Kapoteza fahamu baada ya kuachwa

Kapoteza fahamu baada ya kuachwa

Mwambie huyo mary kuna wnaume wanatafuta wake hapa,,.
 
Haya mambo haya acheni...bora Mary alizimia..maana kuna kipindi unaomba uzimie afu hauzimii....Ila baadae Mary atajiona mjinga kuzimia coz kaachwa tena si ghafla baada ya maumivu tele!!!anyway mambo mengine tunapitia tujifunze...ndiyo skuli ya maisha.
 
Haya mambo haya acheni...bora Mary alizimia..maana kuna kipindi unaomba uzimie afu hauzimii....Ila baadae Mary atajiona mjinga kuzimia coz kaachwa tena si ghafla baada ya maumivu tele!!!anyway mambo mengine tunapitia tujifunze...ndiyo skuli ya maisha.
Kuna mengi sana ya kumfanya Merry kuzimia, kumbuka wameisha pelekana kwa wazazi, imebaki ndoa tu, na wameanzia mbali, kakataa wanaume wangapi kwa ajili yake?
 
Ilikuwa siku ya Ijumaa jioni nikiwa natoka kwenye miangaiko ya utafutaji, nikapigiwa simu na rafiki yake Marry(Sio jina lake halisi), kuwa Marry yuko hospital amepoteza fahamu. Nilitaka kujua sababu iliyopelekea Marry Kupoteza fahamu hakuweza kusema, kwa haraka ilibidi niende hospital ambayo Marry alikuwa akipatiwa matibabu. Baada ya kufika nilikuta kweli Marry hawezi hata kuongea. Marafiki na wazazi wa Mary nilikuta wamejiinamia chini huku wakitokwa na machozi.

Baada ya Muda Marry alipata fahamu japo hakuweza kuongea kwa Muda huo. Nilipewa sababu ya Marry Kupoteza fahamu na rafiki yake aliyenipigia simu. Niliumia sana baada ya kujua sababu ya Kupoteza fahamu kwa Marry ni kuachwa tena kwa kashfa na mpenzi wake waliyekuwa wanatarajia kufunga ndoa hivi karibuni.

Mimi kama rafiki wa karibu sana na Marry kama ndugu, ambao wote tulikuwa tunafanya kazi katika ofisi moja kabla ya mimi kuondoka hapo, Lakini ukaribu wetu uliendelea kudumu. Marry Muda mwingi alikuwa anahitaji ushauri kutoka kwangu juu ya uhusiano wake na mwenzake, kwani aliona Kuna mabadiliko makubwa kutoka kwa mume wake mtarajiwa, upendo ulipungua, kitu kidogo ugomvi mkubwa, kupungua kwa mawasiliano bila yeye kumtafuta hatafutwi, majibu ya mkato. Lakini Marry aliendelea kuvumilia akijua mpenzi wake atabadilika, matokeo yake kamuacha tena kwa maneno makali yanayojeruhi na kuhumiza moyo, na kuchukua mke mwingine na kutangaza ndoa hapo hapo, kwamba Marry hana sifa ya kuolewa na yeye.

Ushauri Wangu kwa wanajamii: Usikubali kuumizwa na mtu asiyejua thamani yako, usikubali kuwa mtumwa wa mapenzi kwa kukubali kuburuzwa na mtu asiyejali hisia zako, usikubali kuendelea kulilea penzi la Kitapeli lisilo hata na Mwelekeo. Jiulize kwa nini mapenzi ya kulize kila siku? Kwa nini uendelee kuwa na mtu anayekupa karaha kila wakati? Eti bila yeye siwezi kuishi!! Ebo, kwani kabla ya kuwa na huyo uliyenaye hukuwa na maisha? Kwani mlizaliwa pamoja ushindwe kuishi bila yeye ?

Don't cry because it's over, smile because it happened. Know that everything happen for a reason may be it happened to let you know that you are brave or that you should not repeat the mistake again. Stay happy never give up!, show confidence of yourself, focus on the potential of the good stretch your goals. Pray, forgive, make friends. Be happy again.
Mwambie anitafutee
 
Marry ni mwanamke mzuri kwa kumtazama, ana sifa za kipekee kuwa mke. Marry ni mvumilivu, ana heshima kwa kila mtu licha ya usomi wake na kazi anayofanya. Tatizo hakupata mpenzi sahihi kwake.

Ni Mary au Marry?
Majina yenu ya siku hizi ya google yanachanganya sana huku duniani.
 
Back
Top Bottom