Kataa Ugali, Ugali ni Mateso

Kataa Ugali, Ugali ni Mateso

Wabongo wakishaanza kupata mia mbili mia mbili utajua tu.

Ugali ndiyo ulimkuza bibi mzaa baba,baba na hatimaye ukakulea,Leo unakuja kuusimanga.

Hela za sisiem zimeshaanza kuwapa jeuri mtaani kiasi cha kuona ugali ni adui wa taifa?
😂😂 wakati adui yao ni ccm
 
Siwezi kula ugali
Ugali chakula cha ovyo
Ugali unaliwa jera
Ushawahi ona wapi Kwenye sherehe au harusi wanapika ugali

Mahindi yaliletwa na wareno ili kuwafanya waafirika wajinga
 
Tumezaliwa tumeukuta ugali tumekuwa tunakula ugali Tena Dona we jamaa vipi afu kijjijini tumekula sana ugali wa ulezi unajua shoo yake wewe na dagaa wa ziwa Tanganyika unavua na shati kabisa we jamaa tuachie ugali wetu nyie kuleni baga zenu huko huko
 
Amin Amin nawaambieni Ugali sio mateso Bali watu wale ugali kwa kiasi😎
 
akiwa na kampeni ya kugombea Urais atatoa ahadi Hamtokula Ugali 😄
 
Kwa nini ule vyakula vya wanyama.

Kwa nini ule kitu ambacho kina nafasi kubww ya kukufanya uwe na mwili usio eleweka.

Kwa nini ule kitu kinachoweza kukuleta high blood pressure na cancer

Kwanini ule kitu kisochokuwa na vitamin and mineral deficiencies,

Kwanini ule MATOFALI



Ugali gani? Kuna aina nyingi za ugali: wa sembe, wa 'dona', wa mtama, wa mihogo, wa ulezi nk.

Inabidi uende shule ujifunze masomo ya sayansi ya afya au Biology. Ujue kutofautisha nutrients zinazopatikana katika aina mbalimbali za ugali.

Ugali hauleti high blood pressure wala cancer moja kwa moja. Tatizo sio ugali, bali ni aina ya chakula kinacholiwa pamoja na ugali, au mtindo wa maisha kwa ujumla. Kwa mfano, mtu anayekula ugali mwingi kisha anakula nyama ya mafuta kila siku, hana mazoezi, na anakunywa soda au pombe — huyo yuko katika hatari zaidi ya kupatwa na magonjwa hayo, sio kwa sababu ya ugali bali kwa sababu ya mtindo wa maisha.

Ugali unatengenezwa kwa wanga kutoka nafaka kama mahindi, mtama au muhogo. Wanga ni chanzo muhimu cha nishati mwilini. Kinachotakiwa ni kiasi sahihi na mlo kamili unaojumuisha mboga, protini na matunda. Kupiga marufuku ugali ni kueneza hofu isiyo na msingi.

Biblia inatuonya katika 1 Timotheo 4:3-5 tujihadhari na watu wanaokataza wengine kula vyakula fulani:

"Wao huwakataza watu wasioe na kuwaagiza wajiepushe na vyakula fulani, ambavyo Mungu aliviumba ili vipokewe kwa shukrani na wale wanaoamini na kuijua kweli.
"
(1 Timotheo 4:3-5)

Soma pia, Mithali 25:16
"Ukipata asali, kula kiasi tu cha kukutosha, ukila zaidi, utatapika.."

Hapo tunafundishwa kula kwa kiasi, sio kupiga marufuku.
 
nikishatinga pensi langu lililobana mapaja na earphone zangu na simu yang ya iphone macho matatu nasikiliza ngoma za zuchu , nalambalamba lips , naenda chimbo la chips YAI ya kushiba na mishkaki fresh tu si inakua unyama sana
Aaah unasemaje?
 
Ugali gani? Kuna aina nyingi za ugali: wa sembe, wa 'dona', wa mtama, wa mihogo, wa ulezi nk.

Inabidi uende shule ujifunze masomo ya sayansi ya afya au Biology. Ujue kutofautisha nutrients zinazopatikana katika aina mbalimbali za ugali.

Ugali hauleti high blood pressure wala cancer moja kwa moja. Tatizo sio ugali, bali ni aina ya chakula kinacholiwa pamoja na ugali, au mtindo wa maisha kwa ujumla. Kwa mfano, mtu anayekula ugali mwingi kisha anakula nyama ya mafuta kila siku, hana mazoezi, na anakunywa soda au pombe — huyo yuko katika hatari zaidi ya kupatwa na magonjwa hayo, sio kwa sababu ya ugali bali kwa sababu ya mtindo wa maisha.

Ugali unatengenezwa kwa wanga kutoka nafaka kama mahindi, mtama au muhogo. Wanga ni chanzo muhimu cha nishati mwilini. Kinachotakiwa ni kiasi sahihi na mlo kamili unaojumuisha mboga, protini na matunda. Kupiga marufuku ugali ni kueneza hofu isiyo na msingi.

Biblia inatuonya katika 1 Timotheo 4:3-5 tujihadhari na watu wanaokataza wengine kula vyakula fulani:

"Wao huwakataza watu wasioe na kuwaagiza wajiepushe na vyakula fulani, ambavyo Mungu aliviumba ili vipokewe kwa shukrani na wale wanaoamini na kuijua kweli."
(1 Timotheo 4:3-5)

Soma pia, Mithali 25:16
"Ukipata asali, kula kiasi tu cha kukutosha, ukila zaidi, utatapika.."

Hapo tunafundishwa kula kwa kiasi, sio kupiga marufuku.
Sawa mchungaji
 
Naona uzi wa singo faza na singo maza sio dili JF bali Kuukataa ugali ndio talk of Jf. Jf kila mtu anachukia yugali 🤣🤣
 
Siwezi kula ugali
Ugali chakula cha ovyo
Ugali unaliwa jera
Ushawahi ona wapi Kwenye sherehe au harusi wanapika ugali

Mahindi yaliletwa na wareno ili kuwafanya waafirika wajinga
Kivipi kutufanya wajinga?
Ila naona sisi Ndio tumeathirika kwa baadhi ya watu kwenye mlo unakuwa sio kamili ukiangalia vyakula vingi watu walivyozoea ni vya carbohydrates

Zikiwa nyingi zinaathiri neurons kuloose fuels caused by insulin resistance that causes decrease of glucose which is less supplied to neurons and low ATP production
Effects zake
it cause loose of focus
Low memory capacity
Decreased attendance
Low processing speed
 
Kwa nini ule vyakula vya wanyama.

Kwa nini ule kitu ambacho kina nafasi kubww ya kukufanya uwe na mwili usio eleweka.

Kwa nini ule kitu kinachoweza kukuleta high blood pressure na cancer

Kwanini ule kitu kisochokuwa na vitamin and mineral deficiencies,

Kwanini ule MATOFALI



Duh.! Week hii ugali umeandamwa sana na wanaume wa Dar sijui nitafute mwanasheria aje kutetea hiki chakula maana sio kwa masimango haya!
 
Siwezi kula ugali
Ugali chakula cha ovyo
Ugali unaliwa jera
Ushawahi ona wapi Kwenye sherehe au harusi wanapika ugali

Mahindi yaliletwa na wareno ili kuwafanya waafirika wajinga


Zamani nilikua hivihivi kule kijijini kwamba wakipika chakula cha ndizi nachukia kabisa sababu kilikua kinafululizwa ila wakibadili hata viazi naona nafuu.... Leo nipo hapa mjini ndizi zilezile ndio naziona bora wakati nilikua naziona kama chakula cha nguruwe

Ongeza kipato chako uweze kubadili vyakula mara kwa mara ndipo utajua thamani ya ugali
 
Back
Top Bottom