Kanisa la Rumi (Roman Catholic) Lilianzisha Uislam ili kuendelelea kuitawala na kuihadaa Dunia

JINA LA DINI

K
itu cha kwanza kabisa ambacho mtu anapaswa kukijua na kukifahamu kwa kina kuhusu Uislamu ni juu ya maana ya neno lenyewe Uislamu. Neno hilo ni la asili ya Kiarabu lenye maana ya kutii au kusalimisha matakwa ya mtu kwa Mwenyezi Mungu wa kweli wa pekee, ajulikanaye kwa Kiarabu kama Allah. Mtu ambaye amesalimisha matakwa yake kwa Mwenyezi Mungu (Allah) huuitwa Mwislamu. Dini ya Kiislamu haikupewa jina kutokana na jina mtu au watu, wala halikuamuliwa na kizazi chochote cha wanadamu kama vile Ukristo ambao ulipewa jina kutokana na Yesu Kristo, Ubudha unatokana na jina la Gautama Buddha, Kunfushian, unatokana na Confucius, Umaksi ulipewa jina la Karl Marx; Uyahudi unatokana na jina la kabila la Yuda na Ubaniani (Uhindu) unatokana na jina la Hindu. Uislamu (kutii amri za Mwenyezi Mungu) ni dini aliyopewa Adam, mtu wa kwanza na mtume wa kwanza wa Mwenyezi Mungu, na Uislamu ndio dini ya mitume wote waliotumwa na Mwenyezi Mungu kwa wanadamu. Kwa kuongezea, jina la Uislamu lilichaguliwa na Mwenyezi Mungu mwenyewe na limetajwa wazi wazi katika kitabu cha mwisho cha Allah (Quran). Allah alimfunulia mwanadamu katika kitabu cha mwisho alichomfunulia Mwanadamu. Katika ufunuo wa mwisho, uitwao kwa Kiarabu Al-Quran Allah ameeleza yafuatayo:-

Leo Nimekukamilishieni Dini yenu, na kukutimizieni neema Yangu, na Nimekupendeleeni Uislamu uwe Dini yenu [Quran 5:3]

Na anayetaka dini isiyokuwa ya Kiislamu basi haitakubaliwa kwake… [Quran 3:83]

Kwa hiyo, Uislamu haudai kuwa ni dini mpya iliyoletwa Arabuni na Mtume Muhammad katika karne ya saba, lakini Uislamu ni mwendelezo wa sehemu ya mwisho ya dini ya Allah, kama ilivyofunuliwa toka mwanzo kwa Adam na mitume waliomfuatia.

Hadi kufikia hapa tutatoa maoni kwa ufupi kuhusu dini nyingine mbili zinazodai kwamba ndizo njia sahihi. Hakuna sehemu yoyote katika Biblia ambayo utakuta kwamba Mwenyezi Mungu amewafunulia watu wa Mtume Musa au vizazi vyao kwamba dini yao inaitwa Uyahudi, au kwa wafuasi wa Kristo kuwa dini yao inaitwa Ukristo. Kwa maneno mengine, majina Uyahudi" na "Ukristo hayakutokana na asili ya Mwenyezi Mungu wala hayani idhini yake. Jina Ukristo halikuwepo hadi muda mrefu baada ya kuondoka Yesu ndipo jina hilo lilipotolewa kwa dini ya Yesu.

Sasa nini lililokuwa jina la kweli hasa, la dini ya Yesu, ambalo linajipambanua na jina lake? (Majina yote mawili Yesu na Kristo yanatokana na maneno ya Kiebrania, kupitia Kigiriki na Kilatini. Jesus ni Kingereza na kwa Kilatini cha Kigiriki ni Iesous, ambalo kwa Kiebrania ni Yeshua au Yehoshua' (Joshua). Neno la Kigiriki Christos ni tafsiri ya Kiebrania kwa neno Messiah, jina la heshima linalomaanisha Mpakwa mafuta.” Dini yake inaakisi mafundisho yake, ambayo aliwaamrisha wafuasi wake kuyakubali kama misingi ya kuwaongoza katika uhusiano wao na Mwenyezi Mungu. Katika Uislamu, Yesu ni mtume aliyeletwa na Allah na jina lake la Kiarabu ni Issa. Kama ilivyo kwa mitume ya kabla yake, yeye naye aliwalingania watu wasalimishe matakwa yao kwa matakwa ya Mwenyezi Mungu (jambo ambalo ndilo linalosimamiwa na Uislamu). Kwa mfano katika Agano Jipya inasemekana kwamba Yesu aliwafundisha wafuasi wake kusali kwa Mwenyezi Mungu kama ifuatavyo:-

Baba [yetu uliye mbinguni], Jina lako litakaswe, Ufalme wako uje, [Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.] (Luka 11:2/Mathayo 6:9).

Wazo hili lilisisitizwa sana na Yesu katika maelezo yake mengi yaliyoandikwa katika Biblia. Kwa mfano, amefundisha kuwa, waliojisalimisha kwa Mwenyezi Mungu, hao peke yao ndio watakaopata uzima wa milele. (Peponi).

Yesu pia alifafanua kwamba yeye mwenyewe amejisalimisha kwa matakwa ya Mwenyezi Mungu.

Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.” (Mathayo 7:21).

Mimi siwezi kufanya neno mwenyewe; kama nisikiavyo ndivyo nihukumuvyo; na hukumu yangu ni ya haki, kwa sababu siyatafuti mapenzi yangu mimi, bali mapenzi yake aliyenipeleka. (Yohana 5:30).

Kuna maelezo mengi katika Biblia yanayoonesha kwamba Yesu aliweka wazi kwa wafuasi wake kwamba yeye siye Mungu.

Kwa mfano, aliposema kuhusu saa ya mwisho alisema:

Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba. (Marko 13:-32).

Kwa hiyo, Yesu kama walivyokuwa Mitume waliopita kabla yake na yule aliyekuja baada yake, alifundisha dini ya Kiislamu: kujisalimisha kwa matakwa ya Mwenyezi Mungu mmoja aliye wa kweli.
YESU hakuleta dini bali upatanisho kati ya mwanadam na Mungu. Yeye ni njia ya uzima, na yoyote amwaminie ataokoka au atauona ufalme wa mbinguni
 
Kaeleza yale ambayo kuna mtu mmoja huwa anadai alikuwa jesuit akaasi, na ndipo akatoa siri za vatcan. Miongoni mwa siri hizo ni ya uislamu kuanzishwa na Vatcan. Unaweza pita hapa kuangalia zaidi.

Wengi hawataki kuijua kweli wapo usingizini
 
How Is the World Diverted and Controlled!
(Waliopewa upeo mkubwa saana kujua mambo kuzidi wengine wamesababisha haya yote )

miaka si mingi iliyopita hapa Tanzania ilisikika kuwa mtoto mwenye akili nyingi katika jumuiya zenye wakatolic na akawa ni mkatolic kulikuwa na mpango wa kumchukua huyu na kumwendeleza kielimu kwenye shule za Mission kwa ajili ya matazamio tegemeo.
Siku hizi sisikii sana sijui wame-adopt mhinu gani tena!!
Ni mengi sana kuhusu wa Roman Catholic Mimi nimetokea huko na nimejua kweli naamini mengi tutayajua
 
hii ni kwa mujibu wa akili zako ambazo bila shaka ni katika wake watanzania wanne wawili vichaa basi we mmoja wapo

qumor weee
Mjadala unahusu dini mnaotukana sijui ni waumini wa dini hzo au la maana katika hzo hakuna inayofundisha kutukana
 
coz ni mada ya kipuuzi aliyepost hana elimu yeyote ya tahlil(mambo ya kale na historia)

kama angekua anajua hicho kitu angejua na ukristo ulivyo anzishwa na paulo na yesu alikua dini gani

mi ndomaana nawatukana coz ni wajinga

unajua usianze ku jaji dini ya mwenzio wakati we yako huiju
 
Mkuu naomba tumia kichwa chako kujifunza utaelewa nini kinaendelea lakini kama ni mvivu wa kufikiri daima hutofahamu chochote
Tatizo zile lesson za kwenye makambi ya Kisabato zinazamisha ..

BTW: ulichoandika ni porojo na stori za vijiwe vya kahawa...
 
Sio kosa lako kwa kuwa Uislamu wenyewe huujui. Mada yako haieleweki pia.
Mkuu Quran imeandikwa kwa msaada wa Rumi (Jesuit ) kutoka na na mkusanyiko wa vifungu ktk Torati na baadhi yalinukuliwa ktk uhalisia wa Dunia Kwa faida ya Kanisa la Rumi (RC)
 
Mkuu utaelewa na itakuingia taratibu haitaki haraka
Hivi unafikiri ulichoandika kwa mtu mwenye akili timamu ataelewa....

Watu watakao support huu ujinga ulioandika hapa wote wanaakili fupi...Ni kwa kiasi kikubwa ni Wasabato.....
 
Back
Top Bottom