Kashfa ya Uzinzi: Lissu amsafisha Mbowe

Kashfa ya Uzinzi: Lissu amsafisha Mbowe

Status
Not open for further replies.
----- lisu naona akili yake inaendelea kuwa na kichaa
hakuna watu wajinga wanaweza kukubali kuwa na kiongozi asiyefata maadili ya kijamii
kuwa kiongozi maana yake unakuwa role model wa vijana walio wengi pamoja na watoto wetu wanaochipukia,sasa mnadhani mtaniambia kuwa watoto na sisi vijana tunajifunza nini kwa kiongozi mkubwa kama mbowe kuwa na tabia za uzinzi tena inasemekana ananunua hadi malaya huko sinza na kinondoni
LAKINI IKUMBUKWE HUYU JAMAA MBOWE AMEOA NA ANAE WATOTO unadhani kutokana na tabia zake za uzinzi mkewe ATAMUAMINI na watoto wake wa ndani ya ndoa WATAMPENDA? kama amekuwa mjasiri wa kuweza kumsaliti MKE WAKE WA NDOA NA WANAE unadhani mtu kama huyu hawezi kuwasaliti watanzania?

TAFAKARI CHUKUA HATUA
 
Kwa sababu ni mkataba baina ya mume, mke na jamii waliyopo.
Ndoa is public, ni mkataba unaotakiwa uwe published in public records.
There's always a public interest in any marriage .... a wedding can be private.

Wewe ukioa mke au kumwacha kamwe jamii haina hasara wala faida yoyote kwani haina mkataba nanyi, lete hoja zenye mshiko utaeleweka bro na sio hizo za kubumba! nyie huko upande wenu mna mpaka kashfa za kubaka na mnalindana mpaka leo hata kupeleka kesi mahakamani mnashindwa, huyo Naibu spika wenu unazijua kashfa zake nyumbani kwake? mtu hajui hata idadi ya watoto wake mtaani?
 
Mimi ni muumini wa CDM na mshabiki mtiifu kwa Mbowe,hata kama ndoa ni jambo la binafsi lkn kwanini akubali kuingia kwenye hizi kashfa kizembe namna hii,CDM inawindwa kila kona,kosa kidogo maadui wanalishikia bango,binafsi nawaomba viongozi wa CDM kuachana na mambo yanayozua maswali kwa jamii...........CDM malizeni hili la Zitto tusonge mbele.
 
Nakumbuka Nyerere aliwahi kusema, kiongozi mzinzi hafai kuongoza nchi!
 
Ndoa siyo jambo binafsi.

Ni kweli hasa ndoa si jambo binafsi hasa ya Mbowe sababu wengi walihudhuria na viongozi wake wa dini ya Kikristo akawaapia kuwa atakuwa na mtu mmoja tu wa chumbani ambaye ni Lilian mbele ya kadamnasi.

Sasa akionekana mahali kwenye Chumba na Mwanamke ambaye sio Lilian makundi ya kadamnasi lazima yapige kelele.
Ndoa ukishachangisha watu tu ukawaalika ukakusanyika nao mahali umeivua hijabu ya kuwa private na inakuwa public hivyo Public ina haki ya kujua Haki za Lilian zinapogaragazwa na vimada wakati maisha yake kawekeza Kwa Mbowe mbele ya public.Public ina haki ya kupiga filimbi ikimwona Mbowe yuko kifuani kwa mwanamke mwingine ambaye sio Lilian.

Tundu Lissu sheria bado kabisa ndio maana vijana wanasheria wadogo wanamgaragaza mahakamani
 
Tundu Lissu nae kawaje siku hizi kuna mengi ya kuongeleaa yeye amekazania Mbowe na Zito
 
Nakubaliana kabisa na Mh Lissu tujadili mwenendo wa serikali yetu bei ya umeme na mengineyo haya ya mtu binafsi tuyaache
 
Nelson Mandela hakuwa na tatizo isipokuwa baadhi ya wake zake. Bill Clinton alikiri na kuomba radhi na neno alilitumia ninalinukuu, " I had inappropriate relationship with Monica Lewinsky".

Naanza kuona kuwa, JK Alikuwa sahihi kusema Lissu ni Hatari sana katika Uongozi Wa taifa hili.

Kumdhalilisha Mandela!? No! thank u
 
KATIKA kile kinachoonekana kama kumsafisha Mwenyekiti wa Taifa wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Freeman Mbowe dhidi ya kashfa ya uzinzi inayomuandama.

Mwanasheria Mkuu wa chama hicho, Tindu Lissu amesema suala hilo ni maisha binafsi ya mtu, ambayo hayawezi kuhusishwa na wadhifa wake kwa namna yoyote.

sifa ya fisadi huanzia na uasherati....Clinton alitubu akasamehewa na huyu wa kwao alitubu lini na kujutia kikamilifu?
 
Ndoa iheshimiwe na watu wote! that's what the bible says.

Hawa akina Lissu majanga hawana maadili hata ufisadi ni private issue hausiani na taasisi
 
Hapa naomba nipingane na mheshimiwa Lissu.

Suala la uongozi na integrity vinaenda mkono kwa mkono. Huwezi kusema eti ni private matters.

Adultery is not only immoral but also a sin. Ukiwa kiongozi lazima uwe unajiheshimu. There's no excuse for moral decadence.

Kiongozi ni mfano kwa na kioo cha jamii. Huwezi kujiita kiongozi mzuri wakati tabia zako ni walakini.

Hakuna shabaha kati ya mheshimiwa Mbowe na Madiba. Ni mifano isiyoingiliana hata kidogo.

Kama kweli mheshimiwa Mbowe ni mzinzi basi ni shurti abadilike kama kiongozi mkuu wa chama kikuu cha upinzani chenye ushawishi mkubwa kitaifa.
 
Kwa kweli siasa ni kitu cha ajabu sana.

Gazeti la Tanzania Daima liliandika ishu ya Kapuya kwa muda wa wiki mbili ndio habari kuu front page. Leo hii wanatetea ya Mbowe kukatisha safari ya mbunge wa viti maalum na kumuita Dubai jiji la maburudani kwa kusema eti hayo ni "mambo binafsi na yanatakiwa kubaki huko huko chumbani".

Ama kweli ukiwa muongo usiwe msahaulifu, utabambwa tu
 
Naona na gazeti lao mama la Tanzania Daima sasa limekoma kuandika habari za Kapuya ili na ya Mbowe yasisambae sana.
 
Viongozi wa CHADEMA ni majanga tupu.

Kwa hiyo kumbe Mh. Mbowe ni mzinzi kwa maana nyingine, tuhuma hizi ni za kweli.

Sasa kama maswala ya Uzinzi ni private affairs. Vipi hili swala la kupewa millions pesa za Tanzania na wale wale kila mara alikuwa akipanda kwenye majukwaa alikuwa anawaita mafisadi.

Pesa za huyu kada wa CCM alizochukua nazo ni private affairs

View attachment 132573

Tunaomba tufahamu mipaka ya private affairs nchini

Kama ameweza kuijibu hoja ya uzinzi, kwa nini hakutaka kuijibu hoja ya "double agent" kwa maana kuwa, mchana ni mpiga vita mafisadi na usiku ni mpokea pesa za mafisadi


Nafikiri hatuna haja ya kuendelea kujadili masuala kama haya ambayo kiukweli hayatufaidishi kwa namna yoyote ile. Labda tungeambiwa kuwa suala hili kwa namna fulani linaathiri utendaji kazi wa mtu, hapo pasi na shaka tungekuwa na kila sababu ya kulijadili. Hii ni sawa na mtu kugombana na mke/mme nyumbani kwake; je hii ina maana mtu huyo si kiongozi bora kwa sababu tu katofautiana na mwenzake?

Pia suala la kile kinachoitwa kupokea fedha za mafisadi, ni vizuri tukawa na uhakika na kile tunachokiandika kwanza na si kukurupuka. Ni vema tungesubiri kwanza kauli za wahusika wenyewe na si kuhitimisha suala ambalo hatujui undani wake ila tunajadili tu kwa sababu ya ushabiki usio na manntiki wala tija kwa demokrasia yetu.
 
Mimi ni muumini wa CDM na mshabiki mtiifu kwa Mbowe,hata kama ndoa ni jambo la binafsi lkn kwanini akubali kuingia kwenye hizi kashfa kizembe namna hii,CDM inawindwa kila kona,kosa kidogo maadui wanalishikia bango,binafsi nawaomba viongozi wa CDM kuachana na mambo yanayozua maswali kwa jamii...........CDM malizeni hili la Zitto tusonge mbele.

Kaka masuala ya Zitto yalishaisha zamani na amebakia kuwa mwanachama wa CDM na mbunge wa Mahakamani, hapa tubadilishane mawazo kuhusu hili la mambo ya binafsi je ni halali kuhusishwa na Kiongozi mwadilifu na si vingenevyo, mimi binafsi sipendi katabia ka uzinzi lakini linapokuja suala la Kiongozi makini basi Mbowe & Slaa ni namba moja...

Hebu angalia huko kwao na anza na mwenye nyumba usikie aliyokuwa anayafanya kila aendapo uingereza
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom