Kati ya PF3 na uhai wa mtu kipi bora?

Kati ya PF3 na uhai wa mtu kipi bora?

Sun is Sun

JF-Expert Member
Joined
Mar 13, 2024
Posts
1,152
Reaction score
1,696
Habari zenu?

Swali hili nalielekeza kwa Wana-taaluma wa afya Madaktari, Manesi.... Je, uhai na PF3 kipi kina umuhimu zaidi, kuna case mbalimbali ambazo waliokumbwa na kadhia za ajali kuchelewesha huduma, na wengine kupoteza maisha kabisa kwa kigezo cha kuhitajika PF3 kwanza.

Kingine nawachana Madaktari na Manesi, sio kwamba ninyi pekee mliosoma zaidi, wengine mmefaulu kwa kuungaunga na wengi wa Manesi pamoja na Clinical Officers form four walikuwa na D-TATU.

Narudia tena wengi wenu mna elimu za kawaida, na course zenu sio special.

Nimemaliza.
 
Hospital zinazofanya hivyo zinaenda kinyume na haki za binadamu, hauna budi kuripoti .
 
Kuna haja ya hizo PF—3 Zitolewe hapo hapo hospitali. Kuna wale askari wanaokuwa kwenye kata husika inatakiwa wawe na ofisi zao kwenye hospitali za rufaa ama mkoa, wilaya ili watu wasikumbwe na adha ya kunyimwa huduma kisa hizo PF3.
 
Habari zenu?

Swali hili nalielekeza kwa Wana-taaluma wa afya Madaktari, Manesi.... Je, uhai na PF3 kipi kina umuhimu zaidi, kuna case mbalimbali ambazo waliokumbwa na kadhia za ajali kuchelewesha huduma, na wengine kupoteza maisha kabisa kwa kigezo cha kuhitajika PF3 kwanza.

Kingine nawachana Madaktari na Manesi, sio kwamba ninyi pekee mliosoma zaidi, wengine mmefaulu kwa kuungaunga na wengi wa Manesi pamoja na Clinical Officers form four walikuwa na D-TATU.

Narudia tena wengi wenu mna elimu za kawaida, na course zenu sio special.

Nimemaliza.

Pole sana.

Wataalamu wa afya (madaktari, manesi nk) wameapa kuokoa maisha ya watu pale wanapoumwa au kuumia kimwili.

Wagonjwa wa ajali huhitaji huduma ya haraka sana ili kuokoa maisha yao, kiutaratibu watu wanapopata ajali cha kwanza kabisa ni kuweka afya zao katika hali ya usalama ndipo mengine yafuate baadae...

Hata hivyo kuna sheria na taratibu zinazowataka waathirika wa ajali/walioshambuliwa nk kuja na PF3 hospitalini wanapofika kutibiwa.

Sheria hiyo imekuwa ikilalamikiwa kutokana na changamoto za kucheleweshewa huduma kwa sababu ya kukosa PF3. Mojawapo ya mapendekezo kuhusu upatikanaji wa PF3 ni kuwe na dawati maalumu za kutolea hospitalini badala ya kwenda kituo cha polisi.

Wahudumu wa afya (madaktari, manesi nk) mbali na kuzingatia viapo vyao pia hulazimika kuzingatia sheria hiyo ya uwepo wa PF3. Lakini cha kwanza ni kuokoa maisha...

PF3 ina umuhimu wake mfano hutumika kudai fidia kutokana na majeraha au ulemavu baada ya ajali nk.

Mwisho, siku zote uhai hupambaniwa kwanza halafu mengine baadae. Kumuacha mgonjwa afe kisa hana PF3 ni kosa kubwa ambalo ni kinyume cha maadili na viapo vya wataalamu wa afya (madaktari, manesi..)

Pia naamini lengo la kuwa na PF3 ni nzuri lakini huwa tatizo pale huduma inapocheleweshwa kwa sababu ya kukosa PF3 kwa hiyo uboreshaji wa sheria inahitaji.
 
Mbona kuna miongozo ilishatoka kuhusu hili Mkuu.

Ila sema tatizo ni kwenye weledi wa mtaaluma husika. Ni watumishi wachache sana wana weledi wa kazi zao.
 
Back
Top Bottom