Watu8
Platinum Member
- Feb 19, 2010
- 76,271
- 108,268
Wee watu8 weewee usifanye mie nikanuniwa na kumwagiea maji ya moto humu. Si unajua wadada zetu kununiana hahahaaa, mie muoga bana kugombana, kupigana kupashuana siwezi, naweza kuchekatuu na kuimba baas!! Sasa ukisema wa humu wa humu mie wa kwenye foleni, usiache wakanitolea upepo bito yangu buree wakati sina hata ugomvi na mtu, mdada wa watu mpoleeee
Na kwanza umenijulia wapi maana uniambiayo ni kweli.... am keen who r u?
Tena ukithubutu kuingia kwenye ndinga langu ntamwagiwa tindikali buree, ntaringaje sasa mjini hapa na sura haina repair looh bora tupungiane tuu kwa foleni
Halafu uache uchokozi bana.
Sijui nijibu swali lipi niache lipi maana umeniuliza utitiri wa maswali na hapa pia nimeweza gundua haiba yako nyingine mpya kabisa, nayo ni udadisi na mdada akiwa mdadisi ujue ana hulka ya uelevu "intelligent"...
Nimekujulia hapa hapa na wala si nje ya hapa kipenzi, halafu ukiniita mi mchokozi dereva wa Nissan utamuitaje sasa hahah...