Mr Dudumizi
JF-Expert Member
- Sep 9, 2020
- 6,977
- 12,440
Habari zenu wana JF wenzangu,
Kwanza kabla ya kuendelea na mada hii ningependa watu wengi wafahamu kwamba mimi nimeandika mada hii kwa utashi wangu mwenyewe. Sikushawishiwa, sikulazimishwa wala kushikiwa akili na mwanasiasa yoyote iwe wa upinzani, wa CCM au wa kujitegemea. Bali nimeandika hili kutokana na mapenzi ya kweli niliyonayo kwa nchi yangu ya asili ya Tanzania.
Ndugu wana JF wenzangu, mimi nimekuwa mfuatiliaji mkubwa wa siasa zetu za Tanzania toka enzi za uanzishwaji wa mfumo wa vyama vingi, hadi leo hii ninavyoandika mada hii, naweza kusema kwamba nina ujuzi na ufahamu wa kutosha kuhusu siasa zetu za Tanzania. Miaka yote hiyo nakiri kwamba niliwahi kuwa mwanachama wa vyama vikubwa tofauti.
Kwanza mimi na familia yetu mpaka bibi zetu na babu zetu tulianza kuwa upande wa NCCR - Mageuzi chini ya aliekuwa mwanasiasa machachari na hodari wa enzi hizo hayati Augustino L. Mrema. Baadae miaka ya 2000, binafsi nikaamua kuhamia chama cha Wananchi CUF baada ya kuona vyama vingine vya upinzani kama vile NCCR Mageuzi na TLP vinaendeleza migogoro mbali mbali. Kwa upande wa familia yetu wengine walihamia TLP, na wengine wakabaki NCCR Mageuzi.
Mwaka 2009 nikajiunga rasmi Chadema, japo sikuwa mwanachama, lakini nikawa shabiki na kuhakikisha natembeza elimu ya kutosha kwa vijana wenzangu ili na wao wajiunge na chama hicho au hata kama hawakujiunga kwa njia ya uanachama, basi wahakikishe wawe wanakipigia kura chama hicho katika chaguzi mbali mbali.
Kwa vile mimi binafsi niliamini kuwa chama hicho kina viongozi wa kweli na wenye malengo ya kweli ya kutuletea ukombozi haswa baada ya kuisomwa na kuelewa ile list ya mafisadi wa taifa letu kule mwembe yanga.
Pilika pilika za kukiombea kura Chadema nilikuwa nazifanya nikiwa tayari naishi nje ya nchi, kwa kuwahamasisha watanzania wenzangu waendelee kukiamini na kukitegemea Chadema katika maisha yao.
Mwaka 2015, niliamua kuachana na Chadema baada ya mwenyekiti wetu na genge lake kuharibu hali ya hewa chamani, na kupelekea matumaini yetu ya kukichinjia baharini chama tawala kuyayuka kama chumvi ndani ya maji. Kibaya au kizuri zaidi CCM wao wakasimamisha mtu ambae ilikuwa ngumu kwa mtu anaejielewa wakati ule kumnyima kura. Jamaa alipata kura kwa wana CCM na wasiokuwa wana CCM, kwa wanasiasa na wasiokuwa wana siasa. Huku kwa upande wa upinzani wakitumia muda mwingi kupangua kashfa za ufisadi walizomuanzishia wao wenyewe mgombea wao.
Hii ni sawa na mwanaume uwambie wazazi wako kwamba unataka kumpa talaka mkeo baada ya kumkuta na mwanaume ndani ya chumba chako wakigegedana. Afu baadae uje uwambie kwamba umeahirisha kumpa talaka baada ya kugundua kwamba mkeo na huyo kijana hawakuwa wakigegedana bali walikuwa wakitafuta panya chumbani kwako. Imagine kwa utetezi huo wazazi watakuelewaje??
Zile zilikuwa ni siasa uchwara ambazo wengi hatupendi zirudie.
Anyway pamoja na pilika pilika zilizotokea miaka 7 iliyopita kati ya CCM na Wapinzani. Sasa chama hicho tawala kimeamua kukaachini na wapinzani ili kumaliza tofauti zao zilizokuwepo huko nyuma, kwa kuanzisha maridhiano ambayo yatapunguza kelele kwa pande zote mbili. Yani upinzani na serikali ambayo ndio CCM yenyewe. Katika hili watu wengi tuliwasifu wapinzani na watawala kwa kukaa chini na kupanga namna ya kuitengeneza upya Tanzania yenye amani, upendo na mshikamano kupitia vyama vya siasa na asasi mbali mbali.
Tuliwapongeza pia wenyeviti wa vyama hivyo ambao ndio waliouwezesha mchakato huo wa maridhiano kama vile mwenyekiti wa CCM mh raisi Samia S. Hassani, mwenyekiti wa Chadema mh Mbowe, mwenyekiti wa CUF mh Lipumba, kiongozi wa ACT Wazalendo mh Zito Kabwe, mzee wa ubwabwa nk.
Naweza kusema kwamba viongozi hao japo wana akili zao, madaraka yao na maamuzi yao, lkn inaonesha kuwa hawafanyi haya kwa mawazo yao, bali kwa kufuata miongozo thabiti ya vyama vyao.
Sasa anapokuja mtu kutoka ughaibuni ghafla na kuanza kupinga hadharani kile kinachofanywa na kiongozi wake au chama chake, huyo anakuwa ni mtovu wa nidhamu kwa chama chake na viongozi wake. Kwa sababu kama mtu haupendi au haukubaliani na kile kinachofanywa na chama chako au kiongozi wako, kwanini usipeleke madai yako katika chama yakajadiliwa na kutatuliwa kichama, badala ya kuja kuliongelea katika public kwa lengo la kumchafua na kumfanya yule kiongozi anaesimamia swala hilo (mwenyekiti) aonekane hana uelewa wowote juu ya swala hilo analolisimamia?
Inamaana mwenyekiti hufanya haya bila kuwashirikisha viongozi wa chama, na kama huwa anawashirikisha ni kwanini makamu huyo asimwambie kwamba hafurahishwi na maridhiano yao, ili wakae chini wayamalize kuliko kuja kulalamikia kwenye mikutano ya hadhara. Matokeo yake mwenyekiti atachoshwa na vijembe na yeye aamue kujibu na kupelekea mtifuano ambao utaharibu mchakato mzima wa hayo maridhiano yaliopo.
Mbona hatujasikia kelele hizi kutoka katika vyama vingine? Yani ni kilekile tu ambacho watu wengi ndio wanakiangalia!
Anyway katika hili mimi nasimama na Mbowe maana watanzania wengi tushachoshwa na siasa za majitaka, kuchafuana, kuingia barabarani kupambana na vyombo vya dola afu mwisho wa siku alieshawishi watu waingie barabarani akimbilie tena ulaya akaendelee ku claim ukimbizi kupitia mgongo wa fujo alizoziratibu mwenyewe nchini kwetu.
Haya yanafanywa sana na viongozi wa nchi za fujo na za vita kama Congo au Nigeria kwa kuendelea kuwadhamini waasi wapigane ili wao waendelee kupewa ukimbizi huko ughaibuni.
Mbowe asitishwe na kelele za chura, yeye aendelee kusimamia kile anachoona kina manufaa kwa taifa na chama chake. Afu huyo mleta kelele akiona hasikilizwi basi aanze chama chake mwenyewe, mbona Zito alipoona haeleweki akaanzisha cha kwake, Lisu anangoja nini?.
Sio kwa vile anaona uchaguzi wa chama unakaribia ndo ajaribu ku take advantage kupitia swala hili ili alitumie kama fimbo katika vikao vya chama kumuangusha mwenyekiti.
Lakini vile vile huenda jamaa amepewa mission na wabeberu ili aje ayumbishe maridhiano kwa lengo la kutengeneza migogoro itakayozaa vita, na vita ikiingia yanakuwa yale ya Congo. Wao wanaingia kujichotea tu bila mtu yoyote kuwa control. Maana wabeleji sio watu wazuri, wanachokifanya Congo na wajomba zao wamarekani kila mtu anakiona.
Hapa wenye upeo unaogusa mbingu ndo wataelewa.
Kwanza kabla ya kuendelea na mada hii ningependa watu wengi wafahamu kwamba mimi nimeandika mada hii kwa utashi wangu mwenyewe. Sikushawishiwa, sikulazimishwa wala kushikiwa akili na mwanasiasa yoyote iwe wa upinzani, wa CCM au wa kujitegemea. Bali nimeandika hili kutokana na mapenzi ya kweli niliyonayo kwa nchi yangu ya asili ya Tanzania.
Ndugu wana JF wenzangu, mimi nimekuwa mfuatiliaji mkubwa wa siasa zetu za Tanzania toka enzi za uanzishwaji wa mfumo wa vyama vingi, hadi leo hii ninavyoandika mada hii, naweza kusema kwamba nina ujuzi na ufahamu wa kutosha kuhusu siasa zetu za Tanzania. Miaka yote hiyo nakiri kwamba niliwahi kuwa mwanachama wa vyama vikubwa tofauti.
Kwanza mimi na familia yetu mpaka bibi zetu na babu zetu tulianza kuwa upande wa NCCR - Mageuzi chini ya aliekuwa mwanasiasa machachari na hodari wa enzi hizo hayati Augustino L. Mrema. Baadae miaka ya 2000, binafsi nikaamua kuhamia chama cha Wananchi CUF baada ya kuona vyama vingine vya upinzani kama vile NCCR Mageuzi na TLP vinaendeleza migogoro mbali mbali. Kwa upande wa familia yetu wengine walihamia TLP, na wengine wakabaki NCCR Mageuzi.
Mwaka 2009 nikajiunga rasmi Chadema, japo sikuwa mwanachama, lakini nikawa shabiki na kuhakikisha natembeza elimu ya kutosha kwa vijana wenzangu ili na wao wajiunge na chama hicho au hata kama hawakujiunga kwa njia ya uanachama, basi wahakikishe wawe wanakipigia kura chama hicho katika chaguzi mbali mbali.
Kwa vile mimi binafsi niliamini kuwa chama hicho kina viongozi wa kweli na wenye malengo ya kweli ya kutuletea ukombozi haswa baada ya kuisomwa na kuelewa ile list ya mafisadi wa taifa letu kule mwembe yanga.
Pilika pilika za kukiombea kura Chadema nilikuwa nazifanya nikiwa tayari naishi nje ya nchi, kwa kuwahamasisha watanzania wenzangu waendelee kukiamini na kukitegemea Chadema katika maisha yao.
Mwaka 2015, niliamua kuachana na Chadema baada ya mwenyekiti wetu na genge lake kuharibu hali ya hewa chamani, na kupelekea matumaini yetu ya kukichinjia baharini chama tawala kuyayuka kama chumvi ndani ya maji. Kibaya au kizuri zaidi CCM wao wakasimamisha mtu ambae ilikuwa ngumu kwa mtu anaejielewa wakati ule kumnyima kura. Jamaa alipata kura kwa wana CCM na wasiokuwa wana CCM, kwa wanasiasa na wasiokuwa wana siasa. Huku kwa upande wa upinzani wakitumia muda mwingi kupangua kashfa za ufisadi walizomuanzishia wao wenyewe mgombea wao.
Hii ni sawa na mwanaume uwambie wazazi wako kwamba unataka kumpa talaka mkeo baada ya kumkuta na mwanaume ndani ya chumba chako wakigegedana. Afu baadae uje uwambie kwamba umeahirisha kumpa talaka baada ya kugundua kwamba mkeo na huyo kijana hawakuwa wakigegedana bali walikuwa wakitafuta panya chumbani kwako. Imagine kwa utetezi huo wazazi watakuelewaje??
Zile zilikuwa ni siasa uchwara ambazo wengi hatupendi zirudie.
Anyway pamoja na pilika pilika zilizotokea miaka 7 iliyopita kati ya CCM na Wapinzani. Sasa chama hicho tawala kimeamua kukaachini na wapinzani ili kumaliza tofauti zao zilizokuwepo huko nyuma, kwa kuanzisha maridhiano ambayo yatapunguza kelele kwa pande zote mbili. Yani upinzani na serikali ambayo ndio CCM yenyewe. Katika hili watu wengi tuliwasifu wapinzani na watawala kwa kukaa chini na kupanga namna ya kuitengeneza upya Tanzania yenye amani, upendo na mshikamano kupitia vyama vya siasa na asasi mbali mbali.
Tuliwapongeza pia wenyeviti wa vyama hivyo ambao ndio waliouwezesha mchakato huo wa maridhiano kama vile mwenyekiti wa CCM mh raisi Samia S. Hassani, mwenyekiti wa Chadema mh Mbowe, mwenyekiti wa CUF mh Lipumba, kiongozi wa ACT Wazalendo mh Zito Kabwe, mzee wa ubwabwa nk.
Naweza kusema kwamba viongozi hao japo wana akili zao, madaraka yao na maamuzi yao, lkn inaonesha kuwa hawafanyi haya kwa mawazo yao, bali kwa kufuata miongozo thabiti ya vyama vyao.
Sasa anapokuja mtu kutoka ughaibuni ghafla na kuanza kupinga hadharani kile kinachofanywa na kiongozi wake au chama chake, huyo anakuwa ni mtovu wa nidhamu kwa chama chake na viongozi wake. Kwa sababu kama mtu haupendi au haukubaliani na kile kinachofanywa na chama chako au kiongozi wako, kwanini usipeleke madai yako katika chama yakajadiliwa na kutatuliwa kichama, badala ya kuja kuliongelea katika public kwa lengo la kumchafua na kumfanya yule kiongozi anaesimamia swala hilo (mwenyekiti) aonekane hana uelewa wowote juu ya swala hilo analolisimamia?
Inamaana mwenyekiti hufanya haya bila kuwashirikisha viongozi wa chama, na kama huwa anawashirikisha ni kwanini makamu huyo asimwambie kwamba hafurahishwi na maridhiano yao, ili wakae chini wayamalize kuliko kuja kulalamikia kwenye mikutano ya hadhara. Matokeo yake mwenyekiti atachoshwa na vijembe na yeye aamue kujibu na kupelekea mtifuano ambao utaharibu mchakato mzima wa hayo maridhiano yaliopo.
Mbona hatujasikia kelele hizi kutoka katika vyama vingine? Yani ni kilekile tu ambacho watu wengi ndio wanakiangalia!
Anyway katika hili mimi nasimama na Mbowe maana watanzania wengi tushachoshwa na siasa za majitaka, kuchafuana, kuingia barabarani kupambana na vyombo vya dola afu mwisho wa siku alieshawishi watu waingie barabarani akimbilie tena ulaya akaendelee ku claim ukimbizi kupitia mgongo wa fujo alizoziratibu mwenyewe nchini kwetu.
Haya yanafanywa sana na viongozi wa nchi za fujo na za vita kama Congo au Nigeria kwa kuendelea kuwadhamini waasi wapigane ili wao waendelee kupewa ukimbizi huko ughaibuni.
Mbowe asitishwe na kelele za chura, yeye aendelee kusimamia kile anachoona kina manufaa kwa taifa na chama chake. Afu huyo mleta kelele akiona hasikilizwi basi aanze chama chake mwenyewe, mbona Zito alipoona haeleweki akaanzisha cha kwake, Lisu anangoja nini?.
Sio kwa vile anaona uchaguzi wa chama unakaribia ndo ajaribu ku take advantage kupitia swala hili ili alitumie kama fimbo katika vikao vya chama kumuangusha mwenyekiti.
Lakini vile vile huenda jamaa amepewa mission na wabeberu ili aje ayumbishe maridhiano kwa lengo la kutengeneza migogoro itakayozaa vita, na vita ikiingia yanakuwa yale ya Congo. Wao wanaingia kujichotea tu bila mtu yoyote kuwa control. Maana wabeleji sio watu wazuri, wanachokifanya Congo na wajomba zao wamarekani kila mtu anakiona.
Hapa wenye upeo unaogusa mbingu ndo wataelewa.