Lwiva
JF-Expert Member
- Apr 17, 2015
- 21,103
- 29,651
Ladha ya Ugali ni mboga ...tumia akili sasa kama unakula ugali na maharage hayo ni mazoezi ya kuishi jela ...ugali una mboga zake na mapishi yake ya mboga asilimia 90 wa wanawake awajui kupika hata dagaa....hata samaki wa mitaa wa kukaanga awapo sawa wanakaangwa hovyo ...mfano kupika dagaa kuna hatua hizi za kuwaandaa ambazo wengi amfuatiNi mbaya ila ugali hauna hata ladha
1)nunua dagaa
2)wachambue kuondoa dagaa wagogo sana na kuondoa vichwa
3)waoshe kwenye maji ya uvuguvugu x3
4)weka sufuria ya maji jikoni ya chemke tia kijiko kimoja cha chumvi na kamulia ndimu au limao
5)tia dagaa kwenye hiyo surufia funika wachemke hadi watoe povu ...ilo povu ni uchafu na shombo .
6)wakisha chemka mwaga hayo maji yenye povu na kuwaosha hao dagaa tena na maji ya uvuguvugu .
7)chukua kikaango na mafuta ya kula wakaange hao dagaa ulio wachemsha hadi wanukie sana
8)wakisha kunukia waepue hapo dagaa wako wapo tayari kwa kuanza mapishi ya aina yoyote ..hizo hatua zote ni hatua za kuwaandaa tu dagaa kabla ya kuwapika mapishi utakayo .HAPO UNAKUWA UMEFANYA KITU KINAITWA ZERO SHOMBO