Kamishna wa Intelijensia ya Jinai CP Charles Mkumbo: Polisi tupo timamu kwaajili ya Uchaguzi Mkuu 2025

Kamishna wa Intelijensia ya Jinai CP Charles Mkumbo: Polisi tupo timamu kwaajili ya Uchaguzi Mkuu 2025

figganigga

Platinum Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
26,662
Reaction score
59,099
Kamishna wa Intelijensia ya Jinai kutoka Makao Makuu ya Polisi CP Charles Mkumbo, wakati akiwasilisha mada kwenye kikao kazi cha 20 cha maafisa habari wa Serikali kilichofanyika Zanzibar Aprili 3 - 6, 2025 alisema Jeshi la Polisi limejiandaa kwaajili ya Uchaguzi Mkuu wa 2025

Mkumbo alisema kwamba Mkuu wa Jeshi la Polisi ameshawaelekeza Nchi nzima watu kujiandaa kwa Uchaguzi. Kwahiyo sasa hivi wapo Timamu hata kama uchaguzi ungekuwa keshokutwa.

Amesema Polisi wana vifaa vya kutosha kutimiza majukumu kabla wakati na baada ya Uchaguzi.

Kahimiza watu kuwa Wazalendo kwa kuipenda Tanzania.

"Sisi ni watoto wa Tanzania hii, iwapo machafuko yakijitokeza tutakimbilia wapi? Hatuna Tanzania A wala N, tuna Tanzania moja tu. Tuhamasishe Uzalendo, Amani Utulivu na Usalama katika kipindi chote cha Uchaguzi". Amesema CP Charles Mkumbo.

 
Yeye Kamishna anakula mshahara mkubwa na maposho ya kufa mtu huku askari wa chini wakiwa na maisha magumu kutokana na kuwa na mishahara mbuzi.

Askari wa Kawaida watasimama na Wananchi mwaka huu kudai Mabadiliko ya kweli

No Reform No Election 💪
 
Yeye Kamishna anakula mshahara mkubwa na maposho ya kufa mtu huku askari wa chini wakiwa na maisha magumu kutokana na kuwa na mishahara mbuzi.

Askari wa Kawaida watasimama na Wananchi mwaka huu kudai Mabadiliko ya kweli

No Reform No Election 💪
Uko USA nini?
 
Askari wa Kawaida watasimama na Wananchi mwaka huu kudai Mabadiliko ya kweli

No Reform No Election 💪
Hawa ambao Chadema kutwa mnawatukana kila siku kuwaita polisiCCM na kuwadhalilisha kuwa bila polisi CCM haishindi kuwa polisi ni sehemu ya uovu bila ushahidi

Ndio wawaunge mkono nyie wehu.wa Chadema?

Mnapotishia kuwa mko tayari kwa uasi mnaelewa maana yake? Kuwa mtaleta usumbufu kwa polisi waache kulala na wake zao majumbani washinde zamu usiku kucha bila usingizi kisa nyie.Wao watafutiwa hadi likizo kwa ajili ya ubwege wenu Polisi gani awapende Chadema?

Katika watu ambao hawawapendi Chadema polisi wanaongoza sababu muda mwingi mnawapa usumbufu

Wakati vyama vingine hata vikifanya mikutano hata polisi waweza wasiende lakini nyie saa yeyote mnaibua vurugu au kutoa matamshi yanayohatarisha amani

Polisi gani wawapende nyie?

Nyie ni risk factor kwa polisi
 
Tanzania ndio nchi pekee ambayo polisi wako busy na mambo ya uchaguzi kuliko wanasiasa na tume ya uchaguzi.

Taifa la vilaza.
 
Back
Top Bottom