Mzito Kabwela
JF-Expert Member
- Nov 28, 2009
- 18,857
- 7,615
Kwa mjibu wa msemaji wa jeshi la Polisi Advera Senso kupitia Clouds Fm leo asubuhi mtu mmoja aliyemtaja kwa jina moja kama Komba ameshakamatwa kuhusiana na kuwepo mtandao mkubwa ndani na nje ya jeshi hilo unajiusisha na kuwalaghai vijana wanaotaka kujiunga na jeshi la polisi.
Inasemekana vijana zaidi ya 200 walitapeliwa kiasi cha shillingi 800,000/= kila mmoja kwa minajiri ya kuwawezesha kujiunga na Chuo cha Polisi Moshi baada ya kuhonga kitita hicho walitakiwa kulipa tena 25,000/= kama nauli ya kuwafikisha Moshi na kweli mabasi matatu yalikodishwa nakuwafikisha Moshi chuoni.....
Jk vunja hili jeshi ili walau tukuone upo serious,unataka wafanye nini ujue wameoza hawa?
Yeye anayetoa Rushwa ili aajiriwe polisi na mpokeaji wote majizi tu, kuna haja gani ya kuhonga ili uwe polisi?!! kwani lazima uajiriwe polisi?!! hata ukilima bado utakua umeitumikia nchi yako kupitia eneo hilo la kilimo...nchi imegeuka kuwa ya kitapeli tapeli tuuu
Baada yakufika chuoni taratibu zote za kuwasajili pamoja na kutakiwa kulipia gharama nyingine za kiasi cha shillingi 50,000/=,walinyolewa vipara na kuanza kupiga kwata kama makuruta wengine.
ilikuwa je!hebu tukumbushe.na mimi mkuu Elli ,kimsingi polisi ni uozo mtupu,unakumbuka ishu ya mke wa Chagonja?
Hivi hizo taratibu za usajili zilifanyika pale pale chuoni Moshi au nje ya chuo?
Hii naiona ni national security issue na uzembe uliokithiri. Ukipewa gharama ya hao watu 200 kulala na kula hapo chuoni kwa usiku mmoja tu utazimia! Hata viwembe vya kunyolea navyo vyauzwa!!!