Kamugisha Kazaura is a new TTCL CEO

Kamugisha Kazaura is a new TTCL CEO

mungu akupe nguvu ya kutekeleza majukumu yako kaka.nchi hi inahitaji vijana tumechoka na wazee wa mvi kutoa matamko wakati wakiwa madarakani walishindwa piga kazi kaka.
 
CV yako haitufai chochote hamna jipya kiutendaji, tunahitaji Safaricom/Safaritel yetu
 
CV tuliyoletewa haijitoshelez, as yeye mwenye alikua ni seemu ya downfall ya TTCL..kielimu yes, yupo vizuri na yupo kwenye field aliyosomea, wasiwasi wangu ni experience, exposure na management! Et toka kuzaliwa kafanya kazi TTCL tu, sitegemei jipya kutoka kwake tena ukichukulia ameteuliwa na system ile ile ya .... walioifikisha nchi hapa!Ngoja tusubr kusikia timu yake ya wasaidizi, labda kutakua na jipya ...
 
Kamugisha kazaura...aka MUGI...hongera kaka, wewe pamoja na Peter Ulanga(CEO-Mfuko wa Mawasiliano) mnawakilisha "timu ile" ya KIBAHA SECONDARY SCHOOL

Mwl. Kazibure(RIP) na Mkuu wa Shule Mwampaja hakika walifanya sehemu yao...

na SISI TUNAKUJA MUGI...hakuna wa kutuzuia......go Kibaha...go...

Hiyo ni timu ya KIBO 1991....

Kwa upeo tu, vijana walikuwa wakali sana.....

Hongereni Peter na Mugi....
 
Hongera sana mungu akuongeze ila kuna malalamiko kwamba wafanyakazi hawalipwi inavyopaswa, eti wanaangalia sura ikiwa nzuri mshahara mkubwa na ikiwa mbaya utajiju sasa anzia na kuweka sawa ishu hizi ili wachape kazi mbona hili shirika pesa ziko waziwazi?! Na mie mkiajiri ntahamia huko huyu muhindi kashanichosha bora nije niitumikie jamhuri.
 
...Bje Kidoogo ya Mada. Hivi Mshahara wa CEO wa TTCL unaweza ukawa Shilingi ngapi katika kipindi hiki cha Ushindani? na wa Vodacom? Airtel? Tigo? Zantel?
 
Hajamalizaaa.....Kwani kampuni yote ya TCCL ni shilingi ngapi? Hongera naamini knowledge is power kulingana na CV yako tu umefunika mbaya...kila la kheri kijana mwenzetu
 
Hello Mjukuu uko juu muraa! sasa kama m2 kapiga umande namna hii kwanini asipewe kitengo? anayesema Nshomile kabebwa apelekwe milembe kupimwa akili,I am sure the guy will deliver much nawakubali watu wanaofanya tafiti kama huyu Iwe!
 
...Wote tunaoitakia Mema TTCL tumuombee Hivyo lakini ni Ngumu Sana.
Anaweza Kuishia kwenye Vicious Circle ya 'Busines as Usual' tu.
Amefungwa Mikono.
Hawezi kuvunja Mkataba wa Ovyo wa TTCL na Celtel/Zain/Airtel Unaoivunja mbavu TTCL wa kutumia Minara na Mitambo ya TTCL bila Kuilipia.
Hawezi kuisambaza itakiwavyo Huduma rahisi ya Simu za Mkononi ya TTCL 073 ambayo ingeweza kuwapiga bao hawa Wahuni wote lakini kwa Vile Wazito wetu wengi wana Hisa kwenye Makampuni haya basi TTCL inabanwa Mbavu ili isisambaze sawa sawa tekinolojia yake ya simu ya Huaiwei kwa visingizio hivi na Vile.
Kuna Mdai amechangia vyema hapo juu. Aitishe ajira mpya na kuzipa kampuni za akina Deloitte kupata wafanyakazi wa aina yake wanaoweza kuipeleka Kampuni yetu ya Taifa.
Kuna Vijeba ndani ya TTCL ambavyo havikubali mabadiliko.
Ninawafahamu watu wawili watatu ambao wameishia Darasa la Saba na Form 4 (potelea mbali kwamba ni ya zamani!) lakini Meza wanazokalia, utazimia mwenyewe.
Ni hawa hawa ambao mteja Mzungu akiingia hawajua waongee nini naye na wanawasukumizia wenzao kwa sababu Lugha haipandi!

Kuna Mengi yanayoweza kumkwamisha Msomi huyu lakini kwa leo niishie hapa na kuwapa nafasi wengine Kuchangia...




Kam ukifanya hivyo alivyosema Babadesi somo yangu ki ukweli kampuni itasonga mbeleeeeeeeeeeee!!!!!!!!!!!!
 
Sijui watoto wetu waliosoma shule za kata kuna siku watakuwa ma CEO?naona u CEO watausikia tu kwenye radio,tv,magazeti na Jamiiforums.Mchezo wenyewe unaanza hivi baba kigogo,anajulikana katika mashirika na taasisi zote,anampeleka mwanae ''shule zilizoenda shule'',pia ni rahisi kumpeleka ulaya kwani visa kwa kijana si tatizo baba kigogo ana connection kote ulaya ,anacheza gofu na mabalozi na pia account yake ya Uswisi inapumua Pound,mwanawe anapelelkwa mamtoni na kusoma chuo chochote kila anachokitaka,na kazi yake ni kusoma tu ,box kwake ni simulizi tu,akializa tu baba yake anampachika sehemu anayojua kwa kuangalia tu kuwa baada ya muda kijana wake atakuwa ''ndarekta'' kwa muda mfupi baada ya wazee a analogi kustaafishwa kwa kutojua ulimwengu wa kidijitali ,baba anampigia ndogo ndogo kijana wake kwa kigogo mwenzake ,na hatimaye ''mtoto wa baba anakuwa CEO'',sasa mtoto wa mkulima na shule za kata hata msingi wa lugha ya mama ,shughuli mwisho wake unabakia mpika chai na mpeleka vipeto vya ofisi.Hili tabaka la watoto wa wakubwa na malofa ndio linazidi kupanuka,watoto wa wakubwa wakishindwa shule wao huwa wabunge,manaibu waziri n.k.
 
Nadhani ni uteuzi makini kinadharia ila kivitendo ni mpaka tutakapoona anachokifanya. Wakati mwingine hawa wasomi wetu wametuangusha mara kadhaa kiutendaji. Sina haja ya kutoa mifano hapa, zaid ya kumtakia kila la kheri Dr Kazaura.
 
I want to add on top of what you've said. I know that to work as a CEO of any big corporation like TTCL requires you to be very experienced to problem solving in whatever circumstance you are, but also you have to be ready to face challenges of any type when it comes to critical situation like the one we are in.
 
I can understand how hard to face the reality of our world today is. But it is inevitable that one should think of keeping in touch with it. No one can change the world in a single day. But if we put our sholders together we can find a way out of our problems in one day.
 
nimependezwa sana kwa kujina kushika nyadhfa nyeti kama hiyo, wazee waache kumpiga mkwara sasa afanye kazi yake kwa amani 🙂
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom