Karibuni mjiunge na chama cha kijamii

HOTUBA YA UTAMBULISHO WA CHAMA KIPYA CHA SIASA NCHINI CHA CCK

Itikadi yake Itikadi ya CCK ni uhafidhina wa kijamii na kiuchumi. Yaani, socio-economic conservatism. Itikadi hii msingi wake ni historia yetu kama taifa na kama jamii ya watu. Tunaamini kuwa tishio kubwa kabisa katika jamii yetu ni kuvunjwa vunjwa kwa familia ya Kiafrika na vile vile matumizi makubwa ya serikali kwenye mambo mengi ambayo kwa kweli serikali isingestahili kuwa inayafanya.

Hivyo, CCK ni chama ambacho kinataka kutetea na kuyahifadhi mambo ya msingi yanayoifanya jamii yetu kuwa ya Kiafrika katika ulimwengu wa kisasa na hasa kutetea na kulinda familia. Tunaamini kabisa kuwa sera zozote na mipango yoyote ya nchi ambayo haiweki mkazo katika kuipa nafuu na kuboresha maisha ya familia sera hizo ni za kutupwa mbali.

CCK ni Conservatives? Kweli, kuna desturi na maadili mengi sana yamemomonyoka, lakini hamuoni kwamba kila mtanzania anakimbilia modernity? ambayo ipo ndani ya demokrasia na maendeleo?

Kwa muda mrefu sasa nchi yetu imejiingiza kwenye sera zenye kutukuza kile kinachoitwa "soko" matokeo yake wakati wenye "soko" wakiendelea kufanya vizuri mamilioni ya familia za Watanzania wanaishi maisha ya wasiwasi wa kudumu. Hivyo, tunataka kupendekeza sera ambazo zitalenga kuinua maisha ya wananchi wetu na hivyo kuinua maisha ya familia.

Kuna makala ya mchambuzi alitueleza kwamba soko lipo tu chini ya mfumo wowote na kwamba Soko lilikuwepo enziii, hata kabla ya ubepari kuingia duniani. Chini ya ubepari, soko limebadilika tu na kuwa soko huria.

Katika kutengeneza itikadi hii mpya chama chetu kitachota pasipo haya wala kuomba radhi katika hazina ya hekima ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na kujifunza huku tukiboresha nadharia zake nyingi ambazo tunaamini ni msingi wa kujenga taifa la watu walio sawa na wenye kuheshimu utu wa watu wote.

HIvyo, tutapinga ubaguzi wa aina yoyote dhidi ya Mtanzania mwingine, tutapigania maadili bora ya viongozi na kuhakikisha kuwa misingi iliyiounda taifa letu ikiwemo kupigania umoja wa Afrika, usawa na haki vinasimamiwa tena. Hatutavumilia kauli za kibaguzi zitakapotolewa na kiongozi au taasisi yeyote; kama Mwalimu alivyosema "Tanzania ni ya wote, na Watanzania ni wote"

Mwalimu Nyerere na Ubapari tena? Mchambuzi pia alitukumbusha lengo kuu la Ujamaa ni kuleta mapinduzi ya kumwangamiza bwanyenye, sasa vipi tena hapo Nyerere na Ubepari? Mapinduzi ya CCM yalikuwa kumtupilia mbali Bwanyenye. Lakini tofauti na zamani, hivi sasa, Bila ya Mabwanyenye, CCM haiwezekani. Na hawa ndio wamekamata Chama, na wanalisha sumu wale wanaotaka kuendeleza flfasa ya MAPINDUZI katika CCM. Jifunzeni kwa Nape.

Kwa kweli ni chama mbadala hasa wa CCM na kinataka kuwarudishia wananchi wa Tanzania fahari yao. Tunataka kurudisha ule moyo wa uzalendo, kuipenda Tanzania na kuona fahari kuwa sisi ni Watanzania.

Kuna kilicho mbadala wa CCM zaidi ya Chadema? CDM tunachukua nchi 2015. Prove me Wrong!!!
 
mzee 6 , mwakyembe na nape watajiunga lini?

attachment.php



Wagonjwa hao wataweza kutuongoza kweli???
 
AKITANDA WEW NI MGENI HAPA AU??UKIPOST KITU KAMA HIKI NI LAZIMA URUDI NA KUJIBU MASWALI SASA WEWE UNAWEKA NA KUKIMBIA KAMA UMEJISAIDIA MAHALI NA KUONDOKA SIO SAWA RUDI HAPA UJIBU MASWALI,MIMI NITAJIUNGA NA CHAMA CHAKO KAMA UTAJIBU KWA UFASAHA HAYA YAFUATAYO

-CCK KINA KATIBA,kama ipo weka hapa kama hamna mna mpango gani
-UCHAGUZI WA CCK ULIFANYIKA LINI-umesema wewe ni mwenyekiti wa CCK taifa,mlichagua lini??
-CCK ina wanachama wangapi kila Mkoa tafadhali
-JE CCK MNA OFISI YA KUDUMU??
-MNAPATA HELA ZENU KUTOKA WAPI??
-MISINGI YENU IKOJE KULE UPANDE WA PILI WA JAMHURI(PEMBA NA UNGUJA)


JIBU HAYO HALAFU NITAULIZA MENGINE BAADA YA MAJIBU YAKO,USISAHAU KUWEKA HAPA FOMU YA KUJIUNGA NA GHARAMA ZENU

miongoni mwa taratibu za kupata walau usajili wa muda ni pamoja na kuwa na katiba,sasa kwa chama kilichopata usajili wa kudumu ni wazi hilo si swali,

kuhusu uchaguzi, ni kuwa hakuna chama kisichokuwa na uongozi wa kukianzisha na sie ni miongoni mwao,tunataraji kufanya uchaguzi kuanzia ngazi ya matawi,kata,wilaya,mkoa na taifa muda si mrefu,karibu ujiunge na upate nafasi ya kugombea

sifa za kupata usajili wa kudumu ni angalau kuwa na wanachama 200 kwa mikoa kumi,kati ya hiyo miwili itoke zanzibar

kuhusu ofisi zetu,zipo za muda sinza maeneo ya legho

pesa zetu zinatoka kwa wanachama wanaokichangia fedha na rasilimali mbalimbali wakijua hiki ndio chama chao cha kuleta ukombozi wa kweli.

swala la muungano ni hoja pana ambayo kupitia mchakato wa katiba mpya,kila mtanzania atapata nafasi pana ya kutoa mawazo na mtazamo wake katika hilo
 
Naona mmefanyia kazi utabiri wa Shekeh Yahaya. Kimsingi, kuitikia witu wa mtu aliyekuwa akiongozwa na mashetani maana yake ni kuiweka nchi chini ya majini na mashetani. Ni tatizo hili hili ambalo limepelekea nchi yetu kuwa katika hali ngumu ya kiuchumi, kielimu na kisiasa.
Ningependa kuuliza ni nini hasa mlichoona hakikidhi haja zenu katika siasa za upinzani mpaka mfikie maamuzi haya. Chadema katika siku za karibuni wamekuwa wakifanya vizuri sana. Kwa nini msingewaunga mkono ili kuweza kukamilisha ukombozi wa nchi? Je ni nini kitakachonishawishi nisiamini kwamba ninyi mnatumika kisiasa kupunguza kura za upinzani ambao chadema imeujenga? Hivi ninyi magamba mtaendelea kuigawa nchi yetu hata lini?


hapo kwenye red: hii inaonyesha namna watanzania tulivyo wavivu wa kufikiri,haiingii akilini kudhani ya kuwa ukiwa mwanachama wa magwanda basi wewe ndo mpinzani,NAAMINI kabisa kuwa chama ni itikadi,itikadi ni imani,kama itikadi yao hao CCK haifanani na chama cha magwanda ni sahihi kabisa kuwa na chama cha itikadi wanayoiona inafaa,itakumbuklwa hata CUF waliwahi kusema chadema wametumwa wakati wa uchaguzi wa mwaka 2005,ni kama vile walitaka kuungwa mkono wao tu na si wengine kusimama kivyao,hii ni changamoto na ni lazima tuikubali
 
CCJ= Chukua Chako Jiondoe (ISSUE IMEKAA KI RUZUKU RUZUKU)

soma hapa tafadhali,maana inaonekana watu hamsomi na mnakurupuka kujibu


Mfumo wa siasa hapa nchini Mojawapo ya matatizo makubwa ambayo yanatusumbua sasa hivi nchini na ambayo athari zake zinatoka kizazi kimoja kwenda kingine ni mfumo wetu wa kisiasa nchini. CCK inaamini kuwa mfumo huu wa kisiasa umepitwa na wakati na hauendani kabisa na matamanio ya kujenga taifa la kidemokrasia. Baadhi ya vitu ambavyo tunaamini vimepitwa na wakati na ambavyo vinahitaji kuondolewa mapema zaidi ni suala la ruzuku kwa vyama vya siasa.

Mfumo wa ruzuku uliingizwa kwenye siasa zetu na CCM kwa ajili ya kutafuta njia rahisi ya kupora raslimali zetu na kujinufaisha kwa migongo ya Watanzania. Hakuna sababu wala ulazima wa chama cha siasa kupewa fedha za umma kwa sababu tu ina watu waliochaguliwa kushika nafasi mbalimbali – huu ni wizi wa wazi! Sisi kama CCK tunataka na tutapigania hatimaye kuondolewa kwa mfumo huu wa ruzuku kwa vyama vya siasa kwani vinazawadia uzembe na ubadhirifu.

Iweje chama ambacho kimeshindwa kusimamia serikali yake na ufisadi umeshamiri chini yake bado kinapewa kila mwezi mabilioni ya fedha ambayo hayajafungwa na utendaji kazi wa chama hicho?

Yaani, haijalishi CCM inatawalaje lakini bado inalipwa kila mwezi na Watanzania! Hivyo, kinyume na vyama ambavyo vinaweza kudaiwa kuwa vimeundwa kwa ajili ya ruzuku CCK imeundwa huku ikiwa inatambua kuwa mfumo wa ruzuku ni wa hatari kwenye siasa zetu na kwa kweli ndio umechangia sana kuchelewesha kung’olewa kwa CCM madarakani!

Hivyo, katika mjadala wa Katiba Mpya sisi kama chama tutapigania na kuhakikisha kuwa ruzuku kwa vyama vya siasa zinafutwa ili kila chama kitegemee wanachama wake na akili zake kujiendesha. Kwani TANU ilipewa ruzuku na serikali ya Mkoloni ili ifanye siasa? Si ilitegemea wanachama wake? Kwanini kama wakati huo iliwezekana leo ishindikane?
 
soma hapa tafadhali,maana inaonekana watu hamsomi na mnakurupuka kujibu


Mfumo wa siasa hapa nchini Mojawapo ya matatizo makubwa ambayo yanatusumbua sasa hivi nchini na ambayo athari zake zinatoka kizazi kimoja kwenda kingine ni mfumo wetu wa kisiasa nchini. CCK inaamini kuwa mfumo huu wa kisiasa umepitwa na wakati na hauendani kabisa na matamanio ya kujenga taifa la kidemokrasia. Baadhi ya vitu ambavyo tunaamini vimepitwa na wakati na ambavyo vinahitaji kuondolewa mapema zaidi ni suala la ruzuku kwa vyama vya siasa.

Mfumo wa ruzuku uliingizwa kwenye siasa zetu na CCM kwa ajili ya kutafuta njia rahisi ya kupora raslimali zetu na kujinufaisha kwa migongo ya Watanzania. Hakuna sababu wala ulazima wa chama cha siasa kupewa fedha za umma kwa sababu tu ina watu waliochaguliwa kushika nafasi mbalimbali – huu ni wizi wa wazi! Sisi kama CCK tunataka na tutapigania hatimaye kuondolewa kwa mfumo huu wa ruzuku kwa vyama vya siasa kwani vinazawadia uzembe na ubadhirifu.

Iweje chama ambacho kimeshindwa kusimamia serikali yake na ufisadi umeshamiri chini yake bado kinapewa kila mwezi mabilioni ya fedha ambayo hayajafungwa na utendaji kazi wa chama hicho?

Yaani, haijalishi CCM inatawalaje lakini bado inalipwa kila mwezi na Watanzania! Hivyo, kinyume na vyama ambavyo vinaweza kudaiwa kuwa vimeundwa kwa ajili ya ruzuku CCK imeundwa huku ikiwa inatambua kuwa mfumo wa ruzuku ni wa hatari kwenye siasa zetu na kwa kweli ndio umechangia sana kuchelewesha kung’olewa kwa CCM madarakani!

Hivyo, katika mjadala wa Katiba Mpya sisi kama chama tutapigania na kuhakikisha kuwa ruzuku kwa vyama vya siasa zinafutwa ili kila chama kitegemee wanachama wake na akili zake kujiendesha. Kwani TANU ilipewa ruzuku na serikali ya Mkoloni ili ifanye siasa? Si ilitegemea wanachama wake? Kwanini kama wakati huo iliwezekana leo ishindikane?

Maandishi ni jambo lingine na utekelezaji ni jambo lingine, CCM kina sera nzuri sana lakini je zinatekelezwa? kadi ya mwana CCM nyuma imeandikwa hivi:
Rushwa ni adui wa haki, sitotoa wala kupokea rushwa, nitasema kweli daima fitina kwangu mwiko.
Kwahiyo hizo ngonjera mlizojaza hapo kuwalaghai Watanzania hazina mashiko.
 
hongereni kwa kuona umuhimu wa jf kuwafikia watz!

lakini labda mtueleza ni madhaifu gani mliyoyaona kwenye vyama vilivyopo kiasi kwamba mshindwe kuyatatua na muamue kuunda chama kipya!?

Kila la kheri maana safari hii ni ngumu
 
Kwa sasa hivi silipwi, umenoa, jaribu tena baadae! Tena nilishawahi kumtumia Nape PM kuwa waanze kunilipa maana mashambulizi nnayopata hapa JF yakiambatana na matusi si kazi ndogo. Kanchunia.

Vipi, Mbowe analipa?
Mimi ni mfadhili wa Demokrasia natumia resource zangu kuchangia mabadiliko wala bila kuwa na nia ya uongozi wa kisiasa, na mara nyingi tu nimewafadhili wanaCCM mtaani kwangu kwa shughuli zao za kichama ikiwemo hata kutoa gari yangu kuwasaidia misafara yao.
Nina mahusiano mazuri tu na wanaCCM mtaani kwangu na bado sijamuuwa kuwa mwanachama wa Chadema, nazifahamu siasa za Tanzania vyema.
 
Back
Top Bottom