LiverpoolFC
JF-Expert Member
- Apr 12, 2011
- 11,496
- 3,388
Annael
Kazi yako umefikisha sassa nenda kachukue chako lumumba!
Kazi yako umefikisha sassa nenda kachukue chako lumumba!
Sasa wewe tatizo lako ni nini? maana umetoka nje ya pointi kabisa. Umeenda nje ya key.
41. Kila mtu anastahili kuwa huru bila kuathiri sheria za nchi, kukutana
na watu wengine kwa hiari yake na kwa amani, kujumuika na kushirikiana na
watu wengine, kutoa mawazo hadharani, na kwa ajili hiyo kuanzisha au
kujiunga na vyama au mashirika yaliyoanzishwa kwa madhumuni ya kuhifadhi
au kuendeleza imani au maslahi yake au maslahi mengineyo.
Ardhi siyo ishu ya muungano mamdogo, wamekukaririsha vibaya. Mzanzibar akija bara ana uwezo wa kumilikishwa ardhi lakini mtanganyika akienda Zanzibar haruhisiwi kumiliki ardhi kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar. Sasa unakurupuka tu kulete ushabiki usiokua na tija, acheni unafiki kama mnanufaika na mfumo kuweni wawazi tu.
25. Maliasili zote za Taifa ikiwa ni pamoja na madini, gesi na mafuta ni
mali ya umma, na Serikali ya Jamhuri ya Muungano au Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar itaweka utaratibu wa kuhakikisha zinatumika kwa manufaa ya
kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
23. Bunge litatunga sheria itakayoweka masharti kuhusu mgawanyo wa
matumizi bora ya ardhi kwa makundi mbalimbali ya jamii.
toa ututsi wako wewe..huna adabu. kama kawaida yenu mnajidai tu. hii ndio dharau gani? fisi wewe.... Toa Hiyo Toilet Pepa Yenu.! Inanuka
Rwanda siku hizi kuna CCM?
.... Yaani Unasukuma Maji Yaingie Kwenye Jiwe, Yaan Zanzbar Ijitegemee Mambo Yasiyo Ya Muungano? Tanganyika Ndo Iwe Serikali Ya Muungano? Hahahahaaa.! Hivi Vituko Kweli.!!
17.-(1) Kutakuwa na Dira ya Taifa ya Maendeleo katika nyanja
mbalimbali kwa kuzingatia haki na wajibu wa kila raia kupata maendeleo.
(2) Katika kutekeleza ibara ndogo ya (1), Mamlaka za Serikali zitaweka
mipango ya kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo.
15.-(1) Lengo la Katiba hii kiutamaduni ni kukuza, kudumisha na
kuhifadhi lugha ya Kiswahili, urithi wa asili na utamaduni wa wananchi.
(2) Katika kuhakikisha utekelezaji wa lengo hilo, Serikali itachukua
hatua zinazofaa ili:
(a) kulinda na kuendeleza lugha ya Kiswahili;
(b) kulinda na kuhifadhi urithi wa asili, malikale na sehemu zenye
umuhimu wa kihistoria ili kuepuka uharibifu, wizi au utoroshaji nje
ya nchi;
(c) kulinda, kuhifadhi na kuendeleza utamaduni wa jamii mbalimbali;
(d) kujenga utamaduni wa kuwepo ushirikiano, maelewano,
maridhiano, uvumilivu na kuheshimu mila, desturi na imani ya dini
ya kila mtu; na
(e) kuweka mazingira yatakayowezesha wasanii kutumia fursa zilizopo
na vipaji vyao katika kuleta maendeleo ya kiuchumi na mabadiliko
katika jamii.
Nimeipitia katiba kipengere kwa kipengere.
Hakika imekaa vizuri sana. nimekuwa nikijiuliza wale wanaoipinga wanapinga kwa hoja zipi!!?
Ailimia kubwa mambo yaliyopendekezwa na tume ya Warioba yamo.
Eti kwa sababu tu kwamba serikali tatu haipo.
Asilimia kubwa ya watu wanaisoma kwa mrengo wa kuipinga. Hawako na free mind.
Kuna mambo mazuri sana mengi. Mfano:
Na kuna mambo mengi sana nitaendelea kuya toa.
Kwa tafsiri yako mtu mzalendo yukoje? anatakiwa afanye nini?
Hebu nipe tafsiri....
Basi tulia uachane na mambo yetu. Endelea na ya kwenu.