Kashfa: Tigopesa wanadhulumu hela za wateja?

Kashfa: Tigopesa wanadhulumu hela za wateja?

Wakuu Naomba hili tuliangalie kwa jicho la tatu .

Kuna malalamiko mengi sana kuhusiana na ucheleweshaji wa kurudisha fedha za wateja zinazotumwa kwa makosa kwa watu wasiohusika .

Ukiongea na customer care unaambiwa fedha zako ziko salama na utarudishiwa ndani ya masaa 24 lakini hawarudishi hata baada ya wiki , ukiwauliza unaambiwa utaratibu ni lazima wawasiliane na yule uliyemtumia hela , na kwamba kutokupatikana kwake ndio sababu ya kuchelewesha kurudisha hela , uongo mtupu ! Maana ni kwamba wateja wote hata kama wako hewani , hakuna ofisa yeyote wa Tigo anayejishughulisha kuwapigia simu kama wanavyodai , Tatizo liko wapi ? Ni kweli kwamba baadhi ya watu wa kitengo cha fedha si waaminifu kama nilivyodokezwa na mtu wa jikoni ? Na kwamba wanasubiri baadhi ya wateja wakate tamaa ili wazipige hela zao ?

Viongozi wa TIGOPESA tupeni majibu .

NB - UZI HUU NI WA UCHUNGUZI NA UTAENDELEA KUONGEZWA NYAMA KWA KADRI TAARIFA ZINAVYOTUFIKIA .
Mimi ni mmja wa waathirika wa tigo hawajarudisha hela yangu yangu tarehe 17-8-2016
 
Hamien voda vida raha sana customer wao

Lakin kwa wenzetu kenya ukikosea kutuma ikienda jwa mtu mwingne hayo andika maumivu maana hairudish na kama huyo mtu akinunua tu salio kwa hyo m.pesa n bhas kabsa uwezekano wakurudi n bhas hata uangaike na customers care wanakwambia kabisa umeshafeli

Safarcom n hatar sana
 
Wakuu Naomba hili tuliangalie kwa jicho la tatu .

Kuna malalamiko mengi sana kuhusiana na ucheleweshaji wa kurudisha fedha za wateja zinazotumwa kwa makosa kwa watu wasiohusika .

Ukiongea na customer care unaambiwa fedha zako ziko salama na utarudishiwa ndani ya masaa 24 lakini hawarudishi hata baada ya wiki , ukiwauliza unaambiwa utaratibu ni lazima wawasiliane na yule uliyemtumia hela , na kwamba kutokupatikana kwake ndio sababu ya kuchelewesha kurudisha hela , uongo mtupu ! Maana ni kwamba wateja wote hata kama wako hewani , hakuna ofisa yeyote wa Tigo anayejishughulisha kuwapigia simu kama wanavyodai , Tatizo liko wapi ? Ni kweli kwamba baadhi ya watu wa kitengo cha fedha si waaminifu kama nilivyodokezwa na mtu wa jikoni ? Na kwamba wanasubiri baadhi ya wateja wakate tamaa ili wazipige hela zao ?

Viongozi wa TIGOPESA tupeni majibu .

NB - UZI HUU NI WA UCHUNGUZI NA UTAENDELEA KUONGEZWA NYAMA KWA KADRI TAARIFA ZINAVYOTUFIKIA .

Me kuna laki moja wanayo Paka Leo since sept.kila nkipiga cmu hola
 
Nina jamaa yangu alizuiliwa laki na 45 ni mwezi sasa hajarudishiwa.....
Hawa ni wezi hatarii
 
Iyooo ni kweli kabisa walitusumbua sana kama wiki mbili ikabidi tuwafuate makao makuu. Makumbusho na bado tukaenda mpaka mlimani city ndo wakatuambia twna tusubiri baada ya masaa 24 itarudi...aseee waache uspoti spoti kabisa na pesa za watu
 
Hameni minilishatupa lain siku nyingi niko Airtel na Vodacom baada ya kuwashitukia na kulaumiwa na kuwa tigo mfilisi
 
Wadau inabidi tushauriane nini cha kufanya na hatua zipi tufuate maana mimi hawa tigo wameshanilizia 103000 niliituma kimakosa toka tarehe 25/12/2016 mpaka leo sijaipata na huduma kwa wateja kila siku wananipa masaa ya kusubiri..
 
Mimi nilituma hela kutoka tigo kwendaa airtell elfu 50 kwa bahati mbaya nikawa nimekoasea namba nilituma kwa mtindo wa hela kuingia kwenye account moja moja baadae nikawasiliana na tigo wakanizungusha baadae wakanambia hela imeshatolewa na wakati mimi nikiipiga ile namba haipatikan nikaenda airtell wakasema hiyo line ilikuwa inadaiwa so sytem ime deduct hiyo hela had huyo mtu aje aweke hela ndio wao wataiota kuiruhisha tigo huyo mtu mwenyewe alikiwa anadaiwa 110,000 alikopa kwenye timiza sasa hapo nilishindwa kuelewa nani alitakiwa kusimamia haki yangu na nani kaniibia maan kama nime comfirm hela ni zangu na nimekosea kutuma why niwajibike kulipa hela mtu mwingine policy zao sizijui ndio maana sikujua pakuamzia nilirud tigo nikawaelezea ishu kamili wakasema hwana cha kufanya sababu hela ipo mikononi mwa airtll..nipo dar na nilienda tigo mliman city na airtell miliman city na morroco had niakaachana hiyo hela...jiulize aliepo mkoani..!

duh aisee pole sana kwa maelezo hayo maelezoyako hiyo hela hesabia tu kama umetoa sadaka. inauma kwakweli
 
Kwanza kabisa pole kwa usumbufu kama mteja wa tigo/pesa.
Kama unatuma pesa kwa mteja wa tigopesa alie sajiliwa JINA LINATOKEA kukosea kupo lakini kukurejeshea pesa baada ya kukosea kuna njia zake n utaratibu wake.Mfano: A kamtumia B lakini A kumbe kamlipa deni B lakini yy A anasema kakosea ndio ugumu unapo kuja ni mpk B apigiwe simu kisha akubali kua kweli kapokea kima kosa hyo pesa.
Kutuma pesa kwenda MTANDAO MWINGINE hii kweli changamoto kiasi kwakua ukituma pesa AIRTEL/VODA/ZANTEL kimakosa.Cha kwanza kabisa piga kule waifungie ile line iliyopokea pesa kimakosa.Baadae ndio upige tigo kwa msaada zaidi.
Na kwa mteja ambaye HAJASAJILIWA wa tigopesa jitaidini kutuma kwa FUMBO LA SIRI ambayo hawezi toa mpk apate namba yako ya simu.na kwa hii uwa inarejea kwako mara baada ya kumaliza kuongea na namba 100.Au baada ya siku 7 hata kama hujaongea na namba 100.
Hili ndio linaongoza zaidi kwa wateja wasio wa aminifu kupata huduma za kimwili {ngono} na kumlipa mtu wake pesa.Baada ya kumaliza haja zao wanazuia pesa wakisema wamekosea kutuma.
Ndio zinazo chelewa sana.
Au mdeni n mdeni /VIKOBA/UPATU//WAPENZI.
Nashea nanyi kama WAKALA/MTEJA WA TIGOPESA.

bora umeeleza vizuri vikaeleweka, ila je kama namba haipatikani kabisa, mfano mimi nna laini ya tigo niliisajili lakini sijawah itumia nna kama miezi miwili
 
Mimi wameshanipiga Mara 3. Mwezi mei, mwezi septemba na Oktoba. Jumla elfu 6500 hv. Wabaya sana Tigo kwa sasa. Tutafute ufumbuzi.
 
Tigo ni jipu. Ukiweka salio na kama hujajiunga na kifurushi chochote lazima huwa wanakukata tu
Hili ni pigo kubwa sana kwa watumiaji wengi wa tigo. Huwa siachi hata sh 1. Nikiweka salio najiunga basi. Hio ndio pona ya hela yangu.
 
Voda wanaiba tu salio la vocha...

Kwenye M-pesa wamefaulu uaminifu.

Tigo hovyo kabisa, ndio maana walipewa cheo cha ule mchezo mchafu...
Voda huwa hawaibi salio la vocha. Ukiwa unaona salio lako linapungua baada ya kiweka vocha jaribu kuhakiki mambo haya;
1. Angalia kama kuna huduma za kulipia ulizojiunga nazo. Mfano: Caller tune, huduma za kupata habari kama nipashe, kabumbu, mwananchi, sokoni, etc..

2. Angalia kama simu yako ni Tecno au Aitel. Hizi simu huwa zinakuwa na uwezo wa data hata zikiwa zile simu ndogo za burtton. Hakikisha umezima data.
Aidha, kama unatumia smartphone hakikksha umezima data kabla ya kuweka vocha.

3. Hakikisha hudaiwi nipige tafu.

Nasisitiza tena, VODACOM HAIWEZI KUKUIBIA VOCHA
 
Voda ndiyo wanaboa zaidi ukituma pesa transaction yao inaonyesha jina mwishoni kabisa baada ya kubonyeza 1

Hii inafanya watu wengi kutuma pesa kusikokusudiwa kimakosa,,

Tigo inakupa option ya kuhakiki jina la mtu unaye mtumia kabla ya kubonyeza 1.
Ila Naunga hoja hawa Customer service wanaboa kupita maelezo.
Ulishawahi kutuma pesa kwa kutumia vodacoma wewe?
 
kiukweli hawa jamaa mi siwaelewi kabisa..tarehe 17/11 nilituma pesa kimakosa kwenda kwa mtu wa voda 50,000/=, baada ya kugundua nimekosea hapo hapo nikampigia sim yule niliyemtumia akawa hapatikani niawema afadhali hapatikani atakua hajaitoa,nikapiga sim tigo hapo hapo wakasema wewasiliana na watu wa voda hela wameizuia huyo mtu hawez kutoa nisubiri masaa 72 pesa itarudi,nikasubiri zaidi ya masaa 72 nikawapigia wakasema nisubir tena masaa 72 kama huyo mtu atakua hajatoa pesa watarudisha,nnachoshangaa kivip huyo mtu awe katoa pesa wakati nili toa taarifa mda mchache baada ya kukosea na vip iwezekane atoe pesa wakati hapatikani mda wote(maana nilikua nampigia almost kila siku,na nilimtumia text incase akipatikana ntapata delivery report),nikasubir tena masaa 72 nilipowapigia wakaanza kuongwa kwa ukali,nikawapigia voda nao sikuwaelewa...hadi leo pesa yangu haijarudi na tule mtu haptikani mpaka leo..hivi TCRA hawahusiki na hizi kesi?
Ni pm namba uliyoitumia hiyo pesa mkuu
 
Voda huwa hawaibi salio la vocha. Ukiwa unaona salio lako linapungua baada ya kiweka vocha jaribu kuhakiki mambo haya;
1. Angalia kama kuna huduma za kulipia ulizojiunga nazo. Mfano: Caller tune, huduma za kupata habari kama nipashe, kabumbu, mwananchi, sokoni, etc..

2. Angalia kama simu yako ni Tecno au Aitel. Hizi simu huwa zinakuwa na uwezo wa data hata zikiwa zile simu ndogo za burtton. Hakikisha umezima data.
Aidha, kama unatumia smartphone hakikksha umezima data kabla ya kuweka vocha.

3. Hakikisha hudaiwi nipige tafu.

Nasisitiza tena, VODACOM HAIWEZI KUKUIBIA VOCHA
Aliyeibiwa ni mimi au wewe?

Na waliahidi kurudisha salio langu ila mpaka kesho hawajanirudishia.

Pathetic!
 
Back
Top Bottom