Kati ya MBOWE na ZITTO, nani yuko sahihi?

Ndugu zangu wajf, baada ya marumbano na minyukano baina ya MBOWE na ZITTO. Sasa naomba mwongozo wenu wanajf kwa kuuliza maswali yafuatayo:-
(a) Nini chanzo cha mgogoro wao!
(b) Mgogoro wao ni kwa maslahi ya nani?
(c) Kwa nini wanarumbana ktk kila kitu?
(d) Nini maslahi ya chama na wanachama ktk mgogoro huo?
(e) Je nani yuko sahihi?
Naomba kuwakilisha.

Wanamgombea dada yako aaah namanisha mke wako. wape watatulia.
 
Watu mnataka nini juu ya Zitto? Zitto juzi juzi magazeti yameandika kuhusu mawasiliano yake na Mkurugenzi wa usalama wa taifa na Rostam azizi na bado mnajipa hope kuwa Zitto ni Chadema huu si uwendawazimu mlitaka muambiwe vipi?? kama mwanahalisi walitoa namba za simu na muda na mara ngapi wanaongea kwa siku. Sio mwenzenu huyo achaneni naye yupo kuharibu tu.

Dont be too quick to trust, Mwanahalisi sio Msahafu na wanaweza kutumika kumchafua mtu kwa maslahi yao binafsi au ya waliowatuma.

Sikuzote usiamini kila unachokisoma kwenye magazeti, siasa zetu hizi za majitaka zinaendeshwa kwa kuchafuana zaidi kuliko facts,kuelekea 2005, tuliambiwa Sumaye ni fisadi mkubwa na ni hatari kwa mali za taifa na tukamhukumu kwa uzushi lakini leo hii yapo wapi? waliokuwa wakimtuhumu kuwa ni fisadi leo hii yamewageukia!!

Tuwe waangalifu sana tusije tukamuhukumu mtu aliye msafi kwa sababu tu ya kuchafuliwa na wanaomhofia kisiasa.
 
Dont be too quick to trust, Mwanahalisi sio Msahafu na wanaweza kutumika kumchafua mtu kwa maslahi yao binafsi au ya waliowatuma.

Sikuzote usiamini kila unachokisoma kwenye magazeti, siasa zetu hizi za majitaka zinaendeshwa kwa kuchafuana zaidi kuliko facts,kuelekea 2005, tuliambiwa Sumaye ni fisadi mkubwa na ni hatari kwa mali za taifa na tukamhukumu kwa uzushi lakini leo hii yapo wapi? waliokuwa wakimtuhumu kuwa ni fisadi leo hii yamewageukia!!

Tuwe waangalifu sana tusije tukamuhukumu mtu aliye msafi kwa sababu tu ya kuchafuliwa na wanaomhofia kisiasa.
kwanini baada ya habari zake kuandikwa gazetini hakukanusha?
 
Mbowe sio kiongozi makini uwezi kumfananisha na Zitto
 
Salamu wana JF. Pamoja na kuwa mimi ni mara yangu ya kwanza ktk kutoa maoni kwenye mtandao wako, ninayo machache ya kuchangia kimawazo. Leo napenda kuchangia sakatala CDM, La kulumbana Mbowe na zito kwenye kikao. Nimefuatilia habari hizi kwa karibu, lakini hazijanifurahisha. watanzania wengi sasa tuna taka kuona chama badala ina kwepo itakayo ingoa CCM madarakani, ambayo kuwayo CHADEMA ndiyo inategemewa kufanya hivyo.

Suala la ununuzi wa magari mitumba inawahusu kamati kuu ya CDM, endapo wote walikubaliana kwa kikao halali. Hata hivyo Tsh. 480 mil. ni nyingi na magari ya mitumba. Lakini hata Zito na Mbowe kulumbana, wote wana makosa kwani wao ni viongozi. ZITO alikuwa wapi wakati budget ya kununua magari imepitishwa na wakati yeye ni ni N/katibu mkuu? Naye Mbowe haoni ni kutumia vibaya hela ya chama? Hawa wote wana tamaa ya uongozi na uchu wa madaraka, hawafai kuendelea kuongoza chama hicho kizuri kinacho kubalika kwa watanzania walio wengi.
Wengine wanachama wenye uwezo wagombee akina Mbowe na Zito sasa wasogee pembeni mpaka hapo watakapojirekebisha.

By Nada, The Prof.
 
Mbowe sio kiongozi makini uwezi kumfananisha na Zitto
. Kwa hilo wote wanafanana, Pengine Zitto angekuwa afadhali km angelumabana na mbowe wakati wanapitisha budget ya kununua magari. Walipitisha wote budget, wanafahamu wamepatana kununua magari mangapi na ya aina gani na ya shilingi kiasi gani. Zito km ni mtu makini alitakiwa ajue hilo kabla magari hayo hayajanunuliwa.

Mbowe pia ana matatizo yake makubwa tu, ni mbabe, anapenda kulazimisha maamuzi. Pia ndugu, uelewe kwamba hawa wote wanasumbuliwa na ugonjwa wa makundi na makambi mabaya kwa ajili ya kugombea uongzi wa chama na Urais 2015.Ndiyo maana nimesema wakae pembeni wote wawili wengine wajaribu.

Nada, The prof.
 
Ndugu zangu wajf, baada ya marumbano na minyukano baina ya MBOWE na ZITTO. Sasa naomba mwongozo wenu wanajf kwa kuuliza maswali yafuatayo:-
(a) Nini chanzo cha mgogoro wao!
(b) Mgogoro wao ni kwa maslahi ya nani?
(c) Kwa nini wanarumbana ktk kila kitu?
(d) Nini maslahi ya chama na wanachama ktk mgogoro huo?
(e) Je nani yuko sahihi?
Naomba kuwakilisha.

Mkuu kuwa specific , umetumwa nini? unazungumzia mgogoro gani? Enzi za ndiyo mzee zilishapitwa na wakati, CDM kuna Democracy ya kweli na si mgogoro.
 
Watu tutambue uongozi shupavu wa kamanda Mbowe. Amekuwa ni kiongozi mwenye msimamo uliopelekea kukijenga chama kilicho imara na madhubuti.

Kikwazo kikubwa kwa usalama wa taifa, CCM na serikali ktk kukibomoa CDM ni Mbowe, wametumia mbinu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kumshawishi arudi CCM ili wampe hata uwaziri ila mbowe alisimama imara kutetea msimamo wake hii imepelekea CCM kumchukia sana kamanda Mbowe, na wako tayari kufanya lolote ili tu kummaliza wakiamini kwamba wataweza kuisambaratisha CDM.

Leo hii Zitto atueleze utajiri mkubwa alio nao ameupata wapi? Mwaka 2005 alipoenda kugombea ubunge alisaidiwa gari pajero naikumbuka ili kufanikisha ushindi wake, leo hii Zitto anaendesha Hammer na magari mengine ya kifahari.

Mbowe ametumia mali zake ktk kukijenga chama, fuso za music, gari aliyokuwa akitumia Dr Slaa, na magari mengine mengi ndani ya CDM yote ni mali ya Mbowe na siyo CDM.

Anapotaka kukiuzia chama magari ambayo chama chenyewe kimeyachakaza kwa nini aonekane mbaya? Wanajamii mtambue ya kuwa Zitto anatumiwa na kwa hilo hatofanikiwa hata kidogo.

Kanyaga twende makamanda wa ukweli ndani ya CDM.
Unaujua mfano alioutoa Yesu?....Mjane mwenye senti chache alittoa kuliko matajiri wote?
Je,walalahoi nao watake kurudishiwa michango yao?
 
CCM acheni kuwagombanosha viongozi wa CDM, naona mmekamia kweli kuimaloza CDM kupitia JF mwaka huu.

Nazjaz naomba niwasiliane nawewe, email yangu ni sbilingi@gmail.com, then huko nipatie namba yako ili nikupigieee. Nimependezwa sana na majibu yako.
Hizo red hazinifanyi nisitishe hazma yangu...
 
Salamu wana JF. Pamoja na kuwa mimi ni mara yangu ya kwanza ktk kutoa maoni kwenye mtandao wako, ninayo machache ya kuchangia kimawazo. Leo napenda kuchangia sakatala CDM, La kulumbana Mbowe na zito kwenye kikao. Nimefuatilia habari hizi kwa karibu, lakini hazijanifurahisha. watanzania wengi sasa tuna taka kuona chama badala ina kwepo itakayo ingoa CCM madarakani, ambayo kuwayo CHADEMA ndiyo inategemewa kufanya hivyo.

Suala la ununuzi wa magari mitumba inawahusu kamati kuu ya CDM, endapo wote walikubaliana kwa kikao halali. Hata hivyo Tsh. 480 mil. ni nyingi na magari ya mitumba. Lakini hata Zito na Mbowe kulumbana, wote wana makosa kwani wao ni viongozi. ZITO alikuwa wapi wakati budget ya kununua magari imepitishwa na wakati yeye ni ni N/katibu mkuu? Naye Mbowe haoni ni kutumia vibaya hela ya chama? Hawa wote wana tamaa ya uongozi na uchu wa madaraka, hawafai kuendelea kuongoza chama hicho kizuri kinacho kubalika kwa watanzania walio wengi.
Wengine wanachama wenye uwezo wagombee akina Mbowe na Zito sasa wasogee pembeni mpaka hapo watakapojirekebisha.

By Nada, The Prof.

jana ulichangia nini ikiwa leo ndio siku yako ya kwanza, mbwembwe nyingiiiiiiiiiii
 
Ndugu zangu wajf, baada ya marumbano na minyukano baina ya MBOWE na ZITTO. Sasa naomba mwongozo wenu wanajf kwa kuuliza maswali yafuatayo:-
(a) Nini chanzo cha mgogoro wao!
(b) Mgogoro wao ni kwa maslahi ya nani?
(c) Kwa nini wanarumbana ktk kila kitu?
(d) Nini maslahi ya chama na wanachama ktk mgogoro huo?
(e) Je nani yuko sahihi?
Naomba kuwakilisha.

Aisee acha hizo bana, fitina mfitini makamba!
 
Tuhuma zako kwa Mbowe hakika ni nyingi, ila nataka kukujuza mambo kadhaa kwamba nyumba unayoitetea sasa (cdm) haikujengwa mara moja ilichukua muda mrefu kuijenga na kuinakshi mpaka wewe na wengine wengi wa aina yako mkaiona na kuipenda.

Mjenzi mkuu ni Mbowe na Slaa na huko nyuma hakukuwa na hili tunaloliona leo la Mbowe kukosa busara, haya yote tunayoyaona leo ni matunda ya mafanikio na ndio maana sasa mnatamani kufaidi au kudidimiza mafanikio hayo ila kikwazo ni Mbowe.

Viongozi wa mwanzo (akiwamo Mbowe) walijenga chama kwa fedha zao na rasilimali zao leo wanaonekana hawana busara.

Kaka Chadema ina watu wazito inaonekana huijui Chadema.

Edwin Mtei,Philip Ndesamburo,Bob Makani na wenzao ndio wajenzi wakuu wa Chadema.Unafahamu Kua Dr.Slaa alikua mbunge wa CCM?
Mbowe alipanda ili chama kisiende 'mbali' lakini Chadema bila Ndesamburo,isingefika hapa
 
CHADEMA haikuota kama uyoga kama watu wanavyofikiri, kuna watu wali-sacrifice maisha yao, mali zao na hata ajira zao ili kuijenga, leo hii mtu unaingia CHADEMA siku mbili tatu unakurupuka kuanza kuhoji magari, pesa, mishahara nk.

Kila chama kina waasisi na misingi, hata kama ni demokrasia lakini lazima ina ukomo. Mimi leo siwezi kujiunga CHADEMA then kesho nahoji mshahara wa Mbowe.

Kuhusu Zitto, huyu jama kashapoteza mwelekeo, aitamghalimu sana kurudisha imani ya washabiki wake na nafikiri ndani ya CHADEMA nafasi yake ndiyo inapotea taratibu. Cha msingi maamuzi ya Vikao ndiyo ya mwisho hata wakiamua kununua bajaji na kuzigawa kila ofisi ya CHADEMA nchi nzima basi huo ni uamuzi wa kikao na si wa mbowe.

Mnaomtetea Zitto mtakuwa na kazi kubwa maana kashajichafua mwenyewe na hana credibility ya kuitwa MPIGANAJI ndani ya CHADEMA.
 
Tafuta thread humu ndani ya jamvi wenyewe wamekuja hapa wakasema hakuna malumbano kati yao wewe unakuja hapa unaspin kwa manufaa ya chama chako CCM tunakuambia ni very wrong strategy

he kumbe ni kweli yale yaliyosemwa na Mukama kwamba jf ni ya chadema???
 
Tafuta thread humu ndani ya jamvi wenyewe wamekuja hapa wakasema hakuna malumbano kati yao wewe unakuja hapa unaspin kwa manufaa ya chama chako CCM tunakuambia ni very wrong strategy

he kumbe ni kweli yale yaliyosemwa na Mukama kwamba jf ni ya chadema???
 
Back
Top Bottom