Kamati za Lowassa na Zitto zavunjwa

Kamati za Lowassa na Zitto zavunjwa

ccm,ccm,ccm,ccm,ccm.............kidumu chama cha mapinduzi,zidumu fikira sahihi za mwenyekiti wa ccm.....zidumu,ndugu zangu leo tumekuja kufanya mambo mawili cha kwanza ni kummaliza Lowassa ili urais uwe hadithi,na pili Zitto kabwe kwani amezoea sana kuchunguza chunguza hela za wakuu huko Uswiss,so tunamziba mdomo
 
Na ile kamati ya nishati na madini ya akina John Mnyika bado iko likizo pamoja uwepo wa sakata lote la gesi. Na spika amegoma kusema Likizo hiyo itaisha lini. Hii ni hatari kwa mustakabali wa nchi yetu.

Mikael,

Kwa mfumo tulio nao sasa, wananchi wanaisimamia serikali kupitia kwa wawakilishi wao, yaani wabunge. Kamati za bunge zinafanya kazi kwa niaba ya wananchi ikiwa ni pamoja na kuidhinisha mapato na matumizi ya fedha, na kukagua mwenendo wa matumizi hayo.

Alichokifanya spika (kuvunja kamati inayosimamia mashirika ya umma), ni kunyang'anya wananchi mamlaka ya kuisimamia serikali kupitia bunge. Huu ni uhaini. Hili ni moja.

Pili, maamuzi haya ya spika - ya kupora mamlaka toka kwa wananchi - yamekuja sambamba na hoja iliyowasilishwa na serikali ya kunyang'nganya (tena) watanzania - kupitia kwa wabunge wao - mamlaka ya kupokea na kuchambua taarifa za mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali!

Nini tafrisiri yake?

Serikali haitaki kabisa 'usumbufu'. Hawataki kuulizwa wala kufuatiliwa kwenye utendaji wake ikiwa ni pamoja na kukaguliwa kwa matumizi ya kodi ya watanzania. Kwa sasa watanzania kujua matumizi ya kodi yao itakuwa ni 'fadhila' toka kwa rais.

Na huu ni mkakati wa kamati mpya wa kamati ya CCM chini ya Mangula, Kinana na Dr Asha Migiro, wa kuondoa 'transparency' kwenye governance system Tanzania. Kelele tulizozikia kule Addis Ababa, kwamba Tanzania imefanya vizuri kwenye utawala bora, ilikuwa ni ujenzi wa uzio ili wakifanya huu uharamia dunia isijue! Na hapa ndipo watanzania wanatakiwa kuwa macho zaidi.

lli kuokoa hii nchi na balaa linaloinyemelea basi 2015 ni vema bunge lisiwe dominated tena na wale wale walioruhusu 'uporwaji' huu wa haki ya wananchi kuisimamia serikali.

Kuhusu bunge
Kwa sasa hivi Tanzania hatuna bunge. hatuna! Tuna idara ya serikali inayokaa Dodoma -mara kadhaa kwa mwaka- ambapo wabunge toka vyama vingine wanaruhusiwa kuingia lakini kuongea inategemea mkalia kiti kaamka vipi siku hiyo. Hatuna bunge. Na kama kuna mtu amerudisha hii nchi nyuma, basi Makinda anaongoza. Makinda atakumbukwa kwa kuuwa Demokrasia Tanzania. Hili halina ubishi. Na huko tunakokwenda, ni mungu mwenyewe anaweza kuinusuru hii nchi na mabalaa yanayopaliliwa na huyu mama. Very unfortunate.
 
Zitto Zuberi Kabwe‏@zittokabwe"@omarilyas: @zittokabwe katika tamaduni za kibunge, budget committee si huongozwa na wapinzani?" Hii yetu itakuwa under ruling party


Yaonekana hata kamati ya bajeti sasa itaongozwa na magamba.....kuna agenda gani jamani?
 
makupa jitahidi kuweka utaifa mbele hata kama unafaidika na huo uozo unaoendelea.

Mkuu uoza ni wa mtu binafsi na si wa kitaasisi msitake kabisa kuwalisha watanzania uwongo
 
Uongozi wa Bunge ni kama vile umepoteza muelekeo, labda tuendelee kusikiliza watakuja na hadithi zipi juu ya kufanya hayo waliyofanya.
 
Kwa hiyo wameifuta kamati ya Zitto ili waendelee kuiba?

Au kuna sababu gani za kufuta hiyo kamati?

Sababu ni kupambana na kanuni ya transparency. Wameingilia kwa fujo na sasa imewashinda,TBC ndio hiyo sasa inatunyima haki ya kujua mambo nyeti,Bunge ltecnically imejipokonya mamlaka ya kujadili report ya CAG. Sasa wameamua kuficha uchafu wao kwa gharama yoyote kama moja ya mikakat yao ya kujisaficha mbele ya wananchi. Nas tunatafuta mbinu ingine ya kuendelea kuwaanika.
 
Last edited by a moderator:
They will never stop changes hata watembee uchi mitaa yote ya Tanzania, tena uchi wa nyama... Let them hide everything, thrtuth shall prevail!!!
 
Mwk mmoja kamati ya ulinzi na usalama mwingine anahamishiwa Mambo ya nje .

Huku political game likiendelea welawelaaaa.
 
Na ile kamati ya nishati na madini ya akina John Mnyika bado iko likizo pamoja uwepo wa sakata lote la gesi. Na spika amegoma kusema Likizo hiyo itaisha lini. Hii ni hatari kwa mustakabali wa nchi yetu.
Wanaogopa hata Kivuli chao, hali hii inajitokeza ndani ya miaka 2 sijui kama 2014 itakuwaje...., Vipi ile ya Cheo mbona haifutwi? ana wameona lile walilolitumaini kwa bwana Zitto halipo naona wamechange mind..... twende kazi kitaeleweka tuuuu
 
Na ile kamati ya nishati na madini ya akina John Mnyika bado iko likizo pamoja uwepo wa sakata lote la gesi. Na spika amegoma kusema Likizo hiyo itaisha lini. Hii ni hatari kwa mustakabali wa nchi yetu.

bila shaka moyo wako utakuwa umefurahi sana maana kwa jinsi usivyompenda zitto plus ule ushahidi wako wa uongo ulioutoa baraza ili zitto afukuzwe japo ulibuma hahaaaa
 
Na ile kamati ya nishati na madini ya akina John Mnyika bado iko likizo pamoja uwepo wa sakata lote la gesi. Na spika amegoma kusema Likizo hiyo itaisha lini. Hii ni hatari kwa mustakabali wa nchi yetu.

bila shaka utakuwa umefurahi kamati ya zitto kuvunjwa maana ambavyo humpendi ulitamani afukuzwe baraza kuu ndo mana ukatoa ushahidi wa uongo
 
Kamati ya Mrema ile inayo ongoza kwa kupokea rushwa#mbunge wa Bahi Omar Baduel haija guswa?
 
Kuna sababu tena muhimu tu.ila pia poac ilikuwa kama inapitiliza majukumu yake mana ilikuwa inafanya hadi kaz za kamati za kisekta....
 
'nulum arbitrium sine' giving reasons for the decisions. Maamuzi ya kiti cha spika hayajatoa sababu ya kufanya ivo.
 
ni wajinga tu ndio wataipa ccm kura! Bunge linatekeleza maagizo ya serikali kuuu! Upumbavu mtupu
 
Back
Top Bottom