Upepo wa Pesa
JF-Expert Member
- Aug 8, 2015
- 21,786
- 35,747
Nilipewa kazi ya kuongea na binti mmoja, ni hivi jamaa yangu mmojaa mbaye yupo vema sana up stairs na yupo ok vya kutosha financially alikuwa Mwanza kwa kazi ya kama 18mnths. Akakapenda kabinti flani ka St Augustine jamaa akaona ngoja akapime kama kanafaa kuwa wife. Jamaa akawa anakasaidia mambo kadha wa kadha ya kifedha ila hakujionesha yupo vizuri kiasi gani na ushauri wa kikasomo. Kalipomaliza chuo kakapiga mtaani mwaka na nusu bila kazi jamaa anakapa pocket money btn kati ya laki na laki tatu kila mwezi. Mwezi mwingine anajifanya mambo hayajaka vema anakapa hamsini kakawa kanasisitizia akajitambulishe kwao. Jaama akakaambia ngoja kwanza kapate kazi. Ikatangazwa kazi ya project moja jamaa akamwambia binti a apply, na cv na kila kitu akamwandalia, kampiga shule kabla ya interview kwenda maswali hayakuwa mbali binti kapata kazi kahamia Dar pesa ya kuanzia maisha jamaa akampa kama 1m akawambia angependa kumpa zaidi ila hali yake mbaya. Binti Dar akawa anakaa kwa mama mdogo alipoanza kula mshahara akaanza kubadilika, mawasiliano yakawa hafifu na akawa na majibu ya mkato kwa jamaa,
Vile nilishatambulishwa na nilikuwa mtu wa karibu nikaombwa niongee naye nijue shida nini. Basi nikakutana na binti anieleze, Duhh nilichoka, maana alinipa kavu kavu kwa jamaa anampenda ila maisha yake ya kuunga unga anahitaji mtu mwenye pesa isiyo ya mawazo. Eti jamaa kumnunulia hata IST hawezi!
Basi nikamwambia mshkaji hakuna mwanamke pale apige chini, akaniambia kuna vitu alishaviona awali ila alitaka kuona tabia yake akishashashika shika vijisenti ili apate udhibitisho.
Jamaa akampigia demu, nashukuru kwa yote, demu akamjibu good looks and being nice do not put nice food on the table and pay expensive school fees. Atafute tu atapata mwanamke wa saizi yake.
Kimsingi jamaa alikuwa ana connection kubwa na project ambapo binti alikuwa ameajiriwa, alikuwa na consulting firm ambapo alikuwa anawafanyia kazi kibao, demu alichoka alipobaini kuwa jamaa yupo vema sana tu na he is a good friend of her regional manager (Tanzania & Zambia) na kuwa kama si jamaa asingepata ile kazi. Sasa akarudi kwangu eti kwa nini sikumwambia ukweli! Kwamba firm inayovutaga mshiko mrefu tu ofisini kwao ni ya jamaa.
Akarudi kumwangukia jamaa eti ni utoto na alizinguliwa na maisha ya Dar jamaa ampe nafasi tena.
Mshkaji kagoma kata kata sasa kina sisi siku hizi demu tunamega kisela huku akiweka jitihada za kutafuta mchumba mwingine. Ila haachi kunilaumu
Duuuuuh!!! Kweli wanawake hawa!!! Na kama jamaa angempokea tu ingekula kwake!!