Maboso
JF-Expert Member
- Feb 18, 2013
- 5,164
- 5,761
CHADEMA itafanya nini:
Na hii ndio Ilani ya uchaguzi ya Chadema 2015. Pitia ukurasa wa 40 na 41
- Kujenga reli mpya na kukarabati zilizopo kwa viwango vya kisasa kwa kuzingatia maslahi ya nchi. Hii ni pamoja na kujenga uwezo wa kuzalisha mataluma ya reli nchini.
- Kuboresha bandari zilizopo na kujenga mpya kama vitega uchumi vya Taifa ili kurejesha biashara tulizopoteza kwa bandari za nchi jirani.
- Kujenga barabara nchini kwa kuzingatia ubora hasa zile za vijijini.
- Kujenga shirika la Ndege la Taifa linalojiendesha kwa misingi ya faida.
- Kujenga miundombinu ya kisasa ili kuondoa misongamano ya magari hasa katika majiji ya Dar es salaam, Mwanza, Kuimarisha usafiri wa majini kwa kuboresha na kuweka miundo mbinu mipya.
- Bandari kuwa njia kuu ya uchumi kwa kuhudumia kilimo na viwanda. Na pia, kuchangia zaidi ya theluthi moja ya pato la Taifa.
- Shirika la ndege la Taifa (Air Tanzania) kuimarishwa ili kutoa huduma nchini na nje ya nchi huku likijiendesha kibiashara zaidi na kwa fiada.
- Wananchi hasa wa visiwani kupata huduma muhimu za kiuchumi na kijamii.
- Mizigo yote mizito kusafirishwa kwa njia ya reli na meli ili kupunguza gharama na kuongeza tija katika uzalishaji. Kupunguza ajali na kulinda miundo mbinu.
- Barabara zinazodumu na zilizo salama zaidi kwa watumiaji.
Na hii ndio Ilani ya uchaguzi ya Chadema 2015. Pitia ukurasa wa 40 na 41