Emc2
JF-Expert Member
- Sep 26, 2011
- 16,808
- 16,951
- Thread starter
- #121
Haki za wanawake
57. Kila mwanamke ana haki ya:
(a) kuheshimiwa, kuthaminiwa na kutambuliwa utu wake;
(b) kulindwa dhidi ya ubaguzi, udhalilishaji, dhuluma, unyanyasaji, ukatili wa kijinsia na mila potofu;
(c) kushiriki bila ya ubaguzi katika uchaguzi na ngazi zote za maamuzi;
(d) kupata fursa na ujira sawa na mwanaume katika kazi zenye sifa zinazofanana;
(e) kulindwa ajira yake wakati wa ujauzito na pale anapojifungua;
(f) kupata huduma bora ya afya ikiwemo afya ya uzazi salama; na
(g) kumiliki mali.