migomo ya vyuo
Member
- Jun 14, 2011
- 58
- 18
Friday, 26 August 2011
Na Waitara Meng'anyi, Tarime
KAMISHNA wa Operesheni za Jeshi la Polisi Nchini, Paul Chagonja, amewaruhusu wananchi wanaoishi maeneo yanayozunguka Mgodi wa North Mara, kuwapiga kama wezi, askari wakorofi wanaowavamia na kuwanyanyasa kinyume na taratibu za jeshi hilo.
Ruhusa hiyo ilikuja kufutia tukio la Jumanne wiki hii, la askari walioendesha operesheni ya kamata watu na kulipua mabomu ya machozi, kwa maelezo kuwa walikuwa wanadhibiti walioingia mgodini kinyume cha taratibu.
"Nasema, ikiwa askari atakuja kukukamata wakati akiwa hana namba Inayoambatana na jina lake, apewe kipigo hadharani na msimhurumie. Huyo si mwenzetu," alisema Chagonja wakati akizungumza na wakazi wanaozunguka mgodi huo jana.
Na Waitara Meng'anyi, Tarime
KAMISHNA wa Operesheni za Jeshi la Polisi Nchini, Paul Chagonja, amewaruhusu wananchi wanaoishi maeneo yanayozunguka Mgodi wa North Mara, kuwapiga kama wezi, askari wakorofi wanaowavamia na kuwanyanyasa kinyume na taratibu za jeshi hilo.
Ruhusa hiyo ilikuja kufutia tukio la Jumanne wiki hii, la askari walioendesha operesheni ya kamata watu na kulipua mabomu ya machozi, kwa maelezo kuwa walikuwa wanadhibiti walioingia mgodini kinyume cha taratibu.
"Nasema, ikiwa askari atakuja kukukamata wakati akiwa hana namba Inayoambatana na jina lake, apewe kipigo hadharani na msimhurumie. Huyo si mwenzetu," alisema Chagonja wakati akizungumza na wakazi wanaozunguka mgodi huo jana.