Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,405
Karibu tena baba baada ya kuugua zaidi ya mwaka....
Mungu ni Mkubwa na azidi kuaminiwa na kuabudiwa. Hivi punde, Samuel Sitta ameomba mwongozo wa Spika na kuomba Professor MWandosya ajitambulishe na kusalimia wabunge kwani sasa afya yake imerudi katika yake ya kawaida. Na kweli, kiongozi wetu huyu mpendwa akasimama na kwenda kwenye podium kwa ukakamavu kabisa na kutoa maneno machache ambayo kama kawaida, hufanya ukumbi husika utulie kama maji kwenye mtungi. Professor amewashukuru watanzania wote waliokuwa wanamuombea usiku na mchana, na vile vile Rais, makamu wa rais, na wabunge wa vyama vyote vya siasa. Baada ya kusalimia wabunge na kutoa shukrani zake, Mh Sitta akamuomba Mwandosya amsalimie Zitto kabwe on his way kwenda kuketi, na akafanya hivyo na kumpa mkono Mh. Zitto ambae nae akapata wasaa wa kumsalimia Mwandosya na kumkaribisha kama naibu kiongozi wa kambi ya upinzani.
Sala zetu mwenyezi mungu hakika amezisikiliza kwani ni jana tu tulikuwa tunamzungumzia hapa. Hatukukata tamaa, na faida yake tumeiona sasa. Tulimkosa kwa muda mrefu sana, lakini sasa tunae tena. Sala zetu zisiishie hapa, ziongezeke mara dufu kwani ndizo zitakazomlinda mzalendo wetu huyu na msomi ambae dunia nzima inamtambua na kumheshimu. Hakujatokea kipindi kingine ambacho tuna muhitaji Prof Mwandosya kama kipindi hiki. Najivunia kuwa CCM kwa sababu ya mtu huyu.
Karibu sana Professor Mwandosya, Tupo nyuma yako mpaka pale mwenyezi mungu atakapoamua vinginevyo.
Mungu ni Mkubwa na azidi kuaminiwa na kuabudiwa. Hivi punde, Samuel Sitta ameomba mwongozo wa Spika na kuomba Professor MWandosya ajitambulishe na kusalimia wabunge kwani sasa afya yake imerudi katika yake ya kawaida. Na kweli, kiongozi wetu huyu mpendwa akasimama na kwenda kwenye podium kwa ukakamavu kabisa na kutoa maneno machache ambayo kama kawaida, hufanya ukumbi husika utulie kama maji kwenye mtungi. Professor amewashukuru watanzania wote waliokuwa wanamuombea usiku na mchana, na vile vile Rais, makamu wa rais, na wabunge wa vyama vyote vya siasa. Baada ya kusalimia wabunge na kutoa shukrani zake, Mh Sitta akamuomba Mwandosya amsalimie Zitto kabwe on his way kwenda kuketi, na akafanya hivyo na kumpa mkono Mh. Zitto ambae nae akapata wasaa wa kumsalimia Mwandosya na kumkaribisha kama naibu kiongozi wa kambi ya upinzani.
Sala zetu mwenyezi mungu hakika amezisikiliza kwani ni jana tu tulikuwa tunamzungumzia hapa. Hatukukata tamaa, na faida yake tumeiona sasa. Tulimkosa kwa muda mrefu sana, lakini sasa tunae tena. Sala zetu zisiishie hapa, ziongezeke mara dufu kwani ndizo zitakazomlinda mzalendo wetu huyu na msomi ambae dunia nzima inamtambua na kumheshimu. Hakujatokea kipindi kingine ambacho tuna muhitaji Prof Mwandosya kama kipindi hiki. Najivunia kuwa CCM kwa sababu ya mtu huyu.
Karibu sana Professor Mwandosya, Tupo nyuma yako mpaka pale mwenyezi mungu atakapoamua vinginevyo.