2012
10,428
7,216
Ukienda Marekani ukaanza kusifu ujamaa wa Karl Marx na sera za kupinga ubepari watakuvumilia kwa muda tu wakiona unaanza kupata ushawishi watahakikisha unapotea. Ubepari na ubeberu ndio sera iliyoletea nchi yao maendeleo na kua tajiri kuliko nchi zote duniani.

Vivyo hivyo kwa Uingereza, Ufaransa na Ujerumani. Ukienda Uchina na Urusi kuna kauli hazivumiliki. China ukitaka kuleta sera za Marekani na za mabepari wa magharibi watakuzuia. Saudi arabia ukitaka kutangaza injili ya Yesu watakudhibiti mara moja.

Leo hivi kuna mtu anakuja Tanzania na anatoa kauli za kejeli na dharau dhidi ya mfumo wetu wa kujali utu na usawa na kupigania ukombozi wa raia kiuchumi. Mtu huyo sio mwingine ni Antipas Tundu Lissu. Lissu hadi sasa ametoa kauli nyingi dhidi ya mfumo wetu wa uongozi unaoegemea maendeleo kwa wananchi kwa usawa.

Hivi punde baada ya kurudi kutoka Ubelgiji alikokua anafundwa kuhujumu uhuru wa nchi yetu; Lissu amedharau na kukejeli mafanikio ya ujenzi wa miundombinu inayojengwa nchini. Eti hata wakoloni walijenga miundombinu barabara reli na bandari.

Huko ubeleji hata kama hawakumwambia msomi wa kiwango chake angejiuliza kama wabeleji walijenga reli gati mto Congo na barabara kwa ajili ya uchumi wa Congo au Ubelgiji. Huyu anajifanya hajui Wakongo zaidi million 10 waliuliwa kwa kushindwa kukamilisha kwa muda kazi zao tu za kitumwa kwenye mashamba ya mpira na ujenzi wa miundombinu ya kikoloni.

Tukirudi hapa Tanzania, reli barabara zilizojengwa na Wajerumani utalinganishaje na reli tunayojenga wenyewe kwa uchumi wetu kama nchi huru, utakua mtu mwehu. Kama Lissu aliyejaa jazba na kisasi ndio utaweza sema miundombinu ya ukoloni ina maana sawa na hii anajenga John Pombe Magufuli.
 
Wacha weweee kila mtu ana haki ya maoni yake uhuru wa kujieleza ni haki yake. Na kama mlivyo WaTanzania ukabila hamna, lakini tatizo lenu ni udini umewajaa, wakiristo wameshika utawala, waislamu wanaonekana hawana sauti. Umeingia Saudia tu na ukaleta udini.

kmbwembwe
 
NI KWELI HATA WAKOLONI WALIJENGA MIUNDOMBINU YAKIWEMO MAJENGO YA SHULE, HOSPITALI, MAHAKAMA, BARABARA, NK. TENA KWA KIWANGO BORA KULIKO CHETU. LAKINI TULIWAKATAA KWA SABABU WALITUNYIMA UHURU WA KUTOA MAONI NA KUJIELEZA.

WALITUNYIMA FURSA YA KUJIAMULIA MAMBO YETU. WALITUNYIMA FURSA YA KUKUTANIKA KATIKA SHUGHULI ZA KISIASA NA KUAMUA MAMBO YETU. WALITUNYIMA NAFASI YA KUHOJI NA KUKOSOA.

MAMBO HAYO YA HOVYO YA KIKOLONI NDIYO ANAFANYA JIWE. HATAKI TUSEME TUNACHOPENDA NA TUSICHOKIPENDA. KWA NINI?
 
kmbwembwe,

Watu wengine bwana, hapa nawe unaona umeandika uzi wa maana. Kijana kaa chini angalia ni mtu wa aina gani unayetaka kumchallenge alafu jilinganishe uwezo wako na yeye ili ujipange kwa hoja sio huu utopolo unaotuletea humu. Huna point humu za kuargue hoja za Lissu.
Hahahah
 
Point muhimu ambayo anaizungumzia huyu mwamba TL ni kwamba maendeleo ya vitu yaende sambamba na maendeleo ya watu.

Ila sio mtu unajisifia kwamba nimefanya maendeleo ya vitu fulani huku umetengeneza unemployment rate kwa 200%, na life gumu kitaa .

Badilika na ujitambue usilidhike na 10000 ya maji unayopewa ili uandike madudu hapa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kmbwembwe,

Watu wengine bwana, hapa nawe unaona umeandika uzi wa maana. Kijana kaa chini angalia ni mtu wa aina gani unayetaka kumchallenge alafu jilinganishe uwezo wako na yeye ili ujipange kwa hoja sio huu utopolo unaotuletea humu. Huna point humu za kuargue hoja za Lissu.
Tatizo nyie nyumbu mumeshatekwa akili kwamba lisu ni msomi anajua wakati anaongozwa na jazba na chuki tu. Hivi sasa mnaomsapoti mumegeuka kasuku kurudiarudia uongo kejeli na matusi anayotoa
 
Back
Top Bottom