Kati ya MBOWE na ZITTO, nani yuko sahihi?

Kati ya MBOWE na ZITTO, nani yuko sahihi?

Jibu hoja mwana, mimi ni chadema damu, ila sifurahishwi na malumbano baina hao wawili. Kama wanacdm ni lazima tutafute suluhisho na ikibidi kuwafukuze wote wawili kutoka chama chetu.
Kwani Chadema inaongozwa na malaika hata wasitofautiane!!?Kwanza uongozi wa Chadema haujawahi kusema pana mgogoro kati Zitto Kabwe na Mbowe ss huu mgogoro ni upi?Hebu na wewe thibitisha hilo usitoe comment kwa hisia sbb umesikia huyu kasema hivi na yule kasema vile
 
... wewe Kwayu kwenu si pale Nshara, jirani na Mbowe? Kwani lazima uvutie kwako? Hakuna ubishi kwamba Mbowe amefanyia nini CDM. Yapo mazuri mengi zaidi ya uloandika hapa. Yapo mengine ambayo si jukumu langu kuyaandika hapa. Kama ni kweli au majungu hayana nafasi kwani:
Mosi: CDM ni Chama, yaani wanachama wake na sera zake
Pili: Safari ya Ukombozi bado ndefu. The war is still on although some battles have been won. Huko tuendako kunahitaji mtu SAFI zaidi yake.
Tatu: Piga ua, ukwe (in-law wa Mzee Mtei) wake changanya na U-billicanas wake bado ni aspects ambazo kwa nji hii ni tatizo. Vijembe kama, ... mchezesha disko... sio kejeli ndogo kwenye uwanja wa siasa za maji taka. Hapa bado sijaweka ile minong'ono ya msokoto flani ..( jah man!). najua iko siku jamaa flani waweza mlipua vibaya mpaka afanane na kituko cha aina yake. Usione watu kimya.
.
Busara na hekima zingetosheleza kutothubutu kuiuzia CDM magari yale.... wengi hawatelewa kwa maana ya kwamba somo halitopanda. Kiongozi yeye anatakiwa alijue hilo. He should swallow that bitter salt pill instead.
.
.
et al.

WEWE NAE, ukijengi cdm. Huwezi kukijenga cdm kwa kumbomoa MBOWE. Wewe gamba ushindwe na ukatike.
 
CCM acheni kuwagombanosha viongozi wa CDM, naona mmekamia kweli kuimaloza CDM kupitia JF mwaka huu.
Afadhali umeliona wana CCM humu JF wameshindwa kuwaondoa mafisadi wanakimbilia mambo ya CDM na Kuyakuuuuza!
 
Watu tutambue uongozi shupavu wa kamanda Mbowe. Amekuwa ni kiongozi mwenye msimamo uliopelekea kukijenga chama kilicho imara na madhubuti.

Kikwazo kikubwa kwa usalama wa taifa, CCM na serikali ktk kukibomoa CDM ni Mbowe, wametumia mbinu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kumshawishi arudi CCM ili wampe hata uwaziri ila mbowe alisimama imara kutetea msimamo wake hii imepelekea CCM kumchukia sana kamanda Mbowe, na wako tayari kufanya lolote ili tu kummaliza wakiamini kwamba wataweza kuisambaratisha CDM.

Leo hii Zitto atueleze utajiri mkubwa alio nao ameupata wapi? Mwaka 2005 alipoenda kugombea ubunge alisaidiwa gari pajero naikumbuka ili kufanikisha ushindi wake, leo hii Zitto anaendesha Hammer na magari mengine ya kifahari.

Mbowe ametumia mali zake ktk kukijenga chama, fuso za music, gari aliyokuwa akitumia Dr Slaa, na magari mengine mengi ndani ya CDM yote ni mali ya Mbowe na siyo CDM.

Anapotaka kukiuzia chama magari ambayo chama chenyewe kimeyachakaza kwa nini aonekane mbaya? Wanajamii mtambue ya kuwa Zitto anatumiwa na kwa hilo hatofanikiwa hata kidogo.

Kanyaga twende makamanda wa ukweli ndani ya CDM.

Watu mnataka nini juu ya Zitto? Zitto juzi juzi magazeti yameandika kuhusu mawasiliano yake na Mkurugenzi wa usalama wa taifa na Rostam azizi na bado mnajipa hope kuwa Zitto ni Chadema huu si uwendawazimu mlitaka muambiwe vipi?? kama mwanahalisi walitoa namba za simu na muda na mara ngapi wanaongea kwa siku. Sio mwenzenu huyo achaneni naye yupo kuharibu tu. Sikuhizi anajidai anavipesa na sauti katuliza si mnamkumbuka kipindi kile cha mwanzo analalama bungeni kama katiwa funguo mpaka kafukuzwa. Hizo busara hamjiulizi Zito katoa wapi????? CCM wenyewe wanawashondwa mafisadi
 
WEWE NAE, ukijengi cdm. Huwezi kukijenga cdm kwa kumbomoa MBOWE. Wewe gamba ushindwe na ukatike.

... on the contrary. Tusiwe kama wale walomdanganya mfalme yule eti kaweka pamba za hali ya juu kumbe yupo uchi mtupu. Tunataka viongozi bora na safi tuchanganye na siasa safi tuwapelekee watu wetu wajikomboe, waondokane na UFUKARA wa kila hali. Au?
 
Tuhuma zako kwa Mbowe hakika ni nyingi, ila nataka kukujuza mambo kadhaa kwamba nyumba unayoitetea sasa (cdm) haikujengwa mara moja ilichukua muda mrefu kuijenga na kuinakshi mpaka wewe na wengine wengi wa aina yako mkaiona na kuipenda.

Mjenzi mkuu ni Mbowe na Slaa na huko nyuma hakukuwa na hili tunaloliona leo la Mbowe kukosa busara, haya yote tunayoyaona leo ni matunda ya mafanikio na ndio maana sasa mnatamani kufaidi au kudidimiza mafanikio hayo ila kikwazo ni Mbowe.

Viongozi wa mwanzo (akiwamo Mbowe) walijenga chama kwa fedha zao na rasilimali zao leo wanaonekana hawana busara.
Mkuu naunga mkono, ila kuna mtu mmoja muhimu sana umemsahau katika kuifikisha CHADEMA ilipo sasa. Naye ni kamanda PENGO! mpe ctredit yake tafadhali
 
Umejitahidi kujenga hoja ila umeegemea zaidi kwenye chuki na mapenzi binafsi, kumbuka huyo Mboye mwenyewe kwenye uchaguzi wa mwaka 2000 alitumia mda na fedha zake kukinadi chama pamoja na wagombea ubunge.

Sikuona aliye sema lolote , ndani ya CHADEMA kuna wabunge zaidi ya 47 lakini ni Shibuda pekeyake aliye enda kula msosi kwa JK, mpaka Wenja akamwambia ni mlafi vipi naye Wenje ni mmachame mwenzie?

Nashangaa unasema eti Lema alikuja kuwahonga hapa UDOM , ni uzushi kwani mimi mwenyewe nasoma hapa na nilimsikiliza bila kutoa fedha zozote nilimuunga mkono.

Sasa wewe hizo fedha alikupea wapi?

Na unajua kuwa rushwa ni adui wa haki kwanini haukumchukulia hatua za kisheria?

ACHA UCHONGANISHI KWANI HAPA TUPO WASOMI HIVYO HAUTA FANIKIWA , KUHUSU HAYO MAGARI MABOVU SOMA GAZETI LA MWANANCHI LA JANA UTAUJUA UKWELI KWANI MBOYE ALITOA MAGARI YAKE BINAFSI KUTUMIKA KWENYE KAMPENI.

HIVYO CHAMA KILIMUOMBA AKIUZIE SASA NANI ALIYE KUAMBIA KUWA KILA KITU CHA MTUMBA KIBOVU?
 
mimi naona aliye sahihi ni mbowe kwani ni chama cha baba mkwe wake halafu yeye ndiye aliyekipa nguvu chama
 
Jibu hoja mwana, mimi ni chadema damu, ila sifurahishwi na malumbano baina hao wawili. Kama wanacdm ni lazima tutafute suluhisho na ikibidi kuwafukuze wote wawili kutoka chama chetu.

ayo ni mambo ya ccm eti chama damu, ebu peleka huko,acha mbowe na zito. mnawachonganisha kipuuzi sana. Kama we ndo unafukuza wajumbe hao si uwaandikie barua kama mlivofanya huko ccm ili kujivua gamba?
 
Ndugu zangu wajf, baada ya marumbano na minyukano baina ya MBOWE na ZITTO. Sasa naomba mwongozo wenu wanajf kwa kuuliza maswali yafuatayo:-
(a) Nini chanzo cha mgogoro wao!
(b) Mgogoro wao ni kwa maslahi ya nani?
(c) Kwa nini wanarumbana ktk kila kitu?
(d) Nini maslahi ya chama na wanachama ktk mgogoro huo?
(e) Je nani yuko sahihi?
Naomba kuwakilisha.
Samahani mkuu naomba kuuliza,kwani ni ipi hiyo migogoro yao?
 
hoja za kuchafuana zilianzishwa na wana cdm wenyewe,akina mrema, mdee, mnyika na regia, kuwachafua wenzao, hivyo issue ikajulikana kuwa lema katumwa ddm ili awatumie wasomi kumzuia shibda, na mrema akatuma habsri haraka gazetini,nayo ikaliki...hahahaaa aiseee mnawafundisha wana ccm namna ya kutuchafua...acheni unafiki...chama kina katiba ni lazima kiende.
 
Hamna shaka kwamba cdm ni chama imara kinachoongozwa na viongozi wenye hekima na busara za kutosha ndio maaana imefika hapa ilipo. Isingekuwa ni kamanda mbowe na slaa kuwa na dhamira ya dhati kuijenga taasisi hii.leo hii kikwete asingekuwa na jeuri ya kuanzisha mchakato wa katiba mpya, asingeahidi maboresho ya mishahara ya wafanyakazi wa uma na mengine mengi. Mbowe alinunua magari yake mapya kabla hata hajaanza kuyatumia chama kikaanza kuyatumia na kuyazungusha nchi nzima, kwa nini hilo hamlioni?
 
Ndugu zangu wajf, baada ya marumbano na minyukano baina ya MBOWE na ZITTO. Sasa naomba mwongozo wenu wanajf kwa kuuliza maswali yafuatayo:-
(a) Nini chanzo cha mgogoro wao!
(b) Mgogoro wao ni kwa maslahi ya nani?
(c) Kwa nini wanarumbana ktk kila kitu?
(d) Nini maslahi ya chama na wanachama ktk mgogoro huo?
(e) Je nani yuko sahihi?
Naomba kuwakilisha.

Wote wako sahihi, katika CDM hakuna zidumu fikra za MKiti. Moto mbele.:israel:
 
Kwenye Threas Moja Huko Nimewashauri CCM juu ya Jambo hili hapa Chini

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...-kwa-viwavi-wenu-mliowatuma-hapa-jamvini.html

Kuna watu Wakasema ni Crap

Sasa hebu tukichambue hiki Kiwavi Jeshi Japo kidogo

Tukumbuke ni lema huyo huyo ndiye aliyekuja chuo kukuu cha dodoma na kutuhonga ( kutupa rushwa) ili tuandamane kupinga shibuda kuonyesha mtazamo tofauti ndani ya bunge, bahati nzuri wanafunzi wenzetu ambao hawakupata hela walikuwa wakali dhidi ya hili.

Kwanza Hapa Kimeshindwa Kuficha Asili yake yaani KUPOKEA RUSHWA

Bila ya shaka lema alifanya kitendo hiki bila ya kuwa na upeo wa kujuwa kwamba kinaweza kuchafua jina la chadema na kuharibu umoja ndani na nje ya chama.

Chenyewe kinadhani kina Upeo Mkuubwa kwa Kununuliwa


Mimi binafsi naweka imani yangu kwa mwanasiasa mwenye mawazo huru na ambaye hawezi kuburuzwa na mtu au kundi lolote. Najiuliza je hawa watu washawahi kusikia kuhusu joe lieberman wa democratic party aliyeenda kuhutubia katika mkutano wa kuzindua kampeni za republican party na kumpinga mgombea wa chama chake(obama wa democratic party).

Hivi Ukipokea Rushwa unakuwa na Mawazo Huru kweli?
 
Ndugu zangu wajf, baada ya marumbano na minyukano baina ya MBOWE na ZITTO. Sasa naomba mwongozo wenu wanajf kwa kuuliza maswali yafuatayo:-
(a) Nini chanzo cha mgogoro wao!
(b) Mgogoro wao ni kwa maslahi ya nani?
(c) Kwa nini wanarumbana ktk kila kitu?
(d) Nini maslahi ya chama na wanachama ktk mgogoro huo?
(e) Je nani yuko sahihi?
Naomba kuwakilisha.

Mbowe ni fisadi hawafai CDM
 
Jibu hoja mwana, mimi ni chadema damu, ila sifurahishwi na malumbano baina hao wawili. Kama wanacdm ni lazima tutafute suluhisho na ikibidi kuwafukuze wote wawili kutoka chama chetu.

Uhai wa Chama chochote cha siasa utauona kwa kuangalia kama ndani ya chama hicho kuna hoja zinazokinzana katika kila kikao cha chama hicho. Chama kisicho na uhai kisiasa ni kile ambacho hakuna kukinzana kwa mawazo ndani ya vikao vyake. Kila kitu akisema mwenyekiti ndicho hicho kinachosikika na kufuatwa na wengine. CDM ni mfano wa chama hai kinachoishi dunia ya leo, ilojaa mawazo mengi yenye kukinzana. Zitto na Mbowe, endeleeeni kukinzana kila itakapobidi, kwani katika njia hiyo chama ndio kitazidi kuwa imara.
 
ngoja niende jukwaa la ajira , maana natafuta kazi
 
Back
Top Bottom