Kanali Muammar Gaddafi (1942 - 2011)

Kanali Muammar Gaddafi (1942 - 2011)

Kuwa na akili wewe ulichoweza kupambazua wewe ni uchochezi tu hapo? Na kuhusu hii nchi wewe unaiona ipo kwenye nuru hii au kwa kuwa wewe unashiba na kwenda kunya kila siku? Ficha upumbavu kama hujui kitu unakaa kimya. I wonder nina argue na mtoto mdogo au jitu hopeless. **** you!
nashukuru kwa matusi yako
sawa basi tz hakuna nuru naomba unieleweshe mie ni kweli pengine uko sahihi ni hopeless TUMO KATIKA GIZA GANI UNIAMBIE?FUNGUKA KIJANA
 
KANALI MUAMMAR GADDAFI (1942 - 2011)





SEHEMU YA TATU



Katika sehemu iliyopita nilieleza namna ambavyo vugu vugu la maandamano jinsi lilivyoibuka na kukolea katikati mwa mwezi February mwaka 2011.


Katika sehemu hii ya tatu nakusudia kuandika zaidi kuhusu namna ambavyo vikundi vya waasi viliibuka na hatimaye kumuondoa Gaddafi madarakani.


Tuendelee…

Baada ya vugu vugu kupamba moto hasa na maandamano kukolea karibia nchi nzima ya Libya, na hatimaye kundi kubwa la polisi na wanajeshi kuasi, taratibu ikaanza vugu vugu la kupinga Gaddafi kwa kutumia silaha badala ya maandamano pekee.


Mwanzoni kabisa mwa vugu vugu hili la kutumia silaha, vikundi vya wapiganaji vilikuwa vinaundwa na raia wa kawaida waliojitolea kushika mtutu.
'Volunteers' hawa waliojitolea kupigana walikuwa wengi wao wanatoka kada za ualimu, wanafunzi, na wafanyakazi katika visima vya mafuta.
Taratibu wanajeshi na polisi wakaanza kujiunga nao na kukoleza moto wa kumoinga Gaddafi kwa mtutu wa bunduki.


Mpango huu (kumpinga Gaddafi kwa silaha) ulikuwa ni mtego mujarabu kabisa wa mataifa ya magharibi ambao waliusuka kwa umakini ili wamuingize Gaddafi ajikaange mwenyewe na pasipo kujua au labda kutokana na kupaniki kutokana vurugu zilizokuwa zinaendelea nchi nzima Gaddafi akajiingiza kwenye mtego.


Kwanini nasema huu ulikuwa ni mtego?


Mara zote mataifa ya magharibi wakiongozwa na Marekani huvamia nchi kwa kisingizio cha kulinda amani au kulinda raia ikitokea serikali ya nchi husika ikianza kutumia jeshi kudhuru raia wake.


Kwa hiyo muitikio wa kijeshi wa Gaddafi baada ya raia wakorofi kuanzisha vugu vugu la kutumia silaha ulikuwa ni mwanya muafaka kwa mataifa ya magharibi kujipenyeza na kutekeleza mkakati wao wa kijeshi.



Vugu vugu hasa la raia kutumia silaha lilishika kasi kuanzia tarehe 17 February 2011.
Baada ya vugu vugu hili la kutumia silaha kupamba moto ndipo hapa napo hata vikundi vingi vya wapiganaji wa kiislamu wenye msimamo mkali vilivyokuwepo miaka yote navyo vikatumia hii fursa kufanya harakati zao kwa mgongo wa kudai mapinduzi na kumuondoa madarakani Muammar Gaddafi.


Mfano katika mji wa Benghazi, vikundi 12 vya kiislamu viliungana na kulinda umoja waliouita "The February 17th Brigade".

Huko mji wa Misrata na Zaria kukaibuka kikundi cha wapiganaji waliojiita "The Libya Shield".


Kwenye miji ya Zatan na Derna kukaibuka kikundi cha kiislamu cha "Libyan Islamic Fighting Group".


Lakini pia kulikuwa na vikundi vingine kama vile "Obaida Ibn Jarrah" na kadhalika.

973967c4e33c3b71ea87629ea7f106eb.jpg

Moja ya michoro ya kumkejeli Gaddafi iliyochorwa mjini Bayda baada ya vurugu kushika kasi nchi nzima

Serikali ya Gaddafi mara kadhaa ilijaribu kujenga hoja kwa jamii ya kimataifa kwamba vikundi hivi vingi vilikuwa na chembe chembe za mawakala wa kikundi cha kigaidi cha Al Qaida lakini vikundi vyenywe vya waasi walikuwa wanakanusha vikali suala hili.


Lakini kuna wakati ambao kamanda mkuu wa vikosi vyote vya NATO, kamanda James G. Stavridis aliwahi kukiri kwamba kwa kadiri ya taarifa za intelijensia ambazo NATO walikuwanazo, walikuwa wanaamini kwamba kulikuwa na uwezekano wa vikundi hivi vya wapiganaji kuwa na mawakala wa kikundi cha Al Qaida.


Lakini kamanda Stavridis akajenga hoja kwamba uwepo wa wanachama hao wa Al Qaida bado hauna ushahidi wa kutosha kuweza kuthibitosha pasina shaka na hadhani kama kujipenyeza kwao kwenye vikundi hivi vya wapiganaji wa Libya waliokuwa wanataka kufanya mapinduzi ya kumuondoa Gaddafi hakudhani kama walikuwa na ushawishi wowote wa kuweza kuathiri mwenendo au misimamo au muelekeo wa vikundi hivi.



Lakini hoja hizi za Kamanda Stavridis hazina ukweli au labda tuseme zina ukweli nusu tu.
Kuna mawasiliano ya siri ya kieletroniki yaliyonaswa ambayo yalitimwa kutoka ubalozi wa Marekani uliopo Tripoli kwenda kituo cha Combating Terrorism Center katika kituo cha kijeshi cha Marekani kilichopo West Point, ambapo mawasiliano haya yanaonyesha kuwa Marekani walikuwa na taarifa thabiti kabisa kwamba moja wapo ya viongozi wa vikundi vya wapiganaji wanaodai mapinduzi kumuondoa Gaddafi, ambaye aliitwa Abu Sufian Ibrahim Ahmed Hamuda Bin Qumu ambaye kwa wakati huu ulikuwa ni kiongozi wa kikundi cha wapiganaji wabaodai mapinduzi wa Libyan Islamic Fighting Group aliwahi kujiunga na wapiganaji wa Taliban huko nchini Afghanistan mwaka 1998.


Pia Abu Sufian Qumu aliwahi kuwa mfungwa katika gereza la Marekani la Guantanamo Bay.


Pia mawasiliano haya ya siri yalikuwa yanajaribu kutahafharisha jeshi la Marekani kuwa yawezakana Abu Sufian Qumu alikuwa na mafungamano na Al Qaida na pia yawezekana alikuwa ni mwanachama wa African Extremist Network.



Kutokana na vurugu zilizokuwa zinaendelea nchi nzima Gaddafi zilimpandisha hasira Gaddafi na akaapa kamwe hawezi kuachia madaraka kwa sababu ya vugu vugu ambalo alikuwa na hakika lilikuwa linaratibiwa kwa siri kubwa na mataifa ya magharibi.

Hivyo basi Gaddafi akaapa kuwasaka wapiganaji wa vikundi vinavyompinga pamoja na wanaowaunga mkono ambapo alijiapiza kwa kauli ambayo ilijipatia umaarufu sana, kwamba atawasaka "mtaa kwa mtaa, nyimba kwa nyumba na kabati kwa kabati."


Gaddafi pia akawabatiza jina waasi kuwa ni "cockroaches" na "rats"!


Ili kuonyesha kwamba hakuwa anatania alichokuwa anakisema, Gaddafi alilihutubia taifa na kusema kuwa anapokea simu za maelfu ya wananchi kutoka Benghazi wanaodai kuwa wametekwa na kuzuiwa kutoka majumbani kwao kama mateka.


Hivyo Gaddafi akatoa rai kwa vikundi vya wapiganaji kuwa wote ambao watajisalimisha au kutuma silaha na kurejea kwenye maisha yao ya kawaida watasamehewa, lakini wale wote ambao warakaidi agizo hilo, kitakacho wapata damu yao itakuwa juu yao wenyewe.



Hii ilikuwa inakaribia mwishoni mwa mwezi February, na baada ya kauli hizi kali kutoka pande zote mbili ndipo hapa hasa vita ya wenyewe kwa wenyewe nchini Libya ikaanza.!!








KIFO CHA MUAMMAR GADDAFI


626af9a6c9a08d3e85ee15c4a50d42ed.jpg

Moja ya vikao vya kwanza kabisa vya vikundi vya upinzani mjini Bayda vilivyopelekea kuundwa kwa National Transitional Council



Yako mengi ningeweza kuandika kuhusu mapigano ya vikosi vya jeshi vitiifu kwa Gaddafi dhidi ya vikundi vya kudai mapinduzi na kumuondoa Gaddafi madarakani. Lakini nisingependa niandike sana kwa leo kuhusu mapigano hayo badala yake nataka kuegemea zaidi kwenye mfululizo wa matukio ya mwishoni mwa vita ya wenyewe kwa wenyewe ambayo yalipelekea kuuwawa kwa Gaddafi.



Tuendelee…


Mwishoni mwa mwezi February (tarehe 27), kukajitokeza muungano wa kisiasa wa vikundi vyote vya wapiganaji ambao wakaunda ummoja amabo waliufanya kama chombo chao cha uwakilishi wa kisiasa.
Umoja huu waliuita National Transitional Council (NTC).


NTC ilijipambanua kama ndio wawakilishi rasmi wa watu na taifa la Libya.


Mwezi March NTC wakatangaza kutoitambua serikali ya Gaddafi na kujitangaza wao kuwa ndio chombo halali chenye mamlaka ya kutawala na kiserikali nchini Libya.


Kutokana na mataiafa ya magharibi kumpinga vikali Gaddafi haikuchukua muda wakaanza kuitambua rasmi NTC kama chombo cha kimamlaka na kiserikali kwa niaba ya Libya.

Hatua hii ya kuitambua NTC kama chombo rasmi chenye mamlaka 'halali' nchini Libya, ilienda sambamba na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuamuru ku-freeze mali zote za Gaddafi kila sehemu zilipo duniani. Kuanzia fedha kwenye mabenki ya nje mpaka mali zisizohamishika.
Na si hivyo tu, ili pia kuzuia Gaddafi na washirika wake wa karibu wasiweze kutoroka kwenda nje ya nchi, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ukalifanya anga lote la Libya kuwa ni "No fly zone" na wakatoa kibali kwa vikosi vya NATO kutumia nguvu zote walizonazo kuwasaidia NTC kumuondoa madarakani Gaddafi kwa kisingizio kwamba serikali yake ilikuwa inatekeleza oparesheni zenye kukiuka haki za binadamu kwa kiwango kikubwa na kudhalilisha utu wa binadamu.



******


Mwanzoni mwa vita hii vikosi vya Gaddafi zilionyesha kila dalili ya kuwashinda vikundi vya waasi wa NTC.

Lakini baadae kibao kikageuka hasa baada ya NTC kuanza kupata usaidizi kutoka kwa Marekani na washirika wake.


Taratibu vikosi vya NTC vikaanza kuchukukua mji mmoja baada ya mwingine na kuiweka kwenye himaya yake.


Vikosi vya waasi vilifanya mashambulizi makubwa mpaka kufanikiwa kuutwaa mji mkuu wa Tripoli. Walipofikia kuutwaa mji huu ilibidi Gaddafi atoroke na kukimbilia maeneo ya kusini mwa Libya.


Gaddafi aliotoroka Tripoli na msafara Mdogo sana wa magari ili asiweze kugundulia na akaelekea Sirte.
Mtoto wake Mutassim Gaddafi alimfuata baadae akiwa na msafara mwingine wa magari.
Akiwa Sirte Gaddafi alijificha ndani ya mji huo kwa miezi kadhaa akiwa na ulinzi mkali wa vikosi vyenye silaha nzito.


Vikosi vya waasi vilizidi kusonga mbele ambapo karibia na mwezi September walifanikiwa kuuteka mji wa Bani Walid ambao ulikuwa na wakazi wengi wenye kumuunga mkono Gaddafi.


Baadae mwanzoni mwa mwezi October waasi wakaanza kuinyesha dalili za kufanikiwa kuutwaa mji wa Sirte.


Wasaidizi wa karibu wa Gaddafi akiwemo Mansour Dhao kiongozi wake wa vikosi vya "People's Guard" ambaye alikuwa pamoja na Gaddafi mafichonj ndani ya mji wa Sirte anadai kwamba ilifika kipindi Gaddafi akawa "anaishi nje ya uhalisia".
Mfano wakuu wake wote wa masuala ya ulinzi walikuwa wanamshauri kuwa watoroke kwenda nchi jirani, lakini Gaddafi alikataa kata kata kuwa hawezi kuondoka Libya.



e31e3fa49cfd8abc9b332bd2d9566bd1.jpg


e03860ac870728758991d28d3af1d01b.jpg


e04263fe2265b5035e4a22579827768f.jpg

Mapigano ya kugombea mji wa Sirte kati ya wapiganaji wa NTC na jeshi la Gaddafi


Baada ya vikosi vya wapiganaji wa NTC kuzidi kusonga mbele na kuuchukua zaidi mji wa Sirte, Gaddafi akafanya kosa kubwa la kutaka kutoroka kutoka mji huu.
Au pengine niseme kosa lake kubwa lilikuwa ni kuondoka wote kwa pamoja wakiwa katika msafara mkubwa wa magari 75.
Tofauti na namna ambavyo waliondoka Tripoli kuja Sirte ambapo waliondoka muda tofauti tofauti katika misafara midogo midogo.


Lakini safari hii waliondoka viongozi wakuu wote kwa pamoja na msafara mkubwa namna hii wa magari 75. Kwenye msafara huu alikuwemo Muammar Gaddafi mwenyewe, alikuwepo kiongozi mkuu wa jeshi Mansour Dhoa na waziri wa masuala ya ulinzi katika serikali ya Gaddafi, Abu-Bakr Yunus Jabr.



Kutokana na ukubwa wa msafara huu ulikuwa rahisi kuonekana hata kutokea angani.!
Wakiwa wamefika kama kilomita 3 nje ya mji wa Sirte, ndege isiyo na rubani (Predator Drone) ya jeshi la Marekani iliwang'amua na kuanza kuwashambulia.
Baadae ndege ya kivita ya jeshi la Ufaransa nayo ikaungana katika mashambulizi baada ya kitengo cha ushushushu wa kijeshi wa NATO kunasa mawasiliano ya simu ya Gaddafi na wasaidizi wake.



Gari ambalo alipanda Gaddafi halikushambuliwa moja kwa moja bali magari ya mbele yake ndiyo yalishambuliwa vibaya na kusababisha pia kupata ajali kwa gari ambalo Gaddafi alikuwa amepanda.


Shambulio hili la kwanza la NATO liliharibu kabisa magari yapatayo 20 na ikasababisha magari yapatayo kumi na moja kujitenga na msafara na kuendeshwa kwa spidi kubwa kukimbia kuelekea kusini mwa nchi.


Baada ya hapo likafuata shambulio la pili ambalo nalo liliharibu magari mengine zaidi ya 20 na kuvuruga kabisa msafara na muelekeo wake. Shambulio hili la pili pia lilisababisha wapiganaji wa ardhini wa NTC kukimbilia upande huu wa mji na kuanza kuushambulia msafara wa Gaddafi.



Kwa mujibu wa taarifa yao binafsi NATO wanadai kwamba hawakuwa wanajua kama Gaddafi yuko kwenye huu msafara Ila wao walishambulia ule msafara kama "military asset" ambayo walihisi ilikuwa na tishio.


Utetezi huu wanautoa ili kuogopa kuvunja kifungu cha kanuni ya mwaka 1973 cha Security Council Resolution. Kwamba NATO hairuhusiwi kulenga (targeting) mtu binafsi pali walenge "a military asset that pose a threat"!
Japokuwa baadae NATO ilikuja kukiri kwamba shambulio lao la anga lilichangia kwa kiasi kikubwa katika kukamatwa kwa Muammar Gaddafi.



Ikumbukwe kwamba mpaka muda huu Gaddafi bado alikuwa yuko hai.
Hivyo basi yeye pamoja na mwanae Mutassim Gaddafi na waziri wake wa ulinzi, Abu-Bakr Yunus Jabr walifanikiwa kutoroka kutoka kwenye msafara huu ulioshambuliwa vibaya kutoka angani na drone pamoja na ndege za kivita za NATO na bado ukiwa unaendelea kushambuliwa, wakatoroka na kwenda kujificga kwenye nyumba za karibu kutoka hapa walipokuwa.!





Wakiwa kwenye hiyo nyumba ya jirani waliyojificha wapiganaji wa NTC wakawashitukia walipo na kuzingira nyumba za jirani.

Majibizano ya risasi yakapamba moto kati ya walinzi wa Gaddafi na wapiganaji wa NTC.
Mutassim, yule mtoto wa Gaddafi akang'amua mapema kwamba hawawezi kujibizana kwa risasi na wenzao milele, muda si mrefu watazidiwa nguvu au kuishiwa risasi.
Hivyo basi akachukua walinzi wapatao ishirini na kutoka nje kwa njia ya kutambaa kwa tumbo lengo lao likiwa ni wafike barabarani ambapo msafara wao ulishambuliwa na kuangalia kama kuna gari lolote zima walitumie kumtoroshea Gaddafi.



Inaelezwa kwamba Mutassim alijitahidi sana kumsihi baba yake afuatane nao, na baada ya mabishano ya dakika kadhaa Gaddafi akakubali kwenda nao.


Wakatumia mtaro mdogo wa maji machafu unaopita eneo hilo la makazi 'kucrawl' ili wasiweze kuonekana.
Walifanikiwa kutambaa kwa tumbo kwenye mitaro hiyo mpaka kupata mkao mzuri wa "defensive position" ili waweze kujibu mapigo ya wapiganaji ya NTC.


Wakiwa hapa mtaroni moja ya walinzi wa Gaddafi alijaribu kurusha bomu la mkono kuelekea muelekeo walipo wapiganaji wa NTC lakini kwa bahati mbaya bomu hilo likagonga ukuta juu ya mtaro na kurudi pale pale walipokaa na kulipuka.

Mlipuko huu ulisababisha kifo cha yule mlinzi pamoja na waziri Abu-Bakr Yunus Jabr na Gaddafi alijeruhiwa vibaya sana.


Muda huu mtoto wake Mutassim alikuw a tayari ameelekea barabarani na wale walinzi 20.


Kwa hiyo licha ya kujeruhiwa vibaya sana Gaddafi na mlinzi wake ambao walibakia hai baada ya mlipuko walimbilia kwenye mtaro mwingine mkubwa zaidi ulijengwa kwa karavati.


Katika purukushani za kujiokoa kutoka pale mahali kwenye mtaro wa awali baada ya mlipuko, Gaddafi alikuwa amepigwa risasi mgongoni na alikuwa amejeruhiwa vibaya sana lakini bado alikuwa hai na anaweza kuongoa na kutembea kama kawaida.



Bado kuna utata ni namna gani wapiganaji wa NTC waliweza kung'amua mahali Gaddafi alikokimbilia kwa mara ya pili (kwenye mtaro mkubwa wa Karavati) lakini dakika kadhaa baadae wapiganaji hao walikuwa wamewasili eneo lilipo karavati.


Kuna baadhi ya wapinagaji wanadai kuwa walifuatilia michirizi ya damu iliyokuwa inamvuja Gaddafi lakini zipo ripoti zinazodai kwamba ni 'drone' ya Marekani ndiyo iliyo 'mtrack' Gaddafi mpaka kwenye mtaro alipokimbilia.



Vyovyote vile ukweli ulivyo, lakini uhalisia ni kwamba wapiganaji wa NTC walifika kwenye mtaro huu mkubwa na kupiga kelele kumuamuru Gaddafi atoke.


Pasipo kukaidi amri hii Gaddafi akatoka mtaroni akiwa amenyoosha mikono juu kwa ishara ya kujisalimisha. Nguo zake na mwili mzima alikuwa ameloa damu chapachapa.


Wapinagaji wa NTC wakalipuka kwa kelele za furaha na ushindi wakitamka kwa nguvu, "Muammar, Muammar, Muammar!!" na wengine wakipiga kelele za 'takbir', "Allah Akbar, Allah Akbar, Allah Akbar".


Video ya mauji ya Kanali Muammar Gaddafi




Gaddafi alikuwa ametiwa mikononi rasmi kwa maadui zake.


Baada ya kumtia mikononi tu, wapiganaji wa NTC ambao walikuwa katika hali ya furaha iliyopitiliza wakaanza kumshushia kipigo.

Baadhi ya wapiganaji wa NTC waliokuwepo eneo wa tukio wanadai kuwa Gaddafi alianza kuwaomba wasimuue na wasiendelee kumpiga. Alipoona vijana hao hawaelewi Gaddafi alitamka maneno kadhaa makali kama vile, "Mungu alaani hiki mnachokifanya", pia akawa anawauliza kwa kurudia rudia, " Mnajua tofauti ya jambo ovu na zuri?"


Lakini vijana hawa ilikuwa ni kama vile maruhani yamewapanda kichwani. Kitu pekee walichokiona mbele yao ni fursa ya kulipiza 'kisasi' ambacho labda hata hawakujua ni kisasi cha sababu ipi?


Yote haya waliyokuwa wanayafanya walikuwa wanayarekodi kwenye video kwa kutumia simu za mikononi.


Katika moja ya video hizo inaonekana moja ya wapiganaji akimuamuru Gaddafi asimame na Gaddafi akatii akijitahidi kusimama kwa taabu sana bila mafanikio.


Kwenye video nyingine wanaonekana wapiganaji hao wakifurahi kwa kupiga risasi hewani mfululizo na mpiganaji anamfanyia Gaddafi kitenfo cha ukatili mkubwa na udhalilishaji kwa kumchoma kisu/bayonet Gaddafi sehemu ya haja kubwa.



Bado kuna utata mkubwa ni muda gani hasa Gaddafi alifariki na aliuwawa vipi.

Kitu ambacho ni dhahiri ni kwamba alikamatwa akiwa hai. Lakini bado kuna swali alikufaje?


Iko video inayoonyesha akipandishwa kwenye gari la wagonjwa na hawa wapiganaji akiwa hai huku wanashangilia kwa kupiga risasi hewani.


6852a194a6f4d61edf17073c9b9875b6.jpg


8c210d7529a709a03981438d360455f4.jpg


2c71d62f6878296918d521b4cb53912e.jpg

Gaddafi mikononi mwa wauaji wake


Iko video nyingine inaonyesha mwili ambao ubaonekana dhahiri kabisa haukuwa hai ukiwa umelazwa kwenye gari la wazi.



Ripoti ya daktari baada ya mwili wake kufikishwa hospitali inaonyesha kwamba mwili ulikuwa na tundu la risasi kichwani.



Mwanzoni waasi walijitetea kwamba Gaddafi alikuwa kutokana na risasi kutoka kwa wanajeshi wake mwenyewe.
Yaani, wapiganaji hao walidai kwamba mara baada ya kumkamata Gaddafi wakiwa kwenye harakati za kumuondoa kutoka kwenye eneo walilomkamata na kumpeleka eneo la kumubifadhi, walishambuliwa ghafla na wanajeshi wanao muunga mkono Gaddafi na katika majibizano ya risasi, moja ya risasi kutoka upande wa wanajeshi wanaomuunga mkono Gaddafi ikampata kiongozi huyo kichwani na kupoteza maisha.


Lakini suala hilo halina ukweli wowote.



Uchunguzi wa kina uliofanyika baadae umegundua kwamba Gaddafi aliuwawa kwa kupiga risasi kichwani pamoja na wenzake wengine sitini na sita akiwemo mtoto wake Mutassim.



Kwa hiyo siku hii ya tarehe 20, mwezi October mwaka 2011, kiongozi wa Taifa la Libya, mtu ambaye alilitoa taifa hilo kutoka 'mavumbini' na kuliweka katika viwango vya juu kuwa moja ya nchi bora kabisa duniani, aliuwawa na raia wake mwenyewe kwa kusaidiwa na maafui zake wa miaka mingi wa magharibi, raia hao walio muua mdio hao hao ambao alitumia zaidi ya miongo minne kuwatumikia na kuwaletea maendeleo ya kihistoria.


October 20, 2011 ndio ilikuwa siku ya mwisho kwa Gaddafi juu ya uso wa dunia akiwa hai.

Soma videokezo hapo chini, post zinazofuata hapo chini baada ya post hii
 
KIDOKEZO #1




MAONYESHO YA MWILI WA GADDAFI


Baada ya kifo chake, serikali ya mpito iliyoongozwa na NTC iliuweka mwili wa Gaddafi kwenye freezer katika eneo la wazi la umma kati kati ya mji kwa ajili ya watu kujionea "ushahidi" kwamba Gaddafi ameuwawa.


Watu wengine walisafiri maelfu ya kilomita kutoka kila kona ya nchi ili kujionea "ushahidi huu".

Mwili wake uliwekwa hivyo pembeni ya mwili wa mtoto wake Mutassim mpaka siku ya Tarehe 24 October, 2011 ambapo uliondolewa kwa ajili ya maziko.

4a9f3e817d23b33a33d8cafb0eabd954.jpg
 
KIDOKEZO #2





KABURI LA GADDAFI



NTC waliuzika mwili wa Gaddafi jangwani katika eneo ambalo halijawahi kugundulika mpaka leo hii.

Mwili wa Gaddafi ulizikwa sambamba na mwili wa mtoto wake Mutassim Gaddafi pamoja na waziri wake Abu-Bakr Yunis Jabr.



Wote kwa pamoja walizikwa tarehe 25 October 2011.
 
KIDOKEZO #3





UNAFAHAMU CHEO CHA MUAMMAR GADDAFI?




Mara nyingi nikiwa "kijiweni" na zikianza stori kuhusu Gaddafi huwa napenda kuwauliza watu 'swali la kizushi' kama wanafahamu Gaddafi alikuwa ni nani nchini Libya!


Yawezekana wewe unafahamu lakini ajabu ni kwamba watu karibia 8 au 9 kati ya kumi ninao wauliza swali hili kama wanafahamu cheo cha Gaddafi, huwa wanajibu kuwa alikuwa ni Rais wa Libya!!


Kama ulikuwa haufahamu nikujuze kwamba Gaddafi hakuwa Rais wa Libya, wala hakuwa waziri mkuu, wala hakuwa mfalme.


Binafsi huwa napenda kusema kuwa cheo cha Gaddafi ni yeye binafsi ndiyo alikuwa anakielewa kiufasaha zaidi maana hata wananchi wake walikuwa hawakielewi sawia na lilipoanza vugu vugu moja ya vitu vigumu vilivyo kuwa vigumu kujieleza kwa wananchi ilikuwa ni cheo chake.


Gaddafi alipenda kujipambanua nafasi yake kama "Brotherly Leader and Guide of the Revolution of Libya" (au kwa kifupi "Brotherly Leader").


Chini yake kuna Rais, kisha kuna Waziri Mkuu na Baraza la mawaziri.


Gaddafi alikuwa anakanusha vikali kukihusisha cheo chake na "ufalme" bali alipenda kujipambanua kama "mtoa muongozo wa taifa" au "visionary" wa taifa.


Lakini mara kadhaa akiwa anafafanua cheo chake alipenda kutumia mfano wa Malkia Elizabeth wa Uingereza kuwa yeye ni "figurative head", ni kiongozi mkuu wa nchi lakini hausiki na shughuli za kuendesha serikali kila siku. Au tuseme hajajipa mamlaka ta kiserikali.


Hii kwa kiasi fulani ilikuwa inakinzana na uhalisia kwa kuwa ukweli ni kwamba Gaddafi licha ya mazuri yake yote, lakini alikuwa ameiweka Libya kiganjani mwake. Anachokisema yeye hakuna mwenye uwezo wa kukipinga na hakuna maamuzi yoyote makubwa yanayofanyika bila yeye kuafiki.


Pia Gaddafi alipenda kuelezea nafasi yake hiyo kama "Philosopher" wa taifa.
Hii inadhihirishwa na nadharia mpya ya kimfumo wa kiutawala aliotumia kuongoza Libya ambao mwenyewe aliuita "Jamahiriya" (state of the masses) ambao yawezekana mfumo huu wa kiutawala hautumiki sehemu nyingine yeyote zaidi ya Libya kipindi cha uhai wake.
 
SEHEMU YA TATU



Nifah Divine... glory to yhwh BansenBurner Alisen Papushikashi Magazine Fire miss chagga SANCTUS ANACLETUS mngony Excel Mussolin5 Jimena Inferiority Complex gwijimimi wambura marwa Hoshea shareef conscious wambeke The Boss Deejay nasmile gkileo Juma chief Mangi flani hivi Ngongo makaveli10 KENZY kadada wa pili Root aretasludovick jonnie_vincy Clkey KAFA.cOm mbewe makedonia Afande Nyati peterchoka Leonard Robert Nchi Kavu STUNTER Chrizo jully Van persie Khalidoun Tetramelyz punje haradari Mazigazi @Alybaba babu na mjukuu platozoom jimmyfoxxgongo Nicodemas Tambo Mwikozi Ls man Heaven Sent sifongo Infantry Soldier haa mym 20acres MTS MarkHilary compos Tembo2 Erick the future nancy1983 Bulah binsaad Fazzaly the wolf everhurt Melvine Mgibeon kijana wa leo samsun Coolant Jagood pacesetter apologize payton George Betram kisengeli Kiranga Jiwe Linaloishi Madame B jay john Guasa Amboni Dinazarde Analyse Diva Beyonce snowhite Mmanu Expected Value onechromosome Missy rose Innocenthezron Immortal_MH Ficus sunola Robot la Matope mamaafacebook II JEKI likikima Compact scorpio me G'taxi YNWA adna yuzo ntamaholo Otorong'ong'o naan ngik-kundie kandukamo1 AFRICA101 mwalidebe Kobe Blaki Womani kalendi savius The Great Emanuel r2ga Ntaluke.N. Transcend Msemachochote Mchumiajuone mwampepec MTOTO WA KUKU Fukara proto cute kawombe zinginary MLALUKO JR Vupu barafu BlackPanther Ntuzu Matola impongo ntamaholo Mkoroshokigoli Deadbody KING easy mahoza Msolo kkenzki deborah1 KIDUDU buffalo44 winlicious riziki Allys MUHUNZI Moses2015 nacktary Liuumi dochivele Renzo @barbers hmjamii mbere TATIANA famicho LUCKDUBE mwanadome Straton memphis ghazar Graph Theory Honey Faith Shunie Slave ddcmanesto zinginary pacesetter Nkanaga KOMUGISHA mikatabafeki johnsonmgaya lee empire wigo MJINI CHAI Asprin mtzmweusi Erasto kalinga Chrizo kichakaa man LULU bike FORTALEZA poleni shibumi ZE DONE umande Edger Sr sir joshua sammoo Roram Password Bavaria hambiliki mwanangu Asili100 Evarist Massawe nice1 Jumong S Rogie 1babake nasreen uberito baest dustless Kilemachocho Tumosa mtembea kwa miguu Debbs Joe scorpnose musacha shibumi seeker of knowledge Simuchi Veni Vidi Vici TUJITEGEMEE abuu garcia Hon Nkundwe Festo Festo marion09 mike2k The dream bro kay vandelintz kirikou1 POINT LOAD lusaka city Dirham Rodcones bato MANCNOO multiphill90 GEORGE Dalali mwanamalundi90 MwaFreeca Roram Ta-kibombo troublemaker mambo KOMUGISHA calabocatz Papaa Azonto Msemachochote Mdomo bakuli tizo1 option dikembe iL Buono fakalava ABDUL KAREEM @Gobe Justine Marack Goodluck Mchika MR UNINFORMED darcity nkasoukumu nG'aMBu thatonegAl kabanga MPARE KIBOGOYO Edward Sambai Rassa mnonje srinavas last king of uscoch proto cute Kennedy krava Rais2020 kbosho Mzee wa BsN sam2000 fuma 999 Bableee dawa yenu The Certified DON SINYORI mij adden



bwii ONTARIO Kobe The Vein Mondray jaxonjaxon successor mzee wa liver sawariya Sitaki ukuda Domhome Mpatanishi MKANDAHARI mtugani wa wapi huyo wealthier cluecell Toyota escudo mgumu2 troublemaker Linamo shedede kamtu33 SteveMollel ngushi Donald stewart Mshuza2 Glycel mnonje Ochuanilove SingleFather Santi DEOD 360 ngushi anatory antony ukhuty chris van chicha auxillius Goma Son Hubeb pes KING DUBU VILLAIN mwayena donbeny Aleppo JipuKubwa shoo61 BOMBAY John mungo Nyakageni bato Dogo 1 sufra chamlungu painscott wegman Bravo Engliash MOSELBAY wa stendi FaizaFoxy bigmind cadabraa Internal Kelvin mwalukas mnonje Kelvin X Somoche Wgr30 Miiku Poise Jabman kalamuyamwalimu BOMBAY the say juxhb witnessj Gide MK Mmanyema mgogoone Mnongane Mandingo koncho77 afsa ngaboru Paradoxer Heavy Metal KIMBURU 06 Raaj kichekoh ngumba njeche kikale DullahTza Goodluck Mshana juliusDarcy Denis Kasekenya mashonga kitalembwa Khaleed Shaban middle east SirChief jiwe jeusi Mkambarani mansakankanmusa
 
MWISHO

Kuna mengi mno ya kuandika kuhusu maisha ya kanali Muammar Gaddafi lakini kwa makala hii nitaishi hapa...
shukrani mkuu the bolded...vipi ile ya JFK?Imemalizika nayo? Mungu abariki kazi za mikono yako
 
MWISHO

Kuna mengi mno ya kuandika kuhusu maisha ya kanali Muammar Gaddafi lakini kwa makala hii nitaishi hapa...
Mkuu asante...

Hivi maisha ya walibya yakoje baada ya miaka 6 ya kifo cha Muammar??

( naomba ufafanuzi kama hautajali)
 
Safi mkuu hata mi napenda atudadavulie kuhusu personal issue zake
Yeah, atieleze marital status, alikuwa na wake wangapi? Watoto wangapi? Halafu nasikia alikuwa anaishi kwenye hema, kivipi?
 
Back
Top Bottom