Katiba imekaa vizuri sana

Katiba imekaa vizuri sana

Nimeipitia katiba kipengere kwa kipengere.
Hakika imekaa vizuri sana. nimekuwa nikijiuliza wale wanaoipinga wanapinga kwa hoja zipi!!?
Ailimia kubwa mambo yaliyopendekezwa na tume ya Warioba yamo.
Eti kwa sababu tu kwamba serikali tatu haipo.
Asilimia kubwa ya watu wanaisoma kwa mrengo wa kuipinga. Hawako na free mind.

Kuna mambo mazuri sana mengi. Mfano:



Na kuna mambo mengi sana nitaendelea kuya toa.

Wewe pimbi unatakiwa kujua haki bila uwajibikiji ni 0 katibaa hii imetoa uwajibikiji kama tunu na viongozi hawaajibiki kabisa so sahau haya mambo ya kisiasa
 
Amir jeshi wa Tanzania ni nani? Je Rais wa Zanzibar anapigiwa mizinga kama nani? Sherehe za Mapinduzi nani anatangulia uwanjani?
Sasa mambo ya kupigiwa mizinga yako kwenye sheria sio kwenye katiba. Kumbuka hapa tunaongelea Katiba please tofautisha. Halafu mambo mengine ni ya itifaki tu sawa kaka. Jaribuni basi kupinga kwa hoja. Unaona sasa.
 
Wewe pimbi unatakiwa kujua haki bila uwajibikiji ni 0 katibaa hii imetoa uwajibikiji kama tunu na viongozi hawaajibiki kabisa so sahau haya mambo ya kisiasa
Mimi sijakuelewa. Hivi neno TUNU kwako lina maana gani?
Kwangu mimi najua Tunu ni zawadi spesho ambayo umebahatika kuwa nayo.
Hebu ngoja tuzitaje TUNU zilizo kwenye RASIMU ya Bunge:-
(a) lugha ya Kiswahili;
(b) Muungano;
(c) utu na udugu; na
(d) amani na utulivu.


Hebu niambie Uadilifu ni Zawadi?
 
Kwenye tatizo ni huko kwenye uongozi wa nchi. Kwa nini waliondoa vipengele muhimu kama wananchi kuwawajibisha wabunge na wanabunge kuwa watu wenye elimu ya form four? ndiyo maana bunge letu litaendelea kuwa substandard na lisilokuwa na viwango. Pia muundo huu wa muungano ni wa ovyo sana haijawai tokea. Kwa nini tusiwe na serikali moja au tatu ili muungano ueleweke? Sasa hivi Tanganyika inaminywa tu na wazanzibar wanadandia tu!
Hii katiba yetu huwezi kusimama hata kuilinganisha na katiba za nchi kama Kenya au SA au Ghana......haina viwango na ni ya kuundwa kimagendo kwa maslahi ya chama kimoja! Huu mpasuko wa kisiasa uliojitokeza lazima utaadhiri utekelezwaji wa katiba mpya pindi itakapokubaliwa na wananchi. Ila CCM kwa vile wanadhani watabaki madarakani milele, ndio maana wamepitisha katiba ya ovyo kama hii! Katiba inafaaa kuwa chama chochote kikishika dola kinaridhika na muundo wa serikali uliopo na si vinginevyo!


Kwa nini ulinganishe na Nchi hizo?
Hujui kuwa UNITED Countris in Africa ni moja tu.
Duniani hazizidi Tano?
Nimejaribu kuweka vipengere vingi tu, vilivyo sahihishwa na kutoa vitu ambavyo vinabadilika.
Huwezi ukaweka maelezo marefu ya miiko ya watumishi wa umma kwenye katiba. sasa sheria zitafanya nini?
Huwezi ukaelezea kila kitu kwenye katiba ila katiba itatoa mwelekeo, kama hii ya sasa.
 
misingi ya utawala bora
6.-(1) katika utekelezaji wa mamlaka au shughuli zozote kwa mujibu
wa katiba hii au sheria za nchi, misingi ya utawala bora katika ibara hii ni
lazima izingatiwe na kufuatwa na taasisi ya serikali, ofisa wa serikali au mtu
yeyote aliyepewa dhamana ya:
(a) kutumia au kutafsiri katiba hii;
(b) kutunga, kutumia au kutafsiri sheria yoyote; na
(c) kufanya au kutekeleza maamuzi ya sera za kitaifa.
(2) misingi ya utawala bora katika jamhuri ya muungano itajumuisha:
(a) uadilifu;
(b) demokrasia;
(c) uwajibikaji;
(d) utawala wa sheria;
(e) ushirikishwaji wa wananchi;
(f) haki za binadamu;
(g) usawa wa jinsia;
(h) umoja wa kitaifa;
(i) uwazi; na
(j) uzalendo.
 
Kwa nini ulinganishe na Nchi hizo?
Hujui kuwa UNITED Countris in Africa ni moja tu.
Duniani hazizidi Tano?
Nimejaribu kuweka vipengere vingi tu, vilivyo sahihishwa na kutoa vitu ambavyo vinabadilika.
Huwezi ukaweka maelezo marefu ya miiko ya watumishi wa umma kwenye katiba. sasa sheria zitafanya nini?
Huwezi ukaelezea kila kitu kwenye katiba ila katiba itatoa mwelekeo, kama hii ya sasa.
Akishika dola CHADEMA au CUF au UKAWA wanavyojiita huoni kama kutakuwa na crisis? Lazima wataifanyia hiyo katiba fundamental changes na hiyo itakuwa katiba gani inayobadilishwa ovyo? Angalia nchi kama marekani akishika huyu au yule huwezi kubadilisha muundo wa serikali lakini hapa kila mtu ana lake kwa vile hakuna maridhiano kwa sababu CCM hakikusikiliza sauti za vyama vya upinzani
Pili, hamjajifundisha chochote kutokana na kura ya maoni ya scotland? Sasa hivi England wanalalamika wabunge wa scotland iweje wanajadili mambo yasiyowahusu. Huo ni muungano wa zaidi ya miaka 300. lakini it was inevitable. na hapa pia mpende msipende lazima Tanganyika itadai haki yake at some point, iwe sa hivi au baadaye tukiwa hatupo, iwe kwa amani au fujo. Lakini CCM hamjali vizazi vijavyo mnachokiona ni hapa na sasa hivi na vitambi vyenu.
 
Akishika dola CHADEMA au CUF au UKAWA wanavyojiita huoni kama kutakuwa na crisis? Lazima wataifanyia hiyo katiba fundamental changes na hiyo itakuwa katiba gani inayobadilishwa ovyo? Angalia nchi kama marekani akishika huyu au yule huwezi kubadilisha muundo wa serikali lakini hapa kila mtu ana lake kwa vile hakuna maridhiano kwa sababu CCM hakikusikiliza sauti za vyama vya upinzani
Tatizo lako ndugu yangu unacomment tuuuuuuu. Hutoi ni vipengere vipi vitakavyo badilishwa? Sijui hata kama umeisoma hii Rasimu.Hebu nakuomba tujadili pointi kwa point. Niambie kifungu kipi kinacho weza kubadilishwa kwenye katiba wakiingia hao unaowasema?
 
Uhuru wa taaluma, ubunifu, ugunduzi na usanii

56.-(1) Kila mtu atakuwa na uhuru wa kushiriki kwenye mambo
yanayoendeleza na kukuza sanaa, taaluma, ubunifu na ugunduzi.
(2) Kila mtu atakuwa na uhuru wa kujifunza, kufundisha, kutafiti na
kueneza matumizi ya matokeo ya utafiti kulingana na kanuni za kitaaluma na za
kiutafiti.
(3) Serikali itakuza na kuendeleza utafiti, ubunifu na ugunduzi katika
sanaa, sayansi na teknolojia kwa kutunga sheria ambazo:
(a) zitalinda hakimiliki na hataza na haki za wabunifu, watafiti na
wasanii;
(b) zitawezesha taasisi za elimu na za utafiti kutumia ugunduzi wao kwa
manufaa ya taifa;
(c) zitasimamia uhamishaji wa sayansi na teknolojia;
(d) zitawezesha kukuza rasilimali watu kwenye nyanja za kitaaluma,
sayansi, teknolojia na ubunifu;
(e) zitalinda na kusimamia ubora wa taaluma, utafiti na matumizi ya
ugunduzi na ubunifu; na
(f) zitafafanua mambo mengine yanayohusu hakimiliki na hataza.
 
Akishika dola CHADEMA au CUF au UKAWA wanavyojiita huoni kama kutakuwa na crisis? Lazima wataifanyia hiyo katiba fundamental changes na hiyo itakuwa katiba gani inayobadilishwa ovyo? Angalia nchi kama marekani akishika huyu au yule huwezi kubadilisha muundo wa serikali lakini hapa kila mtu ana lake kwa vile hakuna maridhiano kwa sababu CCM hakikusikiliza sauti za vyama vya upinzani
Pili, hamjajifundisha chochote kutokana na kura ya maoni ya scotland? Sasa hivi England wanalalamika wabunge wa scotland iweje wanajadili mambo yasiyowahusu. Huo ni muungano wa zaidi ya miaka 300. lakini it was inevitable. na hapa pia mpende msipende lazima Tanganyika itadai haki yake at some point, iwe sa hivi au baadaye tukiwa hatupo, iwe kwa amani au fujo. Lakini CCM hamjali vizazi vijavyo mnachokiona ni hapa na sasa hivi na vitambi vyenu.

Kwahiyo hapa hoja ya UKAWA ni serikali 3, mambo mengine ya wananchi wao hayawahusu.
 
Tatizo lako ndugu yangu unacomment tuuuuuuu. Hutoi ni vipengere vipi vitakavyo badilishwa? Sijui hata kama umeisoma hii Rasimu.Hebu nakuomba tujadili pointi kwa point. Niambie kifungu kipi kinacho weza kubadilishwa kwenye katiba wakiingia hao unaowasema?

Unataka nikuwekee sura nzima ya saba hapa? Inaanza hivi;
SURA YA SABA
MUUNDO WA JAMHURI YA MUUNGANO
Muundo wa Muungano
70. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itakuwa na muundo wa Serikali
mbili ambazo ni:
(a) Serikali ya Jamhuri ya Muungano; na
(b) Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Ukibadilisha hapo umeshaibadilisha katiba nzima maanake msingi wa katiba ni muundo wa muungano. Hii katiba tunayo wote na nakuhakikishia kwamba nimeisoma mara mbili juu chini!
 
Unataka nikuwekee sura nzima ya saba hapa? Inaanza hivi;
SURA YA SABA
MUUNDO WA JAMHURI YA MUUNGANO
Muundo wa Muungano
70. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itakuwa na muundo wa Serikali
mbili ambazo ni:
(a) Serikali ya Jamhuri ya Muungano; na
(b) Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Ukibadilisha hapo umeshaibadilisha katiba nzima maanake msingi wa katiba ni muundo wa muungano. Hii katiba tunayo wote na nakuhakikishia kwamba nimeisoma mara mbili juu chini!

OK. Sasa wewe ulikuwa unataka Serikali tatu au moja au ya mkataba?
Ukotayari kujifunza mantiki ya serikali mbili?
Hebu soma vipengere vyote.
Halafu hebu niambie nitatizo gani kuwa na serikali mbili?
Kwasababu katika mantiki yako ya serikali tatu inatekelezwa kwa kuwa na makamu watatu wa rais
1. Makamu wa kwanza ndiye aliye na mamlaka kote
2. Makamu wa pili wa raisi ndiye Raisi wa zanzibar.
3 Makamu wa tatu wa rais ndiye mtendaji mkuu wa serikali kwa mantiki hiyo ndiye msimamizi wa mambo ya Muungano na mambo yote ya Tanzania bara.


Halafu ikumbukwe Makamu wa kwanza wa rais na makamu wa tatu wa rais wanasifa ya kuwa marais wa JMT ikitokea rais hayupo.

Serikali, Mahakama na Bunge vimetenganishwa.
Katika Rasimu ya pili Jaji na Spika walikuwa na uwezo wa kuwa Rais.

Huoni ingeleta mgongano wa maslahi. Maana Spika anaweza akashirikiana na wabinge au vyoyote kumuondoa rais.
Na ikubukwe kwenye Rasimu hii ya mwisho wabunge wanao uwezo wa kumuondoa rais madarakani.

Sijui umeelewa!!!!
 
Angalia hapa tena.


Mbona mkalia kutuambia masuala ya haki za wavuvi ,wakulima,wafugaji kwa nini hamsemi kama mbuge anaruhusiwa kugombea mpaka atakapochoka yeye! Mtu anayejua kusoma na kuandika anaweza kuwa mbuge determination ya mtu anayejua kusoma na kuandika unaijuaje? Manake hata STD VII wanamaliza hawajui kusoma na kuandika?kwa nini mumewaondolea wananchi mamlaka ya kumwajibisha Rais? Mmesema idadi ya wabunge ktk bunge iwe 50 kwa 50 bila hata kuonesha hyo inapatikanaje nakwambia hvi hii katiba endapo itapita mungu nijalie uzima ktk kipindi cha miaka 10 tu itafanyiwa amendment kwanza hatutakuwa na wazee kama wewe Bungeni
 
Mbona mkalia kutuambia masuala ya haki za wavuvi ,wakulima,wafugaji kwa nini hamsemi kama mbuge anaruhusiwa kugombea mpaka atakapochoka yeye! Mtu anayejua kusoma na kuandika anaweza kuwa mbuge determination ya mtu anayejua kusoma na kuandika unaijuaje? Manake hata STD VII wanamaliza hawajui kusoma na kuandika?kwa nini mumewaondolea wananchi mamlaka ya kumwajibisha Rais? Mmesema idadi ya wabunge ktk bunge iwe 50 kwa 50 bila hata kuonesha hyo inapatikanaje nakwambia hvi hii katiba endapo itapita mungu nijalie uzima ktk kipindi cha miaka 10 tu itafanyiwa amendment kwanza hatutakuwa na wazee kama wewe Bungeni

Sorry kumwajibisha mbuge
 
Kwahiyo hapa hoja ya UKAWA ni serikali 3, mambo mengine ya wananchi wao hayawahusu.
Hayo mambo yote ya wananchi bado yangepatikana iwe kwa serikali moja, mbili au tatu. Hiyo tu ni danganya toto ambayo CCM wanaitumia kuwahadaa wananchi kama wewe. Hivi unadhani kwa serikali tatu 50/50 ya wanawake isingepatikana? Au mambo ya wakulima, wavuvi, wachimba madini na kadhalika yasingezingatiwa? Mambo hayo yanatekelezeka kwa muundo wowote wa serikali kwa hiyo hoja yako haina mashiko!
 
Mbona mkalia kutuambia masuala ya haki za wavuvi ,wakulima,wafugaji kwa nini hamsemi kama mbuge anaruhusiwa kugombea mpaka atakapochoka yeye! Mtu anayejua kusoma na kuandika anaweza kuwa mbuge determination ya mtu anayejua kusoma na kuandika unaijuaje? Manake hata STD VII wanamaliza hawajui kusoma na kuandika?kwa nini mumewaondolea wananchi mamlaka ya kumwajibisha Rais? Mmesema idadi ya wabunge ktk bunge iwe 50 kwa 50 bila hata kuonesha hyo inapatikanaje nakwambia hvi hii katiba endapo itapita mungu nijalie uzima ktk kipindi cha miaka 10 tu itafanyiwa amendment kwanza hatutakuwa na wazee kama wewe Bungeni

Kwajinsi ulivyo comment unaonekana hujaisoma hii rasimu. Nakuomba nivyema ukaisoma badala ya kuleta bra bra hapa. hebu nipe kifungu kinachosema mbunge asiwe na kikomo.
 
Hayo mambo yote ya wananchi bado yangepatikana iwe kwa serikali moja, mbili au tatu. Hiyo tu ni danganya toto ambayo CCM wanaitumia kuwahadaa wananchi kama wewe. Hivi unadhani kwa serikali tatu 50/50 ya wanawake isingepatikana? Au mambo ya wakulima, wavuvi, wachimba madini na kadhalika yasingezingatiwa? Mambo hayo yanatekelezeka kwa muundo wowote wa serikali kwa hiyo hoja yako haina mashiko!

Katiba ya warioba haikusema hayo.
Nakuomba ndugu unijibu maswali yangu mengi tu nimekuuliza unayakwepa kwepa tu.
 
Kwajinsi ulivyo comment unaonekana hujaisoma hii rasimu. Nakuomba nivyema ukaisoma badala ya kuleta bra bra hapa. hebu nipe kifungu kinachosema mbunge asiwe na kikomo.

Sio kifungu ni ibara vifungu vinaaply ktk acts eg Public service act no 8 of 2002 dk 2 nakuletea
 
Katiba ya warioba haikusema hayo.
Nakuomba ndugu unijibu maswali yangu mengi tu nimekuuliza unayakwepa kwepa tu.
Katiba ya warioba haingeongelea mambo hayo kwa sababu kwenye mfumo wa serikali tatu, hayo siyo mambo ya muungano! Hayo mambo yote yangetajwa kwenye katiba ya Tanganyika na katiba ya Zanzibar. CCM wamewatupia changa la macho tena wananchi kama wewe kwa kuwaambia eti mzisome rasimu zote mbili mzilinganishe wakati siyo sahihi kufanya hivyo! Ya warioba ilijikita kwenye yale mambo ya muungano tu! Mambo ya ardhi, vijana, wakulima, wavuvi na kadhalika yote yangetajwa kwenye katiba za nchi washirika. Sijui umeelewa?!
Umeniuliza swali moja tu nalo ni 'Kwahiyo hapa hoja ya UKAWA ni serikali 3, mambo mengine ya wananchi wao hayawahusu.' Naamini nimekujibu vilivyo!
 
Back
Top Bottom