Katibu katibua au katibuliwa?

Katibu katibua au katibuliwa?

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,461
Reaction score
829,851
Mauaji mengine Tabata..mtoa taarifa anasema marehemu kajinyonga, lakini walinda sheria wamegoma hiyo sababu.. Ushahidi ni mwingi sana wa kumtia hatiani lakini kama kawa marehemu hana haki... Huyu si wa kwanza na hatakuwa wa mwisho

Mauaji haya ni mfululizo wa vifo vinavyohusiana na mapenzi.. Bado hatujapoa na kifo cha katibu.. Sio kata lakini na sio tawala! Katibu wa kiroho. Huyu kifo chake kimeacha maswali mengi kuliko majibu! Eti kaamua kujinyonga kisa penzi la mke wa mwajiri wake

Yaani mwizi kajisahau mpaka kajiona ana haki ya kuandika ujumbe mrefu mfano wa barua ya mahaba enzi zetu akililia penzi la wizi tena la mke wa boss? Hivi inaingia akilini kweli hii? Ndio maana nikasema katibu katibua ama katibuliwa!

Ujumbe ni mawasiliano ya wawili nani kavujisha mitandaoni? Mtajwa mtuhumiwa yuko kimya kabisa lakini si vema hapa kumhukumu kwa hili.. Mume ndio kakurupuka.. Haraka haraka hata kabla ya mazishi keshakimbilia mitandaoni na kutangaza msamaha kwa mkewe! Amekuwa na haraka kuliko upesi je analenga kuficha nini?

Aliyekufa ni mwajiriwa wake kwa cheo cha katibu lakini kukiwa na hizo habari za kuchepuka na mkewe halali wa ndoa..! Tuupe muda wakati ya sirini yanaweza kuwa bayana!

Tuliuanza mwaka tukizisoma hizi habari tangu January.. Ni wastani wa vifo viwili mpaka vitatu kwa mwezi, vingine vimevuma sana mitandaoni na vingine havikuvuma sana
Kuna waliua wake/wapenzi
Kuna walioua wake na watoto na wao wenyewe
Kuna waliouliwa wakigombea bibi
Kuna waliouana wakigombea bibi
Kuna waliotaka kuua wote wakafakiniwa mmoja au wote na wao kutoroka na kukamatwa ama kutoroka kusikojulikana

Hizi ni taarifa za,matukio ya vifo, bado zile za walioachwa
Waliojeruhiwa
Waliopata ulemavu wa kudumu nk.. Taarifa kuhusu talaka pia zinatisha sana!
Swami last kujiuliza tunakwenda wapi? Mamlaka na washika dau wako kimya kabisa... Ngoja mmoja wao liwatokee ndio watajitokeza kupaza sauti zao.. Na kwa mwendo huu December mbali

Jamii imeweka ufa na wanajamii..hakuna yoyote aliyeko tayari kwa yeyote walau kwa ushauri wa kujengana, kuonyana kufundishana, kuelekezana na kutiana moyo.. Hakuna nani wa kumshauri nani.. Wakushauri nao wanahitaji kushauriwa.. Wakushauriwa ama hawaamini katika ushauri ama hawazingatii ushauri

Mahusiano ya mwendokasi.. Simu janja ni ziraili wa kifo cha mwili na roho.. Ngoja wauane huko juu na huko mjengoni ndio tutasikia matamko na tume..kwasasa tuendelee kusubiri zamu ya mwingine.. Sijui atakuwa nani..!

December imeshafungua lango.. Katibu katibua ama katibuliwa?




IMG-20221003-WA0161.jpg
 
Lakini marehem alikua pisi🤔..

Anyway, on a serious note mzee wa kilinge, hiki suala la vifo mfuatano linahusishwa na mambo mengi lakini kuu hasahasa ni afya ya akili. Tukubali tukatae, kuna changamoto kubwa ya afya ya akili nchini kwetu na hii inatokana na ukweli kwamba malezi yetu hayafundishi vulnerability in any way.

Sisemi ni mabaya, lakn kutokana na utandawazi hali imekua mbaya zaidi.

Pia hali ngumu ya maisha ni changamoto nyingine. Kumekua na substandard kubwa sana recently ambayo yataka akili kubwa sana kuicircumnivigate.
 
Mbunye huwa IPO kama msumemo inakupiga kotekote inakupa furaha inakupa furaha na maumivu,hii INA apply kwa wote walioa na ambao hawajao.Ukiwa umeoa unapata utamu lakini vilevile unatafuta kwa jasho na kusalitiwa juu.

Uanaume mateso,labda huko mbinguni tutapata ahueni-hapa duniani tukubaliane tu kuzaliwa Mwanaume ni zaidi ya maumivu.
 
Na tatizo jingine tunalokabiliwa nalo kama nchi cases zote hizi zitaishia kuwa ni cold cases, police wetu nao ni suspects wa mauaji na hivi hatuna investigative foresinc dept, ukweli hautakuja kujulikana
Forensic ya nini,yani unitomb.a Mke wa mwenzio alitegemea apewe zawadi ama? Hiyo ndio zawadi.
 
😂😂 me kumchapa mtot tu siwezi cjui ata naonaje yaan je wife? Ivi hao wanaofikia hatua ya kuua wanakua na roho gan? Me wife ata anifanyie kosa gan sitonyanyua mkon wng kumpiga akizingua ni kumfukuza tu nyumban kwang bc hakuna namna nyengine
 
Back
Top Bottom