Kanuni mpya za TFF ni za ovyo kupindukia; wanaendesha mpira kishamba sana!

tpaul

JF-Expert Member
Feb 3, 2008
21,838
18,250
Kwa mujibu wa kanuni mpya za TFF, wachezaji binafsi hawapaswi kuwa na mdhamini ambaye ni mpinzani kibiashara wa mdhamini mkuu wa ligi kuu (NBC). Hili ni jambo la ajabu sana. Kwanini kanuni hii ya ajabu imepitishwa? Nionavyo mimi kanuni hii inalenga kuwarudisha nyuma wachezaji kiuchumi na kuwafanya waishi maisha ya njaa kama ilivyokuwa zamani.

Hii kanuni inawabana wachezaji tu, huku ikiwa haigusi timu shiriki. Kwa mfano Yanga na Simba wanadhaminiwa na benki ya NMB lakini hawajaguswa. Pia Simba wanadhaminiwa na kampuni ya m-bet na pia kuna baadhi ya timu zinadhaminiwa na sportpesa. Na hawa ni wapinzani wa kibiashara. Mbona wao hawawekewi mizengwe?

Pia huko Ulaya, kwa mfano, utakuta Real Madrid inadhaminiwa na Adidas lakini Ronaldo alikuwa anadhaminiwa na Nike na alikuwa akivaa njumu za Nike bila shida. Na pia benki ya Barclays wanadhamini ligi kuu ya Uingereza lakini wachezaji wa Liverpool wanavaa jezi zimeandikwa Standard Chartered bila tatizo.

Hawa ndio wanajua umuhimu wa udhamini kwenye ligi sio hawa TFF wanajifungia kwenye kiota kimoja na NBC na kusahau kuwa huko Ulaya wachezaji wanapiga mpunga wa kutosha kwa kudhaminiwa na wadhamini wengine mbali na mdhamini anayedhamini ligi zao.

Na kibaya zaidi, wachezaji wa ligi kuu hawaruhusiwi sio tu kuvaa jezi au njumu zenye nembo au jina la mpinzani wa NBC tu, bali hata kujihusisha kwenye matangazo (na haya hayana athari kiwanjani). Kwa mfano, mchezaji Clatus Chama anashiriki matangazo ya CRDB na kupiga mpunga mnene. Na pia mchezaji Mwamnyeto anashiriki matangazo ya NMB yanayompa mpunga mnene. Haya yote yatapaswa kukoma mara moja kwa mujibu wa kanuni mpya za TFF.

TFF kama wameshindwa kusimamia maslahi ya wachezaji ni bora TFF ibinafsishwe kwa mwekezaji kutoka nje atakayekuwa anajali maslahi ya wachezaji. Napendekeza wakati tunawauzia waarabu bandari, tuwauzie pia TFF waiendeshe.

Nawasilisha.
 
Na wewe ni mtu wa ovyo pia!
Huyo mtu wa nje utakayembinafsishia TFF una uhakika gani kuwa atakuwa analinda maslahi ya wachezaji...!?

Hiyo trust experience umeitoa wapi!? Au na wewe umewahi kujibinafsisha kwake na ukapata mslahi ambayo unataka wachezaji wetu wapate!??

Hoja yako ni strong ila wewe uliyejivika kilemba cha utetezi ni MBUMBUMBU!!!
 
tatizo sio TFF, hivi vilabu viliunda bodi ya ligi Ili kusimamia maslahi Yao lakini kwa ujinga wa viongozi wao imewaachia mamlaka yote TFF.

kutokana na uundwaji wa bodi ya ligi ni kuajili watendaji wake kitu ambacho hawafanyi badala yake TFF ndio inaajili hao watendaji ila mishahara inalipwa na bodi ya ligi.

Kuingia mikataba na wadhamini na TFF kupata asimia 10 ya mapato ya mkataba lakini TFF imekuwa ikiingia mikataba ya udhamini na kuchukua asilimia 20 ya mapato.

TFF ndio inapanga kanuni za ligi na kuchukua mapato mengi ya ligi kama malipo ya wachezaji wa kigeni.
 
Na wewe ni mtu wa ovyo pia!
Huyo mtu wa nje utakayembinafsishia TFF una uhakika gani kuwa atakuwa analinda maslahi ya wachezaji...!?

Hiyo trust experience umeitoa wapi!? Au na wewe umewahi kujibinafsisha kwake na ukapata mslahi ambayo unataka wachezaji wetu wapate!??

Hoja yako ni strong ila wewe uliyejivika kilemba cha utetezi ni MBUMBUMBU!!!
Kivipi mkuu? Wewe unaona TFF wanaendesha mpira kwa kutumia akili? Je, ukipewa TFF nawe utaiendesha ovyo kama hivi? Acha kutetea ujinga mkuu.
 
Sasa mkuu TFF ifanyeje? Hayo ni masharti ya mdhamini, wenzetu ulaya walishajibrand kupata wadhamini sio shida kama huku kwetu hivo lazima Tff imnyenyekee mdhamini, japo sio fair ila hamna namna, wachezaji watafute wadhamini wengine tuu nje ya mabenk
 
Kivipi mkuu? Wewe unaona TFF wanaendesha mpira kwa kutumia akili? Je, ukipewa TFF nawe utaiendesha ovyo kkama hivi? Acheni kutetea ujinga mkuu.
Tatizo wewe ulipaswa kusema nini inapaswa kuwa suluhisho na sio kulalamika!

Suluhisho ulilolileta liko biased kwasababu ubinafsishaji haujawahi kileta faida kwenye nchi hii..!! Najua unalifahamu hilo hakuna haja ya kutoa mifano!

Toka nje ya box uwe sehemu ya maendeleo ya michezo ndani ya nchi hii!
Ebu fikiria muda wote uliopoteza kwenye keyboard ya simu au laptop yako kutengeneza wazo zuri, halafu wazo lako lingefanyiwa kazi na TFF ungejiona ni mtu wa maana kiasi gani katika jamii ya mpira TANZANIA.
Ondoa akili yako katika ubinafsishaji katika nchi hii, SISI WENYEWE INCLUDING ME AND YOU TUNAWEZA TUKIWAJIBIKA IPASAVYO NA KUONDOA ULASIMU, HAO WAZUNGU HAWANA TOFAUTI YOYOTE NA WEWE.
 
Nimetoa mifano halisi jinsi mpira unavyoendeshwa huko Ulaya na nimetoa suluhisho la kuibinafsisha TFF bado hunielewi unataka mm nifanye nini mkuu?
Tatizo wewe ulipaswa kusema nini inapaswa kuwa suluhisho na sio kulalamika!

Suluhisho ulilolileta liko biased kwasababu ubinafsishaji haujawahi kileta faida kwenye nchi hii..!! Najua unalifahamu hilo hakuna haja ya kutoa mifano!

Toka nje ya box uwe sehemu ya maendeleo ya michezo ndani ya nchi hii!
Ebu fikiria muda wote uliopoteza kwenye keyboard ya simu au laptop yako kutengeneza wazo zuri, halafu wazo lako lingefanyiwa kazi na TFF ungejiona ni mtu wa maana kiasi gani katika jamii ya mpira TANZANIA.
Ondoa akili yako katika ubinafsishaji katika nchi hii, SISI WENYEWE INCLUDING ME AND YOU TUNAWEZA TUKIWAJIBIKA IPASAVYO NA KUONDOA ULASIMU, HAO WAZUNGU HAWANA TOFAUTI YOYOTE NA WEWE.
 
Ni wkt sasa wachezaji binafsi kusimama kama taasisi hususani katika kuwa na agencies na wanasheria wakueleweka wkt wa kuingia mikataba na ivo vilabu..

Vilabu sivilaumu sna kwa kuwa na vyenyewe vinatgemea zaidi pesa iyo iyo ya mdhamini katika kujiendesha so ni lazima kwenye kanuni kama izo vitajipndelea tu vyenyewe!
 
Kwamba eti hata kama mchezaji atapata dili zake binafsi na Benki nyingine basi hawaruhusiwi kutangaza kwa sababu ya mkataba wa NBCTanzania na Ligi huku atakayekiuka akikabiliwa na kufungiwa kwa kipindi cha kati ya mwezi mmoja na mitatu? Huu ni uzwazwa, kama vipi wachezaji wagome tu!
 
ni wkt sasa wachezaji binafsi kusimama kama taasisi hususani katika kuwa na agencies na wanasheria wakueleweka wkt wa kuingia mikataba na ivo vilabu..

vilabu sivilaumu sna kwa kuwa na vyenyewe vinatgemea zaidi pesa iyo iyo ya mdhamini katika kujiendesha so ni lazima kwenye kanuni kama izo vitajipndelea tu vyenyewe!
Kweli kabisa mkuu. Ndio maana nimesema katika sakata hili TFF na vilabu wamejipendelea wenyewe pasipo kuangalia maslahi ya mchezaji. Huko Ulaya wachezaji wanavuna pesa nyingi sana kutoka kwenye matangazo. Lakini huku Tanzania eti TFF wanazuia. Wanataka wachezaji wakaibe? Wapuuzi sana hawa jamaa. Hawafai kabisa.
 
Kwamba eti hata kama mchezaji atapata dili zake binafsi na Benki nyingine basi hawaruhusiwi kutangaza kwa sababu ya mkataba wa NBCTanzania na Ligi huku atakayekiuka akikabiliwa na kufungiwa kwa kipindi cha kati ya mwezi mmoja na mitatu? Huu ni uzwazwa, kama vipi wachezaji wagome tu!
Huu ni upumbavu wa kiwango cha lami mkuu. TFF ni zaidi ya matutusa.
 
Kwa mujibu wa kanuni mpya za TFF, wachezaji binafsi hawapaswi kuwa na mdhamini ambaye ni mpinzani kibiashara wa mdhamini mkuu wa ligi kuu (NBC). Hili ni jambo la ajabu sana. Kwanini kanuni hii ya ajabu imepitishwa? Nionavyo mimi kanuni hii inalenga kuwarudisha nyuma wachezaji kiuchumi na kuwafanya waishi maisha ya njaa kama ilivyokuwa zamani.


Nawasilisha.
HIZO KANUNI ZIMEPITISHWA NA TFF PEKE YAKE AU KWA KUSHIRIKIANA NA VIONGOZI WAWAKILISHI WA TIMU ZOTE ZINAZOSHIRIKI LIGI KUU?
 
Hili lazima liwatoe busha. Hawawezi kukanyaga haki za wachezaji wakaachwa salama.

Na pia nashangaa kwanini kamati inayosimamia hadhi za wachezaji inakaa kimya wakati wachezaji wanadhalilishwa kiuchumi.
Seriously?
 
Hili lazima liwatoe busha. Hawawezi kukanyaga haki za wachezaji wakaachwa salama.

Na pia nashangaa kwanini kamati inayosimamia hadhi za wachezaji inakaa kimya wakati wachezaji wanadhalilishwa kiuchumi.
Najiuliza why hizo kanuni zinapitishwa kienyeji bila wawakilishi wa vilabu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom