Kampuni za kuagiza magari ughaibuni laghai sana

Kampuni za kuagiza magari ughaibuni laghai sana

NI MTAZAMO TU

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2014
Posts
1,203
Reaction score
1,001
Habari wa kuu, elimu ni bora kabla ya kutwendwa maana majuto huwa siku zote ni mjukuu,

Kuna kampuni mmoja nilituma pesa inaitwa tredecarview Gari yenyewe sikufanikiwa na uipata pesa nimezungushwa sana na hawa jamaa mpaka kufanikisha kupata pesa yangu ilichukua muda..

Sasa tunaomba kwa wengine wanaojua makampuni laghai, ambao hawapo kibiashara wayaanike hapa ili iwe faida kwa wana jf..

Nawasilisha...
 
tumia kampuni zenye wakala Dar es salaam,Tanzania kama SBT.COM
 
Asante sana mkuu, nimekuta wa2 wengi wanaisifia sana SBT.CO ngoja nijaribu j3
 
Me pia nimekuwa nawatumia SBT kwa mwaka wa pili sasa na kwa bahati nzuri wamefungua ofisi zao za uwakala hapa Dar. Ni waaminifu sana hawa jamaa
 
Kwanza tradecarview sio kampuni ya kuuza magari,bali kampuni za kuuza magari utangaza bidhaa zao tradecarview,ukitaka kununua gari kupitia kampuni iliyomo tradecarview ni bora ulipie kwa payetrade kwa uhakika zaidi.

Kampuni ya uhakika ni sbt,japanesevehicle(Trust) na Beforward.
 
utakuwa kuna vitu ulkosea, jamaa ni waaminifu na wako active sana
 
Habari wa kuu, elimu ni bora kabla ya kutwendwa maana majuto huwa siku zote ni mjukuu,

Kuna kampuni mmoja nilituma pesa inaitwa tredecarview Gari yenyewe sikufanikiwa na uipata pesa nimezungushwa sana na hawa jamaa mpaka kufanikisha kupata pesa yangu ilichukua muda..

Sasa tunaomba kwa wengine wanaojua makampuni laghai, ambao hawapo kibiashara wayaanike hapa ili iwe faida kwa wana jf..

Nawasilisha...

Ulivutiwa na bei nafuu ya magari kule!! ule ni mtandao tu ambao watu wanaotaka kuuza magari yao wanaweka pale, tofauti na SBT au Be Forward ambao wanauza wenyewe. Ili usipigwe pesa ungetumia huduma yao inaitwa PAYTRADE ambayo ukituma pesa, muuzaji hapewi hiyo pesa hadi alitume hilo gari. Muuzaji akikushawishi mfanye biz nje ya paytrade hapo ndio mwanzo wa kupigwa pesa maana pesa unaituma kwake binafsi. Ni rahisi kuingia mitini. Pole sana.
 
Tradecarview ni mtandao ambao kampuni mbalimbali wanaouza magari hutangaza magari husika humo...... kama sbt, real motors, befoward nk nk.nk

Ili uwe safe zaidi tumia paytrade...
 
Sasa kati ya SBT na Be Forward wanatofauti gani, yupi ni bora zaidi na kwanini?
Embu toeni ufafanuzi kuhusu PAYTRADE, kwanini alipwe fedha yeye wakati sio wakala wa kuuza magari kutoka Japan?
 
Sasa kati ya SBT na Be Forward wanatofauti gani, yupi ni bora zaidi na kwanini?
Embu toeni ufafanuzi kuhusu PAYTRADE, kwanini alipwe fedha yeye wakati sio wakala wa kuuza magari kutoka Japan?

Ipi ni nzuri zaidi kati Sbt na Be foward.Tunaomba mtusaidie anayezifahamu hizo kampuni
 
Sasa kati ya SBT na Be Forward wanatofauti gani, yupi ni bora zaidi na kwanini?
Embu toeni ufafanuzi kuhusu PAYTRADE, kwanini alipwe fedha yeye wakati sio wakala wa kuuza magari kutoka Japan?

SBT na Be Forward wanauza magari wenyewe na wana tovuti zao. Tredecarview ni mtandao ambao hata wewe ukiwa una gari unaweza weka tangazo lako hapo ili uuze. Ni sawa na wewe ufungue tovuti uiite www.uza-nunuagari.com hlf watu wawe wanaweka matangazo yao ya kuuza magari ila wewe mwenyewe huuzi kitu, unafaidia na watu kuweka matangazo yao hapo. Sasa watu wakawa wanapigwa pesa na wauzaji wasio waaminifu. Wenye tovuti yao wakaona waweke huduma iitwayo paytrade ambapo badala ya kumtumia pesa muuzaji, unaituma kupitia paytrade, wao watamtaarifu muuzaji kuwa pesa imetumwa hivyo akutumie gari, akishatuma gari ndio analipwa pesa yake. Ila hiyo huduma utailipia. Ila kama sikosei majuzi walinitumia email wakisema huduma hiyo ya paytrade sasa ni bure. Tredecarview ni sawa na tovuti ya "kupatana" kwa hapa TZ
 
Wadau?.IPI NI KAMPUNI INAYOFAA ZAIDI KWA KUAGIZA MAGARI toka Ughaibuni kati ya

SBt.com na Be Foward?.
Tunaomba mwenye uzoefu (experience) na makampuni yote mawili atusaidie kutudadavulia
 
Ipi ni nzuri zaidi kati Sbt na Be foward.Tunaomba mtusaidie anayezifahamu hizo kampuni

Nishatumia Be Forward, rafiki yangu akatumia SBT, sijaona tofauti kubwa, zaidi majadiliano kwa hasa khs discount kwa SBT hufanywa kwa simu (wanakupigia wao ukionesha kulitaka gari), Be forward yanafanyika kwa email. Magari huchukua wiki 5-6 hadi kukufikia.
 
Me pia nimekuwa nawatumia SBT kwa mwaka wa pili sasa na kwa bahati nzuri wamefungua ofisi zao za uwakala hapa Dar. Ni waaminifu sana hawa jamaa

Acha uongo wewe,kujiunga kwenyewe JF ume Join 7th April.Post 5.
Halafu hapa kuna kitu kinaendelea.
Ila kama kuna mgao tuambiane,ili namie nianze kuwaponda hata kama sina hoja
 
Nishatumia Be Forward, rafiki yangu akatumia SBT, sijaona tofauti kubwa, zaidi majadiliano kwa hasa khs discount kwa SBT hufanywa kwa simu (wanakupigia wao ukionesha kulitaka gari), Be forward yanafanyika kwa email. Magari huchukua wiki 5-6 hadi kukufikia.

Ahsante mdau kwa elimu nzuri.
 
Zanzibar Spices;12418271]Acha uongo wewe,kujiunga kwenyewe JF ume Join 7th April.Post 5.
Halafu hapa kuna kitu kinaendelea.
Ila kama kuna mgao tuambiane,ili namie nianze kuwaponda hata kama sina hoja

Acha jazba kaka! Nimezungumzia duration ambayo nimekuwa nikiwasiliana na kuhudumiwa na SBT, lakin kujiunga JF hyo 7th bado sio tatizo inawezekana nimekuwa mkongwe kuliko ww coz b4 nilikua natumia account na ID tofauti ww. POLE KAKA
 
Back
Top Bottom