Emc2
JF-Expert Member
- Sep 26, 2011
- 16,808
- 16,951
- Thread starter
- #61
Japo kuwa umeandika kwa mwandiko mdogo sana hebu soma Ibara 28 kifungu cha 2Hii ndiyo ilikuwa rasimu ya ukweli. Soma kwa makini utagundua kuwa unaongozwa kwa ushabiki zaidi.
(2) Kwa madhumuni ya Katiba hii, Bunge litatunga sheria
itakayoweka, pamoja na mambo mengine-
(a) tafsiri ya neno zawadi, aina, thamani, kiwango na uhifadhi wa
zawadi za Jamhuri ya Muungano;
(b) masharti ya kufungua akaunti za nje kwa kiongozi wa umma;
(c) masharti ya kumtaka kiongozi wa umma kutoa tamko la mali na
thamani yake, madeni yake pamoja na ya mwenza wake wa ndoa;
(d) masharti ya kuzuia kiongozi wa umma kutoshiriki kufanya
uamuzi wa jambo au shughuli yoyote ambayo ana maslahi nayo
yeye binafsi, mwenza wake wa ndoa, mtoto wake, jamaa au rafiki
yake au mtu yeyote wa karibu;
(e) masharti ya matumizi ya mali ya umma;
(f) utaratibu wa utwaaji wa mali za kiongozi wa umma
zinazopatikana kwa kukiuka sheria;
(g) utaratibu wa kumwajibisha kiongozi wa umma aliyekiuka maadili
na miiko ya uongozi wa umma;
(h) uanzishaji wa mitaala inayohusu Katiba, maadili na uraia, shuleni
na vyuoni; na
(i) mambo yasiyotakiwa kwa watumishi wa umma.
(3) Wadhifa wa "kiongozi wa umma" kama ulivyotumika katika
Sehemu hii utajumuisha kiongozi wa kuchaguliwa au kuteuliwa kama
itakavyoainishwa kwenye sheria za nchi.
Angalia na hapa
29.-(1) Bila kuathiri masharti ya Katiba hii, kiongozi wa umma
ataheshimu na kutii maadili ya uongozi wa umma na miiko ya uongozi.
(2) Bunge litatunga sheria itakayoainisha:
(a) miiko inayopaswa kuzingatiwa na viongozi wa umma;
(b) utaratibu wa kumuondoa kazini kiongozi wa umma kutokana na
kuvunja miiko na kukiuka maadili ya uongozi wa umma;
(c) vitendo ambavyo Kiongozi wa umma hapaswi kuvitenda; na
(d) ngazi au orodha ya viongozi wa umma wanaofungwa na Ibara hii.