Bin Chuma75
JF-Expert Member
- Dec 15, 2012
- 1,003
- 1,102
Wakuu hali ni mbaya kariakoo na viunga vyake, wamachinga wamefunga mitaa yote na baraza zote, hili jambo mkuu baba alizungumzie, hii nchi ni yetu wote, sio wamachinga peke yao. Muheshimiwa baba tuonee huruma na sisi wengine tunaotumia barabara za maeneo ya kariakoo na viunga vyake, wamachinga kwa sasa wamekuwa na jeuri kuliko hata FFU(Fanya Fujo Uone).
Kama kariakoo na viunga vyake vimekuwa ni soko rasmi la wamachinga basi serikali ipige marufuku magari kupita maeneo hayo kwa usalama wa watu na mali zao, maana msukumano uliopo wa wamachinga na waenda kwa miguu ni hatari sana kwenye magari.
Mkuu baba jaribu tu hata kutoka kimya kimya upite maeneo ya kariakoo na viunga vyake uone wananchi tunavyotembea kwa mateso tukihatarisha maisha yetu kwa kugongwa na magari.
Kama kariakoo na viunga vyake vimekuwa ni soko rasmi la wamachinga basi serikali ipige marufuku magari kupita maeneo hayo kwa usalama wa watu na mali zao, maana msukumano uliopo wa wamachinga na waenda kwa miguu ni hatari sana kwenye magari.
Mkuu baba jaribu tu hata kutoka kimya kimya upite maeneo ya kariakoo na viunga vyake uone wananchi tunavyotembea kwa mateso tukihatarisha maisha yetu kwa kugongwa na magari.