Katika hili Magufuli uwe DIKTETA

Benevolent Dictator mara nyingi huleta mabadiliko mazuri sana. Kuminya uhuru, inategemea ni uhuru wa aina gani wa habari.
Kama ni wauchochezi huo hauna msamaha ni lazima uminywe.
Lakini wa kuikosoa Serikali na kutoa njia mbadala sioni kama kuna tatizo.
Maana katiba yetu inaruhusu hilo.
Hata hivyo nimekuelewa mkuu.
Sema ukianza kusakama watu kwa kigezo cha uchochezi huwezi jua mipaka yako na mwisho kujikuta unasakama sana watu wako na kuingilia uhuru wa habari ambao ni muhimu kwa taifa. Nchi zilizokomaa kwenye masuala ya uhuru yanaona njia bora ya kukabiliana na uchochezi ni kuukanusha na si kudeal nao kibabe. Pengine sisi hatuna resources au ukomavu wa kuelewa hilo.

Pia mi siamini kuwa kunaweza kuwa na benevolent dictator. Maana kwenye kufanya hivyo kuna watu anakuwa anawakandamiza japo wanaweza kuwa wachache. Pia anaweza kuwa anafanya maamuzi nje ya taratibu tulizojiwekea kitu ambacho ni kibaya. Udikteta ni kama uganga kwa wakristo, tunaamini hakuna uganga mzuri hata kama ulisaidia kukoponya au kukupa utajiri.
 
Kama huwezi kuweka lijamu mdomoni heri uwakwepe maana utaleta mambo mengine tusiyoyahitaji humu.
Usiyoyahitaji wewe wenzako wanayatafuta, niachie mwenyewe niamue. Unaweza kuninyima kuamkua wazee.

Kama hayakufai si unaruka tu?

Au we Mhariri humu?
 
Hay yawepo ili muradi:
(i) Sheria zifwatwe tusije ingizwa hasara za KiDowanzi,
(ii) Udikiteta usizidi ama kukaribia ule wa Hitla,
(iii) Maamuzi yasifanywe kutafuta zaidi SIFA.
(iv) Maoni ya WENGINE wenye mapenzi mwema na Nchi yasipuuzwe sababu tu wako "upande wa pili", nk. nk..
Kumbe na wewe unaamini HITLER alikuwa DIKITETA!!!

Madhara ya UKOLONI ni makubwa sana.

Wauloze WAJEREMANI kama ADOLF alikuwa DIKITETA. Hayo ya kuambiwa na maadui zake changanya na ya kwako.

Ni kweli aliwaua wayahudi. Lakini hili lilikuwa DAI la wajeremani waliwachukia wageni matajiri nchini kwao na hasa WAYAHUDI. Sawa na DONALD anavyotimua wageni kwake huko. Kwangu huo siyo udikiteta.

Adolf aliwafanya wajeremani wawe taifa kubwa. Wote walimpenda.
 
Usiyoyahitaji wewe wenzako wanayatafuta, niachie mwenyewe niamue. Unaweza kuninyima kuamkua wazee.

Kama hayakufai si unaruka tu?

Au we Mhariri humu?
Mkuu Nakubaliana nawe kabisaa. Naweka breki za dharura.
Nimefurahia comments zako.
Ahsante.
 
Nimemkubali sana Magu. Shida kubwa ni waTz wachache walafi. Kama hao walio saini mikataba hotelini nje ya nchi. Bado wapo na tunao humu uraiani. Luna kundi lingine la wasomi sio wote waliotuweka hapa tulipo.ndio kina muhongo na wenzake kuwataja majina sio vema ndio hao wanaotisha kua tutalipa fidia na kua tulisaini mikataba. Ni Bahati mbaya sana wamesoma kwa Kodi za wananchi hawa masikini. wamesahau uzalendo na utaifa wetu.wanaiba fedha na kuficha kwa hao wezi. Wanataka wawe wao tuu na watoto wao ndio wawe na elimu nzuri wasome ulaya waendelee kututawala na kuiba.this time kuwe na uangalizi hasa kwenye teuzi.km hukusoma nyumbani basi utakua umekosa sifa fulani kwa hio nafasi.pili naomba yafanyike marekebisho makubwa kwenye mitaala toka std 1 hadi chuo kikuu.liingizwe somo la uraia.liwe maalum kufundisha utaifa. Tembelea nchi km Israel, Iran nanyingine nyingi utaona tulichokosa nacho ni Uzalendo.
 
Wana JF kulingana na ripoti iliyotolewa leo na tume ya rais kuhusu MCHANGA ambao kwa miaka 17 tumekuwa tukiibiwa kama nchi ukiwa na MADINI mbali mbali na kuwa undervalued ili tuibiwe, IMEKASIRISHA sana kila mtu.
Katika hili sitakuwa nimekosea kumwomba Magufuli awe DIKITETA MZURI/BENEVOLENT dictator.

Aina hii ya UDIKTETA huwa INAKUBALIKA maana huwa ni ya mtu anayetaka kuwafanyia WANANCHI wake MAZURI kwa MANUFAA ya taifa lake.

Tunaweza kuiga mfano wa aliyekuwa mwanzilishi wa taifa la Singapore. "Lee Kuan Yew"
Yeye aliwafukuza kazi na hata KUWAFUNGA JELA RAFIKI zake na jamaa zake waliojihusisha na UFISADI.

Na kuiweka nchi yake katika ulimwengu wa KWANZA/ First world na kipato kikubwa zaidi ya baadhi ya nchi za ULAYA.

Ni nini kilichomsaidia? Ni udikteta mzuri. Hakuwa na huruma.
Jambo la kwanza KABLA ya yote FREEZE/ZIFUNGE ACCOUNT zao zote za WATUHUMIWA zilizo na FEDHA NYINGI ambazo source yake ni ya MASHAKA.


Magufuli ukicheka na mtu Tanzania HAITABADILIKA.
Kuagiza vyombo vya ulinzi na usalama vifanye kazi ni vizuri. Lakini KUFUATILIA na KUTENDEA kazi MAAGIZO yako hilo nalo ni lingine.Things should start rolling ASAP& NOW!

Mfano mwingine ni ule wa juzi Juzi wa Rais mpya wa Gambia ame FREEZE Dola millioni 50 zilizokuwa ZIMEIBIWA na rais aliyetoka madarakani Jammeh.

Ukitaka nchi INYOOKE. Ni VIZURI Watanzania waanze kuona MALI ZAO na FEDHA zao zilizoibiwa ZIKIRUDISHWA serikalini. BILA kuwa na HURUMA huyu ni mtoto wa nani ama alikuwa nani.
Usipokuwa DIKTETA mzuri sasa basi Tanzania HATUTAPATA MWINGINE tena.

WACHACHE watalia lakini MAMILIONI ya Watanzania WATAKUPENDA na kusema UMETUOKOA.
Mungu IBARIKI Tanzania na Rais Magufuli


naunga mkono hoja na ikiwezekana katiba ipitiwe upya ili marais waliopita wakamatwe na kunyongwa au kuuliwa moja kwa moja maana hawakuwa na huruma na taifa letu na wananchi wake. Rais Magufuli tafadhali sikia kilio cha Watanzania, tunataka Mkapa na Kikwete kunyongwa hadharani au kuuliwa na kutaifishwa mali zao.
 
Nimemkubali sana Magu. Shida kubwa ni waTz wachache walafi. Kama hao walio saini mikataba hotelini nje ya nchi. Bado wapo na tunao humu uraiani. Luna kundi lingine la wasomi sio wote waliotuweka hapa tulipo.ndio kina muhongo na wenzake kuwataja majina sio vema ndio hao wanaotisha kua tutalipa fidia na kua tulisaini mikataba. Ni Bahati mbaya sana wamesoma kwa Kodi za wananchi hawa masikini. wamesahau uzalendo na utaifa wetu.wanaiba fedha na kuficha kwa hao wezi. Wanataka wawe wao tuu na watoto wao ndio wawe na elimu nzuri wasome ulaya waendelee kututawala na kuiba.this time kuwe na uangalizi hasa kwenye teuzi.km hukusoma nyumbani basi utakua umekosa sifa fulani kwa hio nafasi.pili naomba yafanyike marekebisho makubwa kwenye mitaala toka std 1 hadi chuo kikuu.liingizwe somo la uraia.liwe maalum kufundisha utaifa. Tembelea nchi km Israel, Iran nanyingine nyingi utaona tulichokosa nacho ni Uzalendo.
Mbona Magufuli naye aliupitisha huu mkataba?
 
naunga mkono hoja na ikiwezekana katiba ipitiwe upya ili marais waliopita wakamatwe na kunyongwa au kuuliwa moja kwa moja maana hawakuwa na huruma na taifa letu na wananchi wake. Rais Magufuli tafadhali sikia kilio cha Watanzania, tunataka Mkapa na Kikwete kunyongwa hadharani au kuuliwa na kutaifishwa mali zao.
Mkuu pamoja na uchungu wa mali zetu. Tanzania HATUWEZI kufuata MKONDO huo wa KUNYONGANA. Maana once kiongozi akianza kufanya hivyo basi CYCLE/MZUNGUKO wa aina hiyo huendelea zaidi na zaidi. Hata hivyo NAKUBALIANA nawe katika hili la KURUDISHA MALI iliyokuwa imeibiw. IRUDI kwa WANANCHI bila HURUMA.
 
Nimemkubali sana Magu. Shida kubwa ni waTz wachache walafi. Kama hao walio saini mikataba hotelini nje ya nchi. Bado wapo na tunao humu uraiani. Luna kundi lingine la wasomi sio wote waliotuweka hapa tulipo.ndio kina muhongo na wenzake kuwataja majina sio vema ndio hao wanaotisha kua tutalipa fidia na kua tulisaini mikataba. Ni Bahati mbaya sana wamesoma kwa Kodi za wananchi hawa masikini. wamesahau uzalendo na utaifa wetu.wanaiba fedha na kuficha kwa hao wezi. Wanataka wawe wao tuu na watoto wao ndio wawe na elimu nzuri wasome ulaya waendelee kututawala na kuiba.this time kuwe na uangalizi hasa kwenye teuzi.km hukusoma nyumbani basi utakua umekosa sifa fulani kwa hio nafasi.pili naomba yafanyike marekebisho makubwa kwenye mitaala toka std 1 hadi chuo kikuu.liingizwe somo la uraia.liwe maalum kufundisha utaifa. Tembelea nchi km Israel, Iran nanyingine nyingi utaona tulichokosa nacho ni Uzalendo.
Ni wazo zuri sana la kufikiriwa. Maana wengi wetu hatuna uzalendo. Na hiyo ndo inatuletea mambo kama haya
 
Mbona Magufuli naye aliupitisha huu mkataba?
Magifuli hakuupitisha mkataba huu. Hebu gonga penyewe hasa. NI YUPI atakayewajibishwa wakati Magufuli akiwa yungali Waziri? Najua JIBU unalo na unalijua. Taja bila woga wowote.
 
Magifuli hakuupitisha mkataba huu. Hebu gonga penyewe hasa. NI YUPI atakayewajibishwa wakati Magufuli akiwa yungali Waziri? Najua JIBU unalo na unalijua. Taja bila woga wowote.
Magufuli aliupitisha kama Waziri, mikataba mikubwa haiwezi kupita bila kupitia cabinet.

Namuongelea Magufuli kwa sababu yeye ndiye rais sasa na watu wanamsifu kwa kuanzisha hili.

Obviously kuna wengine.
 
Magufuli aliupitisha kama Waziri, mikataba mikubwa haiwezi kupita bila kupitia cabinet.

Namuongelea Magufuli kwa sababu yeye ndiye rais sasa na watu wanamsifu kwa kuanzisha hili.

Obviously kuna wengine.
Hao wengine? TAJA MUANZILISHI wa hili li saga lote. MTAJE usipindepinde.
 
Hao wengine? TAJA MUANZILISHI wa hili li saga lote. MTAJE usipindepinde.
Kwa sasa tuanze na Magufuli anayejinadi anataka kupindua meza aliyoipanga mwenyewe, hapo pia kuna Mkapa na Kikwete na wote waliokuwa kwenye cabinets zilizopitisha.

Nipindepinde kwa sababu gani hasa?
 
Kaanduka Tundu Lissu haya maneno.

*MAJIBU YA LISSU KWA MAKADA WA CCM*

Khamnemba.

Na mimi ni Mtanzania pia.

Tofauti kati yangu mimi na wewe na Magufuli ni hii: Mimi nimepigania nchi yangu katika masuala haya tangu mwaka '99.

Wakati huo tulikuwa na mgodi mmoja tu wa dhahabu, Resolute Golden Pride Nzega. Bulyanhulu ilikuwa haijajengwa. Geita ndio kwanza walikuwa wanafukuza wanakijiji wa Mtakuja.

Nadhani nilikuwa wa kwanza katika nchi hii kupiga yowe kwamba tutaibiwa sana kwenye sekta ya madini.

Wewe sijui ulikuwa wapi wakati huo. Najua Magufuli alikuwa wapi: upande wa MaCCM na wawekezaji hawa.

Nimepigana na wawekezaji hawa mahakamani, kwenye medani ya kisiasa ndani na nje ya nchi hii kwa zaidi ya miaka 15. Nimetetea wananchi completely free of charge Bulyanhulu, Tarime, Nzega, Geita, n.k.

Sijui wewe ulikuwa wapi lakini najua Magufuli alikuwa upande wa nani: wa MaCCM na wanyonyaji hawa.

Soma Rai ya tarehe 17 Julai, 2001, uone tulimwambia nini Mkapa siku anaenda kuzindua Mgodi wa Bulyanhulu.

Sijui ulikuwa wapi lakini najua Magufuli alikuwa wapi: alikuwa anatetea tumbo lake na matumbo ya wanyonyaji hawa.

Nilikamatwa na kushtakiwa kwa uchochezi kwa sababu ya Bulyanhulu. Hiyo ilikuwa December 2002. Nilikaa na kesi hiyo mahakamani Kisutu kwa miaka sita.

Sijui ulikuwa wapi ila najua Magufuli alikuwa wapi: upande wa watesi wa wananchi na wanyonyaji wa rasilmali zetu.

Leo Magufuli anajifanya mzalendo na anahoji uzalendo we yeyote anayepingana nae.

Ni muongo. Anatafuta umaarufu wa kisiasa kwa wasiojua na wasiokumbuka. Ataupata. Kwa siku chache tu. Mark my words: ataumbuka na mtaumbuka.

Mimi ninampinga hadharani. Sio mnafiki, na sijahongwa. Ninampinga kwa sababu atatusababishia matatizo makubwa zaidi kuliko tuliyonayo sasa.

Huo mchanga atauachia upelekwe ambako umepelekwa kwa miaka 16 iliyopita. Kama sheria ndiyo hiyo na mikataba ndiyo hiyo hana pakwenda.

Tatizo ninaloliona ni kwamba by the time anawarudishia mchanga wao, Tanzania itakuwa imekuwa a basket case kama Zimbabwe.

Na tutakuwa tumelipishwa mapesa mengi kama fidia na arbitral tribunals za kimataifa kwa kuvunja mikataba na wawekezaji hawa.

Kama kuna anayefikiri uzalendo ni kufumbia macho masuala haya basi huyo na amuunge mkono Magufuli kwenye upofu wake wa kujitakia.

Ripoti ya Prof. Mruma haitamaliza hata nusu saa under serious scrutiny. Zaidi ya majina ya maprofesa walioiandaa, ripoti hii haina credibility yoyote. Ni kazi ya kisiasa iliyopakwa rangi ya usomi.

Kama umefuatilia taarifa za kitaalamu za Bulyanhulu hata kabla ya Barrick Gold kuingia mwaka '99 utajua ninasema nini.

Sutton Resources, Outukumpu Oy na hata STAMICO walishafanya utafiti mkubwa juu ya utajiri wa Bulyanhulu. Taarifa zipo na zimekuwepo kwa hata mbumbumbu wa jiolojia ya madini kama mimi.

Hiki alichoambiwa Magufuli ni rubbish, hata kama ni ya kiprofesa. Rubbish. Hatuibiwi kwenye mchanga, that's the rubbish fed on the unlettered.

Tunaibiwa kwenye sheria. Kama hamuoni hilo then God have mercy on us.
 
Kwa sasa tuanze na Magufuli anayejinadi anataka kupindua meza aliyoipanga mwenyewe, hapo pia kuna Mkapa na Kikwete na wote waliokuwa kwenye cabinets zilizopitisha.

Nipindepinde kwa sababu gani hasa?
Sasa umenena bila kumumnya maneno. Kwa sababu hiyo. PIGA reverse kidogo ya miaka kumiiliyopita TUTAWAPATA wahusika WAKUU na wahusika wadogo.
 
Sasa umenena bila kumumnya maneno. Kwa sababu hiyo. PIGA reverse kidogo ya miaka kumiiliyopita TUTAWAPATA wahusika WAKUU na wahusika wadogo.
Mi napiga reverse namhukumu mpaka character huyu anayeitwa Mungu.

Bilahuyu tusingepata "chaguo la Mungu" ba bila "chaguo la Mungu" tusingeachia ujinga huu.
 
Mi napiga reverse namhukumu mpaka character huyu anayeitwa Mungu.

Bilahuyu tusingepata "chaguo la Mungu" ba bila "chaguo la Mungu" tusingeachia ujinga huu.
Naomba tu kuwa TUSIMHUSISHE Mungu muumba wa Mbingu na nchi katika hili jambo. Yeye alipomaliza kuumba binadamu akawapa watu ndani yao THE WILL ya KUCHAGUA mema na MABAYA.
Basi kwa kila uamuzi unaufanya huwa ni wako wewe BINAFSI.Ikiwa basi wewe unamwamni Mungu wa kweli muhusishe.

Na kama huamini kama yuko bado ni HIARI yako kuchagua njia uipendayo maana yeye halazimishi.

Mfano mzuri ni kuwa Mungu huwa HATENGENEZI bunduki na silaha mbali mbali duniani zinazoua watu wengi VITANI? Vitu hivi vyote HUTENGENEZWA na ni BINADAMU yeye mwenyewe.

Mfano ukiamua kupanda GOROFANI ili URUKE ufe, bado utakufa na HATAKUZUIA your will ulivyokusudia.

Hivyo basi KUPANGA ni KUCHAGUA.
Mungu hahusiki na MATAMSHI wala MAAMUZI ya mtu binafsi.
 
Naomba tu kuwa TUSIMHUSISHE Mungu muumba wa Mbingu na nchi katika hili jambo. Yeye alipomaliza kuumba binadamu akawapa watu ndani yao THE WILL ya KUCHAGUA mema na MABAYA.
Basi kwa kila uamuzi unaufanya huwa ni wako wewe BINAFSI.Ikiwa basi wewe unamwamni Mungu wa kweli muhusishe.
Na kama huamini kama yuko bado ni HIARI yako kuchagua njia uipendayo maana yeye halazimishi.
Mfano mzuri ni kuwa Mungu huwa HATENGENEZI bunduki na silaha mbali mbali duniani zinazoua watu wengi VITANI? Vitu hivi vyote HUTENGENEZWA na ni BINADAMU yeye mwenyewe.
Mfano ukiamua kupanda GOROFANI ili URUKE ufe, bado utakufa na HATAKUZUIA your will ulivyokusudia.
Hivyo basi KUPANGA ni KUCHAGUA.
Mungu hahusiki na MATAMSHI wala MAAMUZI ya mtu binafsi. ya mtu binafsi.
Kwa nini kaumba ulimwengu ambao mabaya yanaweza kutokea wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezi kutokea?

Kama yupo at all?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom