Kapata kazi kanitupa

Kapata kazi kanitupa

Mkuu LUBEDE, kwanza kabisa pole kwa yaliyokukuta. Kwa kweli yakupasa umshukuru Mungu kwa kukufunulia na kukuonyesha tabia za huyo mwanamke ambaye wewe ulidhani ndio chaguo sahihi katika maisha yako.

Kuna msemo wa zungu unaosema "There are two things which defines a person. His/her patience when he has nothing and his/her attitude when he/she has everything." Kama hiyo kazi imemfanya huyo mwanamke akuone huna thamani kwake basi ujue huyo hakufai. Tabia ya wanawake kama hao ni ya wale ambao wanatanguliza fedha, mali na anasa za huu ulimwengu mbele kuliko utu. Kwa kweli badala ya kulalamika yakupasa umshukuru Mungu kwa kukuonyesha tabia ya huyo mwanamke before its too late maana huwezi jua, pengine huko mbeleni angeweza kukufanyia mamb makubwa na ya kukuumiza zaidi ya hili.

Mimi nakushauri mkuu usikate tamaa na badala yake usali na umuombe Mungu akujalie akujalie mke mwema ambaye alikuandalia tangu kuumbwa kwako.

Well said mkuu,nashukuru kwa kunipa moyo kwa niaba ya wote walionitakia nguvu na ujasiri wa kufanya nione kawaida,game yake ilikuwa ngumu katika familia yao,nikaona sababu atakuwa mwenzi wa maisha na mama wa mbeleni wa wanangu na nguvu ya kumtengeneza kielimu ninayo(pesa)nikaona kiroho safi sio mbaya nim'shape ili asiwe mzigo,na mwisho kaamua kuwa punda na kunilipa mateke,haina shida,lengo la kuandika hapa ni kuwapa alert wahangaikaji wenzangu kuwa haya mambo wengi tunayasikia tu na kuhisi kama ni stori za kumchekesha mfalme,haya mambo ni real wakuu,wanawake hawaaminiki,yaani nimeamini kweli "CURIOSITY KILLED THE CAT"
 
Last edited by a moderator:
ngoja Kwanzaa...kakutana na wajanja mjini wacha wachezee ngozi ichuje ndio atarudi kwako kiongozi shukuru ulipiga mzigo fresh na kama ulibahatika kupata na hii kitu 0713 shukuru yaishe tafuta mwingine
 
asomeshe mara ngapi na kamaliza na kazi kapata

Sikurogwa wakuu,nilihisi mimi ni kijana makini na mwenye uelewa nisiyehitaji ubabaishaji kwenye hilo,kumbe hamna kitu,nimejikuta nabakia kuwa kibarua ambaye sikuuelewa mtego wa fundi..
 
Nampongeza huyo binti! Ukimsomesha mtu asiye ndugu yako unatakiwa kujua kuwa ni kama umetoa sadaka na usitegemee malipo au kitu fulani!

Pengine kuna ndugu zako waliitaji huo msaaada ulishindwa kuwasaidia lakini ukamsaidia aliyedhani ni muhimu sana na atathamini mchango wako!

Nafikiri umevuna ulicho panda na hayo ndio mavuno na ni funzo kwako..! Nampongeza huyo binti..
 
Sikurogwa wakuu,nilihisi mimi ni kijana makini na mwenye uelewa nisiyehitaji ubabaishaji kwenye hilo,kumbe hamna kitu,nimejikuta nabakia kuwa kibarua ambaye sikuuelewa mtego wa fundi..

pole sana kijana mwenzangu njoo kwangu upate pumziko la nafsi i dont need yo pesa wala vitu i only need yo love
 
Ama kweli "NO LIFE WITHOUT A WIFE, BUT A WIFE CAN BE A KNIFE TO CUT OFF YOUR LIFE" huyu mwanamke pamoja na kusimamia show zote tangu high school, chuo na kurudi mtaani hana muelekeo, nikatumia unguli wangu mjini kapata kazi T.R.A.

Nikaona ni wakati muafaka home wamjue mambo mengine ya kuwa pamoja milele yaendelee,wakamtambua na sifa tele kuwa najua kuchagua,mwisho wa siku hata posa hatujapeleka anasema alikurupuka nimuache, afanye kwanza kazi, anahisi kuwa single ni vizuri zaidi kwake, atanifikiria baada ya miaka miwili.

Sitaki tena kuoa?

Pole sana brothr bt amin ipo siku atakuja analia
 
Usijali kuoa utaoa mwingine

Huyo inabidi ukae chini uongee na Mungu kwamba maumivu aliyokupatia na hauna kosa lolote kwake basi yampate mara millioni moja na akukumbuke katika kila hatua yake maishani mwake.

Omba Mungu akupe nguvu na umsahau pia na umshukuru kuwa amekuepusha mabaya maishani mwako kwa kukuonyesha sasa hivi huyo mchumaji alivyo.

Hakufai kuwa mke songa mbele utapata uliyepangiwa ma Mungu.

Furahia haukumuweka ndani angekumaliza roho na kuumiza haswa.
 
Well said mkuu,nashukuru kwa kunipa moyo kwa niaba ya wote walionitakia nguvu na ujasiri wa kufanya nione kawaida,game yake ilikuwa ngumu katika familia yao,nikaona sababu atakuwa mwenzi wa maisha na mama wa mbeleni wa wanangu na nguvu ya kumtengeneza kielimu ninayo(pesa)nikaona kiroho safi sio mbaya nim'shape ili asiwe mzigo,na mwisho kaamua kuwa punda na kunilipa mateke,haina shida,lengo la kuandika hapa ni kuwapa alert wahangaikaji wenzangu kuwa haya mambo wengi tunayasikia tu na kuhisi kama ni stori za kumchekesha mfalme,haya mambo ni real wakuu,wanawake hawaaminiki,yaani nimeamini kweli "CURIOSITY KILLED THE CAT"

Ungemtia mimba mapema
kama watoto wawili tu akilu ingemkaa sawa
 
Sometimes maamuz magum yanahitajika temana naye atakuumiza kichwa chako
 
​Ni kwel mchumba hasomeshwi lakini ni zaidi kuwa katika macho yakibinadamu utasema ni mbaya sana ila katika mach yakiroho ni vyema maana ambayo yangekuja ni makubwa zaidi...
 
mshukuru Mungu kwa yote pia jitahidi na umuombe Mungu akusahaulishe huyo mtu. Kilichomtokea huyo mchumba wako ni tamaa tu kwani huko alikoenda atakuwa amepata m/ume mwingine ambaye ana pesa zaidi yako amemdanganya nae bila kufikiria amemkubalia. Ipo sana hiyo kwenye maofisi akija dada mgeni aliye single wale ma-player wanamtokea na kumrubuni kabla hajausoma mchezo anapigwa bomba baadae anapigwa chini na akistuka atajilaumu sana.

Baadae atarudi kwako ila utaamua mwenyewe maana utakuwa ushajua tabia ya mama watoto wako mtarajiwa.

Kuna kanuni za kiume hapa ulizikiuka ambazo ni mbili
1. Kumwamini m/mke na kujitoa jumla as if ni mkeo wa ndoa
2. Kumsomesha mchumba

Hivyo viwili m/ume hutakiwi kuvifanya abadani utakuja kulia kilio kikubwa sana na kulaani wanawake wote wakati kosa niwewe kukiuka hivyo vitu viwili

Tafuta m/mke mwingine ila usimwamini 100% wala usimsomeshe maana ni jukumu la wazazi wake hilo
 
tatizo wadada wengi hawana utu.... wanapenda kujiangalia kwanza wao kabla ya uhusiano uliopo.... Pole mkuu, wewe achana nae, endelea na maisha yako, maana kuna msemo wasema "katika mauhusiano, unaweza ukamfanya mpenzi wako mke/mume bora kwa mwanaume/mwanamke mwengine"... ume play part yako... so u have to move on... usijeshika makali kwa sasa, wakat mpini unakuja, we vumilia
 
Back
Top Bottom