Kampeni maalumu: 2025 Mpe mama tabasamu

KARLO MWILAPWA

JF-Expert Member
Apr 10, 2019
2,590
4,601
Ndugu zangu,

Nimekusudia kwa mapenzi mema na moyo mkunjufu kufanya kampeni maalumu itakayokwenda Kwa jina la 2025 MPE MAMA TABASAMU. Kampeni hiyo itakuwa na malengo kuu matatu

Lengo la kwanza, kufikisha ujumbe maalumu kwa watu wote, nikielezea kazi na mafanikio ya CCM na Rais Samia. Lengo hili litakwenda sambamba na kuutaka Umma kuwa wavumilivu maana tunaelekea nchi ya Ahadi.

Lengo la pili, kukisaidia Chama Cha Mapinduzi Kwa ushauri, maoni na mapendezo ili Kwa pamoja tutekeleze kampeni hii ya 2025 MPE MAMA TABASAMU. Naomba Chama changu mnipokee niwasaidie kwenye eneo hili.

Lengo la tatu, kuwaomba wananchi Kwa nini 2025 tunatakiwa TUMPE MAMA TABASAMU. Kulingana na kazi kubwa, nzuri na ya kupigwa mfano kama sehemu ya shukrani na fadhila hatuna budi kumpa TABASAMU. MPE MAMS TABASAMU Kwa kumpa ushindi wa kishindo na kukipa ushindi wa kishindo Chama Cha Mapinduzi.

Kwa pamoja, tuungane kutekeleza kampeni hii ya 2025 MPE MAMA TABASAMU. naamini tutakuwa pamoja.

Karibuni maana kampeni hii nakusudia imfikie Kila mtu hususani mwenye umri wa kupiga kura. vijana, wazee, wakina baba ,wakina mama karibuni Kwa kampeni ya 2025 MPE MAMA TABASAMU

Ahsanteni.
 
Wewe unajua kabisa kuna kosa lilifanyika kumpa nafasi raia wa nchi ya kigeni (ya Zanzibar) kutawala nchi yetu ya Tanganyika Kwa jina la "muungano fake", yet bado wewe unaanzisha kampeni ya kipuuzi ya kufagilia kosa hilohilo liendelee kufanyika?

Au na wewe ni Mzanzibari na hivyo unamfagilia Mzanzibari mwenzako?

This is my polite advise to you. Please, remove this rubbish from JF screen server immediately.

Hatuhitaji ujinga huu. Sisi hatuhitaji kuendelea kuwa wajinga zaidi wakati tayari tulishajua makosa yako wapi ya shida na taabu inayopitia nchi yetu..

Tunataka Mtanganyika awe Rais wa Tanganyika bila kujali atatoka chama gani. Lakini huyu mwanamke Tena raia wa kigeni, IT'S A BIG NO!!
 
Ndugu zangu,

Nimekusudia kwa mapenzi mema na moyo mkunjufu kufanya kampeni maalumu itakayokwenda Kwa jina la 2025 MPE MAMA TABASAMU. Kampeni hiyo itakuwa na malengo kuu matatu

Lengo la kwanza, kufikisha ujumbe maalumu kwa watu wote, nikielezea kazi na mafanikio ya CCM na Rais Samia. Lengo hili litakwenda sambamba na kuutaka Umma kuwa wavumilivu maana tunaelekea nchi ya Ahadi.

Lengo la pili, kukisaidia Chama Cha Mapinduzi Kwa ushauri, maoni na mapendezo ili Kwa pamoja tutekeleze kampeni hii ya 2025 MPE MAMA TABASAMU. Naomba Chama changu mnipokee niwasaidie kwenye eneo hili.

Lengo la tatu, kuwaomba wananchi Kwa nini 2025 tunatakiwa TUMPE MAMA TABASAMU. Kulingana na kazi kubwa, nzuri na ya kupigwa mfano kama sehemu ya shukrani na fadhila hatuna budi kumpa TABASAMU. MPE MAMS TABASAMU Kwa kumpa ushindi wa kishindo na kukipa ushindi wa kishindo Chama Cha Mapinduzi.

Kwa pamoja, tuungane kutekeleza kampeni hii ya 2025 MPE MAMA TABASAMU. naamini tutakuwa pamoja.

Karibuni maana kampeni hii nakusudia imfikie Kila mtu hususani mwenye umri wa kupiga kura. vijana, wazee, wakina baba ,wakina mama karibuni Kwa kampeni ya 2025 MPE MAMA TABASAMU

Ahsanteni.
Ishu siyo tabasamu tunahitaji mtu serious haswa na fikra pevu za kulikomboa taifa hili lenye utajiri wa mali lakini watuwake maskini.
Tabasamu mpe mumeo/mkeo msituletee mahaba kwenye kulijenga taifa
 
Kama ni maendeleo yamefanyika chini ya uongozi wa Samia au kama mmavyosema maendeleo yamefanywa na Samia kwanini yasijionyeshe yenyewe hadi wewe umsemee ??

Mbona hapa kwa wenzetu sijawahi sikia wanatenga siku kusema maendeleo yaliyofanywa rais??

Muache Samia maendeleo aliyoyafanya yanajionyesha na ndio yanasemwa na yanayowagusa wananchi acha nyie mnaolipwa kumsemea.

Wananchi wanaona maendeleo kwenye sukari, umeme, maji , mafuta na miundombinu hayo hayahitaji nguvu yanaongelewa sana bila malipo.
 
Kama ni maendeleo yamefanyika chini ya uongozi wa Samia au kama mmavyosema maendeleo yamefanywa na Samia kwanini yasijionyeshe yenyewe hadi wewe umsemee ??

Mbona hapa kwa wenzetu sijawahi sikia wanatenga siku kusema maendeleo yaliyofanywa rais??

Muache Samia maendeleo aliyoyafanya yanajionyesha na ndio yanasemwa na yanayowagusa wananchi acha nyie mnaolipwa kumsemea.

Wananchi wanaona maendeleo kwenye sukari, umeme, maji , mafuta na miundombinu hayo hayahitaji nguvu yanaongelewa sana bila malipo.
Kama unachosema ni sahihi basi kusingekuwa na haja Kwa mataifa makubwa yaliyoendelea kuwa na kampeni za Urais Kwa sababu maendeleo yanaonekana dhahiri sana.

Lengo la kuongelea mafanikio ya Rais Samia si Kwa ajili ya wanaofahamu kazi za Rais na mipango aliyonayo bali Kwa wale wasiofahamu. Mtu ambaye haumwi hahitaji daktari ila mgonjwa
 
Ishu siyo tabasamu tunahitaji mtu serious haswa na fikra pevu za kulikomboa taifa hili lenye utajiri wa mali lakini watuwake maskini.
Tabasamu mpe mumeo/mkeo msituletee mahaba kwenye kulijenga taifa
Rais Samia ni mzuri kwenye ujenzi wa Taifa Kwa kutumia falsafa yake ya 4R na mahusiano ya kimataifa lakini bila kuwaambia watu ili wajue wasiomtakia mema Rais Samia watakuja kupotosha kazi yake nzuri.

Lengo la MPE MAMA TABASAMU ni kuwakumbusha kuwa wavumilivu maana Taifa bora chini ya Rais Samia inakuja
 
Wajinga kama wewe mpo wengi. Mpeni tabasamu mama yenu. Upigaji uendelee
Kama ni mfuatiliaji mzuri wa ripoti za kimataifa basi utakubaliana na Mimi kwamba katika kipindi cha utawala wa mama kulingana na ripoti ya Transparency International rushwa imepungua sana nchini huku kwingine duniani hali ikiwa mbaya. Mama kuimarisha eneo la rushwa na ufisadi na anazidi kufanya vizuri
 
Mza
Wewe unajua kabisa kuna kosa lilifanyika kumpa nafasi raia wa nchi ya kigeni (ya Zanzibar) kutawala nchi yetu ya Tanganyika Kwa jina la "muungano fake", yet bado wewe unaanzisha kampeni ya kipuuzi ya kufagilia kosa hilohilo liendelee kufanyika?

Au na wewe ni Mzanzibari na hivyo unamfagilia Mzanzibari mwenzako?

This is my polite advise to you. Please, remove this rubbish from JF screen server immediately.

Hatuhitaji ujinga huu. Sisi hatuhitaji kuendelea kuwa wajinga zaidi wakati tayari tulishajua makosa yako wapi ya shida na taabu inayopitia nchi yetu..

Tunataka Mtanganyika awe Rais wa Tanganyika bila kujali atatoka chama gani. Lakini huyu mwanamke Tena raia wa kigeni, IT'S A BIG NO!!
Mzanzibari ni mtanzania, hii ni JMT na sio Jamhuri ya Tanganyika.
 
Kwamba unataka kumnyang'anya kwa nguvu Mzee Wassira kazi yake ya mikakati...!!!
Uzuri wa wanaCCM ni kwamba hata aliyepo kijijini anajua jukumu lake ni kusaidia ushindi wa Chama hivyo Kila mtu ana nafasi yake lakini yenye uzito tofauti na ya mwingine
 
Back
Top Bottom