Katiba imekaa vizuri sana

Katiba imekaa vizuri sana

Raisi kapewa mamlaka makubwa yakuteua mpaka kuku sasa ndo kukaa vzur uko? Tume huru ya uchaguzi haiwez kuteuliwa na raisi isome tena vzur
Tatizo we mjinga unawaza madaraka tu kwa mfano Rais asipoteua kabisa nafasi zote zikapatikana kwa njia zingine sisi wananchi wa kawaida inatusaidia nini,hapa jamno la msingi tunaangalia kama mambo yanayolenga wananchi wa kawaida moja kwa moja yamo au hayamo ndiyo jambo la msingi kiukweli katiba ipo vizuri sana.
 
... Mkuu, Huyo Jamaa Atakuwa Kada Wa Ccm, Anajaribu Aone Kama Takataka Yao Inakubarika Au La
Halafu wewe mnyarwanda mambo ya tanzania wewe yanakuhusu nini kama siyo kuchafua nchi yetu bure hebu fuata yenu.
 
Ulinzi na usalama
259.-(1) Vyombo vya ulinzi na usalama wa Taifa vitakuwa ni:
(a) Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania;
(b) Jeshi la Polisi la Jamhuri ya Muungano; na
(c) Idara ya Usalama wa Taifa.
(2) Wajibu wa vyombo vya ulinzi na usalama wa Taifa na mfumo wa
usalama ni kulinda mipaka ya Jamhuri ya Muungano, rasilimali za nchi, maslahi
ya raia na watu wengine, mali zao, haki na uhuru, mamlaka za nchi, amani na
umoja wa kitaifa.
(3) Katika utekelezaji wa majukumu yao, vyombo vya ulinzi na usalama
wa Taifa na kila mtumishi wa vyombo hivyo hataruhusiwa:
(a) kuwa na upendeleo kwa njia yoyote;
(b) kujiunga na chama chochote cha siasa au kuendeleza maslahi ya
chama chochote cha siasa au sera zake;
(c) kuhujumu maslahi ya kisiasa au mpango wa kisiasa ambao ni halali
chini ya Katiba hii;
(d) kutishia, kudhulumu au kuwatendea ukatili raia na watu wengine; na
(e) kutii amri yoyote isiyokuwa halali.
(4) Mtu hataruhusiwa kuanzisha taasisi, kampuni, jumuiya au shirika
linalohusiana na ulinzi na usalama wa Taifa au ushirika wa kijeshi, isipokuwa
kama inavyoruhusiwa na Katiba hii au sheria.
(5) Vyombo vya ulinzi na usalama wa Taifa vitakuwa chini ya mamlaka
ya Amiri Jeshi Mkuu.
(6) Bunge litatunga sheria kuweka masharti kuhusu utekelezaji wa
majukumu, uratibu na usimamizi wa vyombo vya ulinzi na usalama wa Taifa.


 
Mambo ya Muungano haya hapa

1. Katiba na Mamlaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
2. Ulinzi na usalama wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
3. Usalama na usafiri wa anga.
4. Uraia na uhamiaji.
5. Jeshi la Polisi.
6. Sarafu na Benki Kuu.
7. Kodi ya Mapato inayolipwa na watu binafsi na Mashirika, ushuru wa forodha na ushuru
wa bidhaa zinazotengenezwa nchini Tanzania na zinazosimamiwa na Idara ya Forodha.
8. Mambo ya nje.
9. Usajili wa vyama vya siasa.
10. Mahakama ya Juu na Mahakama ya Rufani.
11. Elimu ya Juu.
12. Baraza la Taifa la Mitihani na mambo yote yanayohusika na kazi za Baraza hilo.
13. Utabiri wa hali ya hewa.
14. Utumishi katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano.

 
Hapo ndio unapo shindwa kuelewa mantiki ya katiba hii. Ngoja nikukumbushe kitu kimoja tu.
Zanzibar itajishughulisha na mambo yasiyo ya Muungano yanayo husu zanzibar. Lakini JMT itajihusisha na mambo yote ya Tanzania bara na mambo yote ya Muungano. Get the point?

.... Yaani Unasukuma Maji Yaingie Kwenye Jiwe, Yaan Zanzbar Ijitegemee Mambo Yasiyo Ya Muungano? Tanganyika Ndo Iwe Serikali Ya Muungano? Hahahahaaa.! Hivi Vituko Kweli.!!
 
Hapo ndio unapo shindwa kuelewa mantiki ya katiba hii. Ngoja nikukumbushe kitu kimoja tu.
Zanzibar itajishughulisha na mambo yasiyo ya Muungano yanayo husu zanzibar. Lakini JMT itajihusisha na mambo yote ya Tanzania bara na mambo yote ya Muungano. Get the point?
Yaani wewe kiazi tu, kama mama ni mtanganyika nenda znz leo upeleke maombi ya kununua ardhi uone kama utamilikishwa.
 
Halafu wewe mnyarwanda mambo ya tanzania wewe yanakuhusu nini kama siyo kuchafua nchi yetu bure hebu fuata yenu.

.... Hata Wanyarwanda Ni Wenzetu Tu, Mbona Wewe Ni Mkongoman Hatusemi.! Hii Ni Nchi Yetu Wote
 
.... Yaani Unasukuma Maji Yaingie Kwenye Jiwe, Yaan Zanzbar Ijitegemee Mambo Yasiyo Ya Muungano? Tanganyika Ndo Iwe Serikali Ya Muungano? Hahahahaaa.! Hivi Vituko Kweli.!!
wewe ni mnyarwanda mambo ya TZ hayakuhusu na ni vigumu wewe kuyaelewa. Wewe endelea tu na kanchi kako hako. Tunawaheshimu na hata kwenye katiba inasema kuheshimu uhuru wa nchi zingine. Ya kwenu hayatuhusu.
 
... Mkuu, Huyo Jamaa Atakuwa Kada Wa Ccm, Anajaribu Aone Kama Takataka Yao Inakubarika Au La
Halafu nafikiri huyo jamaa ni mgumba maana angekuwa na watoto angefikiria maisha yao baada ya yeye kwenda kaburini,
 
Yaani wewe kiazi tu, kama mama ni mtanganyika nenda znz leo upeleke maombi ya kununua ardhi uone kama utamilikishwa.
Sasa wewe tatizo lako ni nini? maana umetoka nje ya pointi kabisa. Umeenda nje ya key.
 
Yaani wewe kiazi tu, kama mama ni mtanganyika nenda znz leo upeleke maombi ya kununua ardhi uone kama utamilikishwa.

... Mkuu, Tanzania Kazi Tunayo, Ona Hilo Jamaa Halijui Linachokiandika, Linaendekeza Ushabiki Tu. Mbona Mim Ni Ccm Damu Lakin Naona Hamna Kitu Kwenye Hiyo Takataka
 
Halafu nafikiri huyo jamaa ni mgumba maana angekuwa na watoto angefikiria maisha yao baada ya yeye kwenda kaburini,
Ongelea katiba na pointi kwa point sio kuleta porojo hapa. Tao ibara ipi unaipinga kwanini. Sio kutoa bra bra tu.
 
Umesharudi toka Dodoma? Upambafu mloufanya mnaona hautoshi bado umatuletea hapa JF. Itisha mikutano na ccm wenzako ndo muongee huo uchafu wenu mmekosa hata aibu. Mijizi sugu!
 
... Mkuu, Tanzania Kazi Tunayo, Ona Hilo Jamaa Halijui Linachokiandika, Linaendekeza Ushabiki Tu. Mbona Mim Ni Ccm Damu Lakin Naona Hamna Kitu Kwenye Hiyo Takataka
Rwanda siku hizi kuna CCM?
 
Hivi wewe akili unazo kweli? Nikiuliza kwanini unanitukana utakuwa na jibu?
Acha bana mambo hayo ni ya watoto. Kwani unataka nifuate unayotaka wewe?

... Unaandika Na Kushabikia Utumbo, Na Utatukanwa Tu.!
 
1. Makamu wa kwanza ndiye mgombea mwenza wa rais
2. Makamu wa pili ni Rais wa Zanzibar
3. Makamu wa tatu ni waziri mkuu.

Unaielewa mantiki yake?

Kuna kipengele kinachokataza Waziri mkuu kutoka Zanzibar? Maana Waziri mkuu atapendekezwa na Rais kutoka katika chama chenye wabunge wengi. Jee Rais akitoka Zanzibar na akamteua Mbunge wa Makunduchi kuwa Waziri mkuu itakuwaje?
Nikusaidie, Rais Mzazibar, makamu wa pili Mzanzibari na Makamu wa tatu ( waziri mkuu) Mzanzibari wapi Tanganyika hapo?
 
Lugha ya Taifa
4.-(1) Lugha ya Taifa ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni
Kiswahili na itatumika katika mawasiliano rasmi ya kitaifa na kiserikali.
(2) Bila kuathiri masharti ya ibara ndogo ya (1), lugha ya Kiingereza au
lugha nyingine yoyote ya kimataifa inaweza kutumika kama lugha rasmi ya
mawasiliano ya kiserikali, pale itakapohitajika.
(3) Kwa mujibu wa Ibara hii, lugha ya alama kwa viziwi na lugha ya
alama mguso kwa viziwi wasioona, zitakuwa lugha rasmi za mawasiliano.
(4) Serikali itaweka mazingira yatakayowezesha kuwepo kwa
mawasiliano mbadala zikiwemo lugha ya alama, lugha ya alama mguso,
maandishi yaliyokuzwa na nukta nundu kwenye sehemu muhimu za umma na
katika vyombo vya habari vinavyotangaza habari zake kitaifa kwa ajili ya watu
wenye ulemavu.
 
wewe ni mnyarwanda mambo ya TZ hayakuhusu na ni vigumu wewe kuyaelewa. Wewe endelea tu na kanchi kako hako. Tunawaheshimu na hata kwenye katiba inasema kuheshimu uhuru wa nchi zingine. Ya kwenu hayatuhusu.

.... Tena Wewe Ni Muganda. Ulikimbia Vita Ya Idd Amin, Rudi Kwenu Huko
 
Mwekezaji atakuwa na haki ya kutumia ardhi" hapo ndipo mtego ulipo,mbona haielezi kinagaubaga?, ni sheria ya kulinda wawekezaji na kuwafukuza wananchi.Hiyo ni geresha tu

Hebu soma kwa makini ibara 22 kifungu 2 hapa chini:-



(a) raia wa Tanzania pekee ndiye atakayekuwa na haki ya kumiliki
ardhi ya Tanzania, na haki hiyo italindwa kwa mujibu wa Katiba hii;
(b) mtu ambaye siyo raia wa Tanzania atakuwa na fursa ya kutumia
ardhi kwa ajili ya uwekezaji na maendeleo mengine ya kiuchumi na
makaazi;
(c) haki ya kumiliki, kuendeleza na kuhifadhi ardhi kwa ajili ya
makundi mbalimbali ya jamii wakiwemo wakulima, wavuvi,
wafugaji na makundi madogo itatambuliwa na kulindwa kwa mujibu
wa Ibara hii; na
(d) kila mwanamke atakuwa na haki ya kupata, kumiliki, kutumia,
kuendeleza na kusimamia ardhi kwa masharti yaleyale kama ilivyo
kwa mwanaume.
 
Back
Top Bottom