Kapata kazi kanitupa

Kapata kazi kanitupa

Nilipewa kazi ya kuongea na binti mmoja, ni hivi jamaa yangu mmojaa mbaye yupo vema sana up stairs na yupo ok vya kutosha financially alikuwa Mwanza kwa kazi ya kama 18mnths. Akakapenda kabinti flani ka St Augustine jamaa akaona ngoja akapime kama kanafaa kuwa wife. Jamaa akawa anakasaidia mambo kadha wa kadha ya kifedha ila hakujionesha yupo vizuri kiasi gani na ushauri wa kikasomo. Kalipomaliza chuo kakapiga mtaani mwaka na nusu bila kazi jamaa anakapa pocket money btn kati ya laki na laki tatu kila mwezi. Mwezi mwingine anajifanya mambo hayajaka vema anakapa hamsini kakawa kanasisitizia akajitambulishe kwao. Jaama akakaambia ngoja kwanza kapate kazi. Ikatangazwa kazi ya project moja jamaa akamwambia binti a apply, na cv na kila kitu akamwandalia, kampiga shule kabla ya interview kwenda maswali hayakuwa mbali binti kapata kazi kahamia Dar pesa ya kuanzia maisha jamaa akampa kama 1m akawambia angependa kumpa zaidi ila hali yake mbaya. Binti Dar akawa anakaa kwa mama mdogo alipoanza kula mshahara akaanza kubadilika, mawasiliano yakawa hafifu na akawa na majibu ya mkato kwa jamaa,

Vile nilishatambulishwa na nilikuwa mtu wa karibu nikaombwa niongee naye nijue shida nini. Basi nikakutana na binti anieleze, Duhh nilichoka, maana alinipa kavu kavu kwa jamaa anampenda ila maisha yake ya kuunga unga anahitaji mtu mwenye pesa isiyo ya mawazo. Eti jamaa kumnunulia hata IST hawezi!

Basi nikamwambia mshkaji hakuna mwanamke pale apige chini, akaniambia kuna vitu alishaviona awali ila alitaka kuona tabia yake akishashashika shika vijisenti ili apate udhibitisho.

Jamaa akampigia demu, nashukuru kwa yote, demu akamjibu good looks and being nice do not put nice food on the table and pay expensive school fees. Atafute tu atapata mwanamke wa saizi yake.

Kimsingi jamaa alikuwa ana connection kubwa na project ambapo binti alikuwa ameajiriwa, alikuwa na consulting firm ambapo alikuwa anawafanyia kazi kibao, demu alichoka alipobaini kuwa jamaa yupo vema sana tu na he is a good friend of her regional manager (Tanzania & Zambia) na kuwa kama si jamaa asingepata ile kazi. Sasa akarudi kwangu eti kwa nini sikumwambia ukweli! Kwamba firm inayovutaga mshiko mrefu tu ofisini kwao ni ya jamaa.

Akarudi kumwangukia jamaa eti ni utoto na alizinguliwa na maisha ya Dar jamaa ampe nafasi tena.

Mshkaji kagoma kata kata sasa kina sisi siku hizi demu tunamega kisela huku akiweka jitihada za kutafuta mchumba mwingine. Ila haachi kunilaumu

Duuuuuh!!! Kweli wanawake hawa!!! Na kama jamaa angempokea tu ingekula kwake!!
 
Toka nianze kusikia stori za tu kumsomesha mchumba,lazima jamaa atendwe yaani hii ni kama kanuni ya maisha ukiikiuka lazma ile kwako..

MCHUMBA HASOMESHWI
 
Fanya mpango mkuu umpe mimba iwe kumbukumbu kwako... maana hawa viumbe ni kinyonga.
 
Usijali kuoa utaoa mwingine

Huyo inabidi ukae chini uongee na Mungu kwamba maumivu aliyokupatia na hauna kosa lolote kwake basi yampate mara millioni moja na akukumbuke katika kila hatua yake maishani mwake.

Omba Mungu akupe nguvu na umsahau pia na umshukuru kuwa amekuepusha mabaya maishani mwako kwa kukuonyesha sasa hivi huyo mchumaji alivyo.

Hakufai kuwa mke songa mbele utapata uliyepangiwa ma Mungu.

Furahia haukumuweka ndani angekumaliza roho na kuumiza haswa.

Upo sahihi, alichokifanya huyo binti hata muumba wetu hawezi kukikubali na siku moja atamuonyesha kuwa alimkosea. Ila kumbuka LIKUEPUKALO LINA HERI NA WEWE.
 
mshukuru Mungu kwa yote pia jitahidi na umuombe Mungu akusahaulishe huyo mtu. Kilichomtokea huyo mchumba wako ni tamaa tu kwani huko alikoenda atakuwa amepata m/ume mwingine ambaye ana pesa zaidi yako amemdanganya nae bila kufikiria amemkubalia. Ipo sana hiyo kwenye maofisi akija dada mgeni aliye single wale ma-player wanamtokea na kumrubuni kabla hajausoma mchezo anapigwa bomba baadae anapigwa chini na akistuka atajilaumu sana.

Baadae atarudi kwako ila utaamua mwenyewe maana utakuwa ushajua tabia ya mama watoto wako mtarajiwa.

Kuna kanuni za kiume hapa ulizikiuka ambazo ni mbili
1. Kumwamini m/mke na kujitoa jumla as if ni mkeo wa ndoa
2. Kumsomesha mchumba

Hivyo viwili m/ume hutakiwi kuvifanya abadani utakuja kulia kilio kikubwa sana na kulaani wanawake wote wakati kosa niwewe kukiuka hivyo vitu viwili

Tafuta m/mke mwingine ila usimwamini 100% wala usimsomeshe maana ni jukumu la wazazi wake hilo
Hata mkeo pia kujiachia jumla ni tatizo.Wang nlimpenda sana na bahati nzuri nlikuwa vema kipesa,matokeo yake nkiend kutafuta pesa ye aenda short time nje ya ndoa.Kustuka, nambebeleza aache huo mchezo, akaenda mahakamani kutaka talaka.Hawaaminiki hawa.
 
Hata mkeo pia kujiachia jumla ni tatizo.Wang nlimpenda sana na bahati nzuri nlikuwa vema kipesa,matokeo yake nkiend kutafuta pesa ye aenda short time nje ya ndoa.Kustuka, nambebeleza aache huo mchezo, akaenda mahakamani kutaka talaka.Hawaaminiki hawa.

Pole sana wanawake mchawi wao ni mmoja
 
Hata mkeo pia kujiachia jumla ni tatizo.Wang nlimpenda sana na bahati nzuri nlikuwa vema kipesa,matokeo yake nkiend kutafuta pesa ye aenda short time nje ya ndoa.Kustuka, nambebeleza aache huo mchezo, akaenda mahakamani kutaka talaka.Hawaaminiki hawa.

duh pole sana haya mambo ni mabaya sana vp lakini amerudi? maana wanadanganywaga baadae akili zikiwarudi wanakuja wanatembelea magoti
 
Tumia unguli wako umuondoe kazini kama umemuweka kumtoa simple
 
JFimenipa ujasir na ukatil fulan,m/mke hatakiw akuelew umeumia kias gn,keep on your own bro,pray hard,4gv&4get her(amen)
 
Pole sana, kwa uzoefu wangu, tuliza akili, iko siku. Hao pimbi wa aina hiyo tumeona wengi sana wanagonga mwamba.

Kweli mkuu... Akisha gonga mwamba atajileta na wakati huo wewe atakua below your standards.....
 
Hivi vilio tutazid kuvisikia sana kwa sababu watu hamuelewi MCHUMBA HASOMESHWI.
 
Huyo demu ni shenzi type sana.Ebu nipe no yake nimshauri akurudie.
 
Pole sana zungumza naye ujue tatizo nini kwanini amebadilika

Huyu dada hajabadilika, ila amekuwa "original". Ule Unyenyekevu ulikuwepo kwa sababu ya kutokuwa na kipato tu. She is showing her true colors
 
Back
Top Bottom