Kanjanja

Perry

JF-Expert Member
Feb 24, 2011
10,043
2,000
Heshma mbele wakubwa!naomba mnisaidie kunipa maana ya neno 'kANJANJA'
 
Heshma mbele wakubwa!naomba mnisaidie kunipa maana ya neno 'kANJANJA'

Kwa ninavyojua mimi neno "kanjaja" ni msimu (slang?) ulioibuka wakati wa serikali ya awamu ya 3. Neno hili lilitumiwa na Rais Mkapa kuwabeza/tukana waandishi wa habari. Kwa kutumia neno "kanjanja" alimaanisha mwandishi alisiyepikwa vema i.e asiyemahiri kwenye taaluma yake-mbabaishaji, "msanii". Hapa lilitokana na waandishi wa habari waliokuwa wanaandika habari tu bila kujielimisha kuhusu mada husika na hivyo wanajikuta wanaandika taarifa zisizo sahihi ambazo hazijafanyiwa utafiti wa kutosha aghalabu kwa sababu mwandishi hajui taaluma yake vizuri. Hakuna umakini. Basi akawaita waandishi wa Tz makanjanja. Ni kama neno "kihiyo" lilivyoibuka.
Kanjanja=mtaaluma feki, msanii, "incompetent".
 
Back
Top Bottom