Kashfa ya kutisha jeshi la Polisi

314052_322130297877672_700126719_n.jpg
 
Tuko salama mahali popote? Utapeli unapoingia kwenye sehemu nyeti hivyo kweli ni suala la kuogopesha. Nashangaa hadi leo yule mwanamke hajakamatwa wala uchunguzi wowote hujafanyika. What a disgrace!
 
Yaani kama vile movie ya kijasusi,watu zaidi ya 200 wanaingia CCP wanalala,bila uongozi kujua ualali wao?what shame Police of Tanzania?chuo chenye kutrain wapelelezi ? Kwa hili Polisi wa Tanzania mtupe maelezo yalioenda shule kwa kweli
 
Kwa mjibu wa msemaji wa jeshi la Polisi Advera Senso kupitia Clouds Fm leo asubuhi mtu mmoja aliyemtaja kwa jina moja kama Komba ameshakamatwa kuhusiana na kuwepo mtandao mkubwa ndani na nje ya jeshi hilo unajiusisha na kuwalaghai vijana wanaotaka kujiunga na jeshi la polisi.

Inasemekana vijana zaidi ya 200 walitapeliwa kiasi cha shillingi 800,000/= kila mmoja kwa minajiri ya kuwawezesha kujiunga na Chuo cha Polisi Moshi baada ya kuhonga kitita hicho walitakiwa kulipa tena 25,000/= kama nauli ya kuwafikisha Moshi na kweli mabasi matatu yalikodishwa nakuwafikisha Moshi chuoni.....

Vijana waliotapeliwa wasiende kutoa malalamiko kwa kuwa wakifika wao ndo watakamatwa kwa kuhonga Jeshi la polisi ili wapate ajira. Polisi watawageuzia kibao. Sasa kama hayo yote yamefanyika pale CCP Moshi, na eti mtu mmoja ndo amekamatwa, inakuja akilini hapo?

Huyo mtu mmoja alikuwa dereva wa mabasi matatu, aliidhinisha hayo magari, akatoa amri ya kunyoa vipala na akaitekeleza mwenyewe, akawapa sehemu za kulala huyo huyo mmoja, akawalisha chakula, akawapa maji na sabuni za kuogea...jamani kwanini tunakuwa wajinga?

Haya yote ni mipango ambayo inasukwa na mtandao wa Jeshi la Polisi na wanajua. kwa nini mfano asingekamatwa Mkuu wa Chuo cha Polisi Moshi?

Kwa nini Kamanda Kamuhanda wa Iringa hajakamatwa hadi leo? Wakubwa wanalindana ndio maana nasema vijana waliotapeliwa wasiende huko kulalamika kwa vile watageuziwa kibao.
 
Kama kujiunga tu upolisi kazi ambayo daah.. anyway, ni kwa rushwa, sasa polisi wa namna hiyo utamwambia maneno gani aache kupokea rushwa? Ndio maana madogo wa bodaboda wanapata shida sn mtaani. Polisi hata 500 haachi. Hali ni mbaya
 
Yeye anayetoa Rushwa ili aajiriwe polisi na mpokeaji wote majizi tu, kuna haja gani ya kuhonga ili uwe polisi?!! kwani lazima uajiriwe polisi?!! hata ukilima bado utakua umeitumikia nchi yako kupitia eneo hilo la kilimo...nchi imegeuka kuwa ya kitapeli tapeli tuuu

Mkuu kwa hali tuliofikia Tanzania leo bila ya kutoa rushwa iwe ya cash au ngono kupata kazi ni shughuli pevu..! Sio Polisi tu hata ajira kwenye sekta nyingine zinapatikana kwa mtindo huo wa rushwa au kujuana.. So kwa mtazamo wangu hauko sahihi kumuhukumu alielazimishwa na jamii iliomzunguka kutoa rushwa ili apate uwezo wa kujikimu..

Kwenye kulima ndio hakufai kabisa mkuu.. Umeona wakulima wa korosho wanavyolilia hela zao..? Umeona wakulima wa mahindi Rukwa walivyolalamika mahindi yao kuoza kwa kuwa hawana pa kuyaweka na wanalazimishwa kutokuuza mazao yao kwa wafanyabiashara wa kigeni ambao wanalipa hela nyingi..?

Umeona wakulima wengi huko mikoani wakilalamika kupata hasara kwa kuwa au wamecheleweshewa mbolea au wameuziwa mbolea fake ambayo ilipelekea kuharibu mazao yao..?
 
Baada yakufika chuoni taratibu zote za kuwasajili pamoja na kutakiwa kulipia gharama nyingine za kiasi cha shillingi 50,000/=,walinyolewa vipara na kuanza kupiga kwata kama makuruta wengine.

Hii naiona ni national security issue na uzembe uliokithiri. Ukipewa gharama ya hao watu 200 kulala na kula hapo chuoni kwa usiku mmoja tu utazimia! Hata viwembe vya kunyolea navyo vyauzwa!!!
 
Tukisema Mwema anaongoza genge la wezi watu watabisha!!. Hili ni suala la TISS hebu fikiri hao wangekuwa mapolisi Nchi ingekuwa na usalama! au tuseme huu ndio mtindo wa recruitment ya vyombo vya usalama!! Are we safe?

The security systems needs an overhaul. It is only an insane person who would appreciate TISS working only to stop opposition while internally this is the situation! Hakuna serikali hapa!! wala Nchi. hasa tunapoambiwa hizi zinatakiwa "siri za serikali" Grrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr!!
 
Hii ni issue nyingine ambayo IGP na timu yake wanatakiwa wajichunguze na kuona kama kweli wana umuhimu wa kuendelea kuwapo kwenye uongozi wa jeshi la Polisi..

Huu mtindo wa kubebana unafikia mahali pabaya maana Jeshi la Polisi ni taasisi nyeti ambayo kila raia anaitegemea kwa usalama wake.. kama leo nako ndio kuna huo "organized" utapeli raia wa Tanzania hatuko salama.. Imagine Polisi wamekuwa wanawaua ovyo raia..

Wanawabambikia kesi zicizo na kichwa wala miguu raia wacio na hatia.. Leo wameonyesha rasmi kumbe kwenye utapeli wao ndio waalimu..!

Presidaaa inasemekana jamaa ni shemeji yake ila kwa hili aone aibu.. Akae pembeni yeye na makamishnaa wote waliopo sasa.. at least Jeshi lionekane kujaribu kujiondoa kwenye tope hili la aibu na fedheha kubwa..
 
Hivi hizo taratibu za usajili zilifanyika pale pale chuoni Moshi au nje ya chuo?

Hata mie nimejiuliza! Na je usajili hauambatani na rekodi iliyopo kuwa anayesajiliwa ndiye anayepaswa kuwepo? Kwa hiyo hata miye ambaye sikuwepo kwenye 'intake' hiyo ningeruka uzio na kujipanga kunyolewa wangeendelea tu kunipokea?

Na hao CCP Moshi wana majibu ya kutoa waache kutuletea mauzauza, kweli basi zima linaingia watu hawastuki?

Na je hao waliopokelewa ni mara ya kwanza hicho kinachokea au kuna 'intake chapchap' nyingine zilishapita?
 
Polisi.....Polisi.....Polisi.....Jeshi la Polisi Tanzania!!!! Kero tupu, makashfa yao makubwamakubwa ya kikatili kwa raia!

Natamani siku moja tupate serikali mpya iliyo makini, hizi kero zitabaki historia.

Hii tuhuma ni nzito serikali ilifanyie kazi. Watuhumiwa ni jeshi la polisi sababu chuo cha polisi kilihusika kuwapokea na kuwapatia huduma za awali kwa malipo ya pesa taslim, sasa huyu msemaji anapowataka walalamikaji kutuma UJUMBE (yaani sms) kwa IGP inaleta picha gani? yaleyale ya tume ya .... kifo cha Mwangosi. Kama nakumbuka vizuri, mwaka 2001 pale Kituo cha polisi msimbazi mishahara ya polisi iliibiwa palepale ndani, yaani walijiibia wenyewe hatukusikia anafungwa mtu.

Sasa tatizo limekua, sasa ni janga la kitaifa. Kila intake inapoingia chuoni huwa ina taratibu zake, kama idadi,bajeti n.k. sasa hao watu zaidi ya 200 walipitaje getini pasi kuhakikiwa majina yao, na chakula walichopewa (naamini hawakulala na njaa) bajeti yake iliidhinishwa na nani? Mimi nafikiri kama shida ni ushahidi basi huyo mkuu wa chuo pamoja na Komba wanatosha.

Lakini pia huu ni udhaifu wa wazi wa mkuu wa jeshi la polisi. Kama Rais aliyemteua akimwacha, basi hili ni pigo jingine kwa seriksli yake. Mkuu wa chuo asisubiri kufukuzwa nashauri akabidhi tu ofisi aondoke zake lakini ashitakiwe pia
 
Hii naiona ni national security issue na uzembe uliokithiri. Ukipewa gharama ya hao watu 200 kulala na kula hapo chuoni kwa usiku mmoja tu utazimia! Hata viwembe vya kunyolea navyo vyauzwa!!!

Kana-Ka-Nsungu upo!? Ulipotea sana mzee mkubwa, karibu tena. Haya mambo yote ya rushwa na mengine mengi ya kushangaza yanafanywa na hii serikali ya CCM kwa ridhaa ya Watanzania. Kwa madudu kama haya na mengine mengi yaliyokwisha fanywa na hii serikali, bado wananchi wanawarudishia madiwani 22?? Ajabu! na bado mengine mengi ya kushangaza na kufadhaisha yatafanywa. Kupanga ni kuchagua.
 
Kama mchangiaji mmoja amesema kuwa polisi ni sehemu ya jamii, na jamii yetu inabudu rushwa, je sisi kwa nini tushangae polisi kula rushwa? mbona wajumbe wa chama ................., walikuwa wanachukua rushwa hadharani na vyooni hatukuona kama hilo ni tatizo, wamechukua polisi tunaifanya ni issue, washughulikieni kwanza wale waliokuwa wanatoa na kupokea rushwa wakati wa uchaguzi wa chama cha ............. zaidi ya hapo waacheni polenio waendelee na maisha yao.
 
Rushwa iko mpaka Makao Makuu ya Polisi aliko Mwema mwenyewe ambako hata kupelekwa kozi na kupata cheo kuna bei yake! Sishangai kabisa kuwepo kwa mtandao wa aina hiyo ambao ukiu'trace'utakupeleka Makao Makuu.

Polisi ya kweli ilshaendaga miaka mingi na Nyerere na sasa tuna waganga njaa.
 
kama U-IGP jamaa alipewa kwa sababu ni shemeji bila merit yoyote maana hata u-RPC mbeya ulimshinda kaukimbia, mlitegemea nini?
 
Kwa kweli nimesikitishwa sana na taarifa hii kama ni ya kweli


yan vijana kwa masikito makubwa kabisa wametapeliwa pesa zao,na kazi pia wamekosa

mbaya zaid wakafikia had hatua ya kuwanyoa nywele zao

hebu pata picha na upara wako safi tuh unaingia kwenye gari kurudi makwenu,,kweli hii ni haki??

Poleni sana ndugu mliokumbwa na mkasa huo
 
Back
Top Bottom