Let me conclude!! Na wanaume wasio na pesa+six packs ndo wanaongoza na majibu mabaya huku jf???hahahah ni mtazamo tuuuu
Ha ha ha ha haa umejuwaje?
Let me conclude!! Na wanaume wasio na pesa+six packs ndo wanaongoza na majibu mabaya huku jf???hahahah ni mtazamo tuuuu
Wanajeshi wapo warembo, acha kabisa, hasa wale wadada wanaopiga gwaride kiustadi, dah, nawapenda sana. Unakuta mdada kavaa magwanda yamemkaa vizuri, ana nidhamu halafu anapiga gwaride kama vile anaongozwa kwa remote, akishika bunduki hasa ile niipendayo, dah full kunitia mzuka!
Wadada wabaya ndio wanaoongoza kwa kauli mbaya.
Mara nyingi nikienda maofisini kutafuta huduma mbalimbali napokelewa na akina dada. Sasa katika "observation yangu for years". Nimekuja kugundua kuwa wadada wengi wabaya (tabia, roho, wanavyovaa, makeup, moods zao, feelings, mawazo, perception zao towards themselves (kujikubali au kujikataa) and towards others, namna wanavyochangamana na watu, communication skills, etc., - hivi vyote na vingine ndivyo vinawafanya akina dada wawe wabaya au wazuri) wana kauli chafu/mbaya.
Utawakuta muda wote wana hasira, hawako tayari kukusikiliza au kukuhudumia, yaani watakuhudumia kwa kujilazimisha wee mpaka kero. Usiombe afungue mdomo kama unamwuuliza kitu, kauli yake unaweza kuzimia!
Lakini wadada wazuri ukikutana nao, hata kama ulikuwa unamtafuta The Boss - labda, Manager, Mkurugenzi, Headmaster, dah, shida yako inaweza kuishia hapo!
Yaani unakuta mdada sauti nyororo (natural, sio ile fake kama Mmarekani), anakusikiliza vizuri, halafu anakuangalia machoni, macho safi yanang'aa halafu yanablink blink kidogo kwa mbali, aibu kidogo ya kishikaji, amevaa vizuri, halafu anapendeza, hakuna kitu chochote fake mwilini mwake (vinavyoonekana, huko ndani sjui, anajua yeye).
Wadada wazuri mara nyingi wamenikaribisha vizuri "Mambo kaka? Karibu, karibu kiti, nikusaidie nini kaka? Kama ukimweleza umepata shida kuhusiana na huduma fualani, utasikia "Pole mpenzi", akiwa romantic sana "pole mpenzi wangu, nafuatilia swala lako sasa hivi", etc.,
Sasa ukitaka kujua wadada wazuri au wabaya kwa sifa nilizozianisha hapo juu. Fuatilia comments zao au kauli zao humu Jf, hawajifichi ng'o. Hata kama huwajui lakini haiwezekani "consistently" mtu akawa na kauli kama maji ya ndimu, ndio tabia zao. Kwa hiyo, wale mnaodate online hasa Jf, kama unataka/hutaki garasha, anza na comments au threads zake.
NB: Sitaji mtu, sitaki kesi. Over
Weka picha
Kutana na traffic mwanamke mweusi halafu akamate gari la mdada mweupe......
nadhan itafika mahali ndoa zitakuwa hamna kabisa.....DEMBA ndoa zenyewe ni ndoa sasa, hivi ukihesabu ndoa zenye sifa za kuitwa ndoa, mfano, hapa mjini Dar zitazidi 100 kweli? Ndoa siku hizi ni kama academic certifications, alimradi tu mtu aweke rekodi naye ameoa au kuolewa.
aiseee. watu wataka kubembelezwa bana. tuwabembeleze waume zetu majumbani. tukawabembeleze watu maofisini. hivi nyie kuweza?
oa mwanajeshi!
hapo sasa!!
yani hata mtu ukireply vibaya, mdau anavunja pc! teh teh!
Aiseeee.
Binadamu tuna sura nyingi.
Binadamu sisi tukiona hali ya hewa ni safi/shwari lazima tutamani kuichafua.
Binadamu sisi tulio chafua hewa ,tunapo fanikiwa kuichafua kweli kweli basi sisi ndio tunakuwa wa kwanza kuanzisha semina na thread tukiomba hile hewa safi irudi/tukijaribu kusafisha.
Na tukijiuliza kwanini tuna chafua hali ya hewa utasikia oooo tunapenda tuuuu.
ALIYESEMA BINADAMU WOTE TU VICHAA HAKUKOSEA NA KILA LEO USHAHIDI WA MSEMO WAKE UNA PATIKANA.
Aiseeee
Muongo mkuu.
nipo bestito naona twanangwa eti wabaya.......sasa sijui wale wakaka wenye comment mbaya ni wazuri.