Kanisa la TAG Kaskazini Pemba lachomwa moto

Yesu ni kivipi aseme kwenye KOLANI ILIYO ANDIKWA MIAKA MIA SITA NA USHEHE BAADA YAKE!!!, HIVI HUWA MNATUMIA AKILI NYIE MAISLAM?
.... na wanasema wale waliokufuru (wakristo) " Wewe si Mtume" Sema: Mwenyezi Mungu anatosha kuwa shahidi baina yangu na baina yenu na pia yule mwenye ilm ya Kitabu (Tourat, Injil na Zaburi)
 
Lete ushaidi wa maneno in red? It is very very imperative in your next reply you farward same. What you wrote is very sensitive religious accusation.


Mchungaji wa Kanisa la Full Salvation, Christopher Mtikilla ‘ameifungukia’ kauli ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete kuwa, baadhi ya viongozi wa dini nchini wanajihusisha na biashara haramu ya madawa ya kulevya, Ijumaa Wikienda linashuka naye.

Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu Ijumaa iliyopita, Mtikilla alisema tamko la JK ni la kweli kwa vile wapo baadhi ya viongozi wa dini wasiofuata maadili ya kazi yao na kufanya biashara hiyo. Akaongeza kuwa, yeye anamjua mmoja (jina tunalo).

“Rais alisema kweli, wala wasipinge. Kama kuna kiongozi yeye hafanyi biashara hii, ajue kuna wenzake wanafanya,” alisema kwa kujiamini Mtikilla.

Aidha, Mtikilla ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha DP, alimtaja mchungaji mmoja wa kanisa la kiroho la jijini Dar es Salaam ambaye ana waumini wengi kuwa, na yeye anafanya biashara hiyo na watu wengi wanajua.

“Mfano…(akamtaja jina) yule ni mfanyabiashara wa haya madawa, nani asiyejua bwana. Huyu na wenzake wengi ndiyo siri nzito ya kuwa matajiri wakubwa kwa sababu ya fedha haramu.”
Pia, alisema kuwa, mchungaji huyo alidakwa na madawa miaka ya karibuni, baadhi ya viongozi hao wa dini walisikia, lakini akahoji, “ni kwa nini hawakutoa tamko?”
Mchungaji Mtikilla aliongeza kuwa, haoni sababu ya viongozi wa Baraza la Maaskofu Tanzania kumkomalia JK kuweka hadharani majina ya viongozi wa dini wanaojihusisha na madawa ya kulevya.

Akahoji: “Mbona kuna maovu mengi yanayofanywa na viongozi wa dini ikiwemo ubakaji, ulawiti, utapeli na ushirikina lakini baraza halitoi tamko lolote?

“Kila mmoja ana mapungufu yake, serikali kuna mahali inakosea kwa sababu suala hili siyo la kulizungumzia kwenye majukwaa bali kama wapo wanaotuhumiwa, wakamatwe na uchunguzi wa kina ufanyike ili sheria ichukue mkondo wake.
“Pia viongozi wa dini wanakosea sana kutoa tamko dhidi ya rais. Hakuna sehemu ambapo maandiko matakatifu yanawataka kutumia jazba kukabili changamoto wanazokutana nazo.
“Kama kiongozi hafanyi haya, ajue kuna wenzake wanajihusisha na michezo isiyofaa, ikiwemo hili la biashara ya madawa ya kulevya. Tuache kuteteana na kujificha nyuma ya mwavuli wa dini. Siku hizi wengi hawaaminiki, wanajali fedha kuliko huduma ya kuchunga kondoo wa Bwana,” alisema Mtikila.

Wiki mbili zilizopita, katika hafla ya kumsimika Askofu John Ndimbo wa Kanisa Katoliki, Mbinga, Ruvuma, Rais Jakaya Kikwete alisema kuna baadhi ya wachungaji wanaojishughulisha na biashara ya madawa ya kulevya.
Alisema watumishi hao wa Mungu wamekuwa wakitumia nafasi zao kwenye paspoti kuingiza au kutoa madawa ya kulevya.

Ndipo maaskofu wanaounda Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) walipokutana Juni Mosi, mwaka huu mjini Dodoma chini ya Mwenyekiti, Mchungaji Peter Kitula na kumpa saa 48 Rais Jakaya Kikwete kuwataja kwa majina viongozi aliodai wanafanya biashara hiyo haramu.

Viongozi wengine wa dini wanaounda jumuiya hiyo ni Askofu Valentino Mokiwa (Anglikana, pia ni Kaimu Mwenyekiti), Alex Malasusa (KKKT) na Moses Kulola (EAGT).
Wengine ni maaskofu kutoka makanisa ya Moravian, African Inland, Baptist Tanzania, African Brotherhood, Church of God na Kanisa la Biblia.
Makanisa mengine yaliyopo kwenye Jumuiya hiyo ni Mbalizi Evangelist, Mennonite, Presbyterian, Salvation Army na Tanzania Yearly Meeting.
Miaka ya karibuni, kumekuwa na baadhi ya wachungaji wa kiroho wanaolalamikiwa na baadhi ya waumini wao kwa kuwa na utajiri mkubwa.

Waumini hao wamekuwa wakiwatuhumu wachunga kondoo wao kuwa, wanamiliki mamilioni ya fedha, magari ya kifahari, nyumba za kisasa huku wao, wakiwa kama kondoo, wanaishi maisha ya ufukara wa kutupwa.

Hata hivyo, uchunguzi wa kina wa gazeti hili umebaini kuwa, baadhi ya wachungaji nchini, wanashindana kumiliki magari ya bei mbaya huku baadhi ya kondoo wao wakishindwa kulipia kodi ya chumba cha shilingi elfu thelathini (30,000/=) kwa mwezi.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom