Katambi: Tumedhibiti wimbi la wahamiaji haramu, Uhamiaji imedhibiti na kufunga njia za vipenyo 1,777

Katambi: Tumedhibiti wimbi la wahamiaji haramu, Uhamiaji imedhibiti na kufunga njia za vipenyo 1,777

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
4,783
Reaction score
14,975
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Patrobas Katambi amesema katika kudhibiti wimbi la wahamiaji haramu wanaoingia nchini. Idara ya Uhamiaji imedhibiti na kufunga jumla ya Vipenyo Elfu Moja Mia Saba Sabini na Saba vilivyopo maeneo mbalimbali nchini, vilivyokua vinatumika kuingia nchini kwa njia hiyo isiyo halali.

Ametoa kauli hiyo wakati wa ziara iliyofanyika Makao Makuu ya Idara ya Uhamiaji, jijini Dodoma ambapo pia aliongozana na Naibu Waziri Ayoub Mohamed Mahmoud ikiwa ni mara ya kwanza baada ya kuteuliwa na Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ambapo Naibu Waziri na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala pia walipata nafasi ya kutoa neno.
 
Back
Top Bottom