Kapten John Komba: Lowassa anafaa kuwa Rais 2015

Kapten John Komba: Lowassa anafaa kuwa Rais 2015

Kama JK ameweza kuwa raisi kwanini EL ama yy mwenyewe Kapteni ashindwe kuwa raisi !
 
Akihojiwa na Salama Jabri kwenye kipindi cha "Mikasi" Mwimbaji Maarufu wa CCM na Kiongozi wa TOT amesema kwa maoni yake binafsi Mwaka 2015 anayefaa kuwa Rais wa Tanzania ni Edward Lowassa.

CC Pasco

Hivi jamani majimbo mengine hayanaga watu wakuchaguwa kuwa wabunge. Na watu wanao ishi kwenye majimbo hayo wanaupeo gani. Mimi kama ningetoka jimbo analowakilisha huyu mjinga ningelikana kabisa
 
Akihojiwa na Salama Jabri kwenye kipindi cha "Mikasi" Mwimbaji Maarufu wa CCM na Kiongozi wa TOT amesema kwa maoni yake binafsi Mwaka 2015 anayefaa kuwa Rais wa Tanzania ni Edward Lowassa.

CC Pasco
Kwani katiba inasemaje vipi si zamu ya Zanzibar 2015
 

Huko Mbinga hakuna watu wanaofaa kuwa wabunge zaidi ya huyo mpenda vitoto, mfikiria tumbo na mzee wa kusinzia Bungeni
"Cap Komba"??

images
images
images
images


Nitakuwa sijamtendea Haki mzee Wassira nisipoweka picha yake ya kusisnzia Bungeni kama Komba ila yeye totoz hapana

images
 
Kapt Komba ajitoa mhanga, asema Lowassa Rais 2015:
komba+bungeni.jpg

"Kujitokeza kwa Kapteni Komba kunafanya hadi sasa idadi ya wabunge waliotangaza msimamo wa kumuunga mkono kufikia wawili"



Dar es Salaam.Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Kapteni Mstaafu, John Komba amevunja ukimya na kutamka wazi kuwa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, ndiye chaguo lake na atakuwa Rais ajaye uchaguzi wa 2015.
Komba anakuwa mtu wa pili kumtaja Lowassa hadharani kuwa anafaa kwa rais 2015.
Itakumbukwa Mbunge wa Viti Maalumu, Beatrice Shelukindo (CCM) naye alivunja ukimya baada ya kutangaza kumuunga mkono Lowassa kumrithi Rais Kikwete.
Shelukindo alitoa kauli hiyo wakati akiwasalimia wakazi wa Monduli baada ya kukaribishwa kuchangia ujenzi wa Hosteli ya KKKT, kwenye sherehe za kukaribisha Mwaka Mpya zilizofanyika nyumbani kwa Lowassa na kuhudhuriwa na makada kadhaa wa CCM.
Akizungumza na Mwananchi katika mahojiano maalumu jana, Komba ambaye ni Kiongozi wa Kundi la Uhamasishaji cha CCM Tanzania One Theatre (TOT Plus), alisema mtazamo wake kwa mtu anayefaa kumrithi Rais Jakaya Kikwete ni Lowassa.
Komba aliyeingia kwenye siasa kutokana na msukumo wa mama yake aliyekuwa msaidizi wa Bibi Titi Mohamed, alisema anazo sababu kuu tano za kumkubali Lowassa kuwa Rais na atasimama popote kumtetea.
“Nakuambia Lowassa ndiye anafaa kuwa Rais... unafikiri kuna mwingine. Nina sababu zangu tatu,” alisema Komba na kuhoji:
“Wewe unakwenda kwenye harambee, nani leo hii anaweza kusaidia kuchangia kwa fedha nyingi na zote hizo ni kwa maendeleo yanayokusudiwa kama siyo Lowassa?”
alisema Komba ambaye ni mahiri katika kuinadi CCM, katika kampeni mbalimbali za udiwani, ubunge na urais.Juu ya kuwa atakuwa katika wakati mgumu endapo anayempigia debe hatokuwa, Komba alisema: “Mimi sikwambii ni nani, lakini wapo Mawaziri waliomkana, lakini leo hii wapo kwenye Serikali hii hii ya Rais Kikwete.
“Mimi nasema Lowassa, na kama akipita sawa nitaburudiiika kwelikweli, lakini kama akiteuliwa mwingine, mimi nitakuwa naye...nitamwimbia hadi mwisho. Kazi yangu si unaijua, nitampigia debe kwa kuwa si mtu wa mtu mmoja, ni uteuzi wa wanaCCM ule si wa Komba.” alisema.
Mbali na kumnadi Lowassa, Komba alisifu uimara wa chama chake kuwa kinaimarika siku hadi siku na ndicho kinachotoa viongozi wa kweli na hata wananchi wanakikubali.
Akizungumzia suala la rushwa ndani ya CCM, Komba ambaye pia ni Mbunge wa Mbinga, alisema kama chama kuna watu wa aina nyingi, kuna wasafi, kuna wachafu lakini wote wako kwenye mstari mmoja.
Alisema kuwa vita ya rushwa ndani ya CCM itamalizika endapo kila kiongozi atasimamia kwenye haki na maadili ya uongozi na pia kutambua wajibu wake ndani ya chama.Komba alijipigia upatu kuwa ameleta maendeleo katika jimbo lake kwani jimbo linatazamika ikilinganisha na miaka ya nyuma kuwa wananchi walikuwa wakiishi maisha ya tabu na kimaskini ilhali wana raslimali za kutosha.


Chanzo: MCL
 
anasumbuliwa na kitambi mwacheni aseme huenda ndo mazoezi ya kukipunguza
 
Hakusema ndiye atakayekuwa rais, bali alisema kama ni chaguo lake angependekeza Lowassa awe rais. Kwa mara ya kwanza leo naungana na huyu mwanakwaya.

Eddo for presidency!!!!
 
mkuu kwanza labda nikuambie tu ukubali ukatae,watu wakigoma na wtz wanatambuw ww ndo adui namba moja wa zitto zuberi,hiz fitna zote za kuchafuliwa kwa zitto kwny mitandao yakijamii ww ben sa nane ndo unayeongoza kundi hilo na hili unalifnya kwa makusudi kabsa kwaajili ya kumridhisha mbowe na babu yenu huyo dr slaa.Na hili umelifnya makusudi baada ya lile jaribio la kumwekea sumu kwenye chakula kushindwa!na hata hapo sahv najuw sahv umejiandaa ni jinsi utahakikisha unamtenganisha mwigamba na roho yake,usifikir tz ni ile ya zaman,yote haya yako waz
Nimeamini wakati mwingine majina tunayojipa yanaleta tashwira halisi ya mtu mbun'go ?? Kweli wewe ni huyo mdudu. Hili jukwaa sio saizi yako kama uliyoandika hapa yanatoka kichwani.
 
Last edited by a moderator:
Hivi jamani majimbo mengine hayanaga watu wakuchaguwa kuwa wabunge. Na watu wanao ishi kwenye majimbo hayo wanaupeo gani. Mimi kama ningetoka jimbo analowakilisha huyu mjinga ningelikana kabisa
bola komba ila kama ningelikuwa natoka ktk haya mjimbo ningehama, mbeya mjini, iringa mjini, nyamagana mwanza kawe Arusha mjini na ubungo nahakika hawa wabunge wao ni viplate vibaya.
 
Nimeamini wakati mwingine majina tunayojipa yanaleta tashwira halisi ya mtu mbun'go ?? Kweli wewe ni huyo mdudu. Hili jukwaa sio saizi yako kama uliyoandika hapa yanatoka kichwani.
hata kiplate akiposte naye anajiona anaweza tenda jambo ktk jamii! hebu jiangalie kwa mara nyingine kisha jitasmini mwenyewe kisha utajua utumbo ulio upost. limbukeni wa mitandao.
 
Last edited by a moderator:
Lowasa ana bahati alishauriwa astaafu na kastaafu maana serikali iliogopa iwapo wananchi wangefahamu kashfa zake toka alipokua waziri wa ardhi mpaka waziri mkuu wasingemkubali hata awe katibu tarafa.Watanzania tusikubali kula matapishi yetu alishaangushwa uwaziri mkuu vipi atakua Rais.
 
Back
Top Bottom