Last emperor
JF-Expert Member
- Mar 22, 2015
- 10,346
- 9,881
Chama ni kikubwa sana,ni wazi alikuta mambo mengi ofisini ya kufanya.pia kwasababu hakuwepo kwenye circle ya uongozi wa chama kuna mabo mengi ya kujifunza,na sio aanze kukurupuka tu na kuanza kutoa matamshi magazetini ilimradi tu aonekane yupo.Binafsi ninamuamini sana Mbowe,ni mwanasiasa na mwana mikakati makini sana.Bila mbowe siasa za upinzani nchini zingekuwa zimekufa au za hovyo za kubweka tu magazetini na sio mikakati ya kuchukua nchi.Ushauri wangu mkubwa kabisa kwa katibu mkuu,yeye afanye kazi moja,kukijenga chama ngazi ya chini kabisa,kuhakikisha chama kina ofisi na watendaji kila kijiji/mtaa,kwasababu dr.slaa alikifikisha chama ngazi ya kata,yeye ashuke chini sasa,kijiji/mtaa mpaka vitongoji.Hasahasa vijijini,maana huko ndo ccm wanakopata kura nyingi.Ukishawamaliza ccm huko,basi.Kwa maneno mengine aanze maandalizi ya uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 sasa hivi.Zingatia haya...achana na siasa za magazetini na mbwembwe.Leta ushindi wa mitaa..tutakupima kwa hilo..numbers don't lie...