Kamati ya Sitta kuiundia zengwe UKAWA

Kamati ya Sitta kuiundia zengwe UKAWA

amakyasya

JF-Expert Member
Joined
Jun 26, 2013
Posts
3,480
Reaction score
918
Ni baada ya kushindwa kufikia muafaka wa maridhiano. Kamati imeamua kuendelea na bunge la katiba endapo UKAWA hawatarudi bungeni agosti 5. Pia wamedai kuwa wataenda kuwashtaki UKAWA kwa wananchi.
Source: Mwananchi.
 
Wasioingia bungeni wapigwe chini tu. Simpo.
Hapo kwenye red, huo ndio utumbo wa mnyama gani? Ulitaka kusema "simple" au hayo ndiyo matokeo ya shule za kata ambapo kiingereza chako kimekomea hapo?
 
Ni baada ya kushindwa kufikia muafaka wa maridhiano. Kamati imeamua kuendelea na bunge la katiba endapo UKAWA hawatarudi bungeni agosti 5. Pia wamedai kuwa wataenda kuwashtaki UKAWA kwa wananchi.
Source: Mwananchi.
i


Jamani nisaidieni kuelewa,najua swala hili lina pande mbili.Mbona tunambiwa ya UKAWA tuu,kususia vikao na ushawishi unao fanywa ili warejee ukumbini? Ajabu hatuelezwi juhudi za kushawishi upande wa pili kukubali kujadili Rasimu ya tume ya katiba na si vinginevyo! Kuna nini hapo?
 
Wawashitaki kwa wananchi kwa kosa lipi! La kutoshiriki kuchukua posho ya laki 3 kwa siku au kukataa kujadili rasimu feki ya ccm? Sitta alilikologa mwenyewe muacheni alinywe. Watanzania tulimuamini lakini akaingia kwenye mtego wa mafisadi akachakachua kanuni, tangu siku hiyo nikampotezea hana sifa kabisa ya utawala
 
i


Jamani nisaidieni kuelewa,najua swala hili lina pande mbili.Mbona tunambiwa ya UKAWA tuu,kususia vikao na ushawishi unao fanywa ili warejee ukumbini? Ajabu hatuelezwi juhudi za kushawishi upande wa pili kukubali kujadili Rasimu ya tume ya katiba na si vinginevyo! Kuna nini hapo?

Umesema kitu mkandarasi. Juhudi kubwa zingefanyika kuwashawishi ccm kujadili rasimu ya Warioba na si vinginevyo lakini wao wanaangaika na ukawa tu.

Kwa nini ccm wasijitokeze na kusema tutajadili rasimu ya warioba kama ilivyopendekezwa na wananchi? Niwambie tu kwamba tumepiga sana kelele lakini hawatuelewi hawa ccm sasa wakumlaumu ni Rais basi
 
Mlisema ukawa ndio chanzo cha vurugu sasa inakuwaje mlazimishe watu mliodai ndio chanzo cha matatizo warudi? Ukawa tumejiridhisha kuwa nyie ni watetezi wetu hampo hapo kwaajili ya posho.
 
-Chui kuwa hakimu mbuzi atashinda kesi? Ukawa wana akili sio kama wachumia tumbo kama ccm.

-Sita kumbe naye ni kilaza nampongeza sana lowasa kwani sita amejimaliza mwenyewe kwenye mbio za urais hivyo lowasa hana tena mpinzani ccm
 
Nashauri Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania liitishwe ili kubadili sheria ya Bunge Maalum ili kusiwe na ulazima wa akidi ya Theluthi Mbili. Pia nashauri kuwa vifungu juu ya muundo wa muungano vipitishwe kwa mujibu wa maoni ya walio wengi na Bunge Maalum lijikite sana kwenye masuala yanayohusu moja kwa moja maslahi ya wananchi
 
i


Jamani nisaidieni kuelewa,najua swala hili lina pande mbili.Mbona tunambiwa ya UKAWA tuu,kususia vikao na ushawishi unao fanywa ili warejee ukumbini? Ajabu hatuelezwi juhudi za kushawishi upande wa pili kukubali kujadili Rasimu ya tume ya katiba na si vinginevyo! Kuna nini hapo?

Walioweza pigia kilele swala hilo kwa upande wa ccm ni wachache sana na yote hyo ni UNAFIKI TU wengi wanajiuma uma tu kwa vile walioharibu mchakato wapo madarakani

Ccm inatumia pesa nyingi sana kwa wamiliki wa vyombo vya habari hasa hariri wa vyombo hivyo ili kuendelea kupotosha kuhusu upande wa ukawa ila kiuhalisia wenye tatizo hapa ni wale walioingiza swala la serikali mbili ambalo halimo ndani ya rasimu hii ya pili

Kila ukawa wanavyokutana na ccm au viongozi wa serikali ukawa mara nyingi wanabaki kwenye ajenda yao kuu ya kutaka rasimu ya pili pamoja na misingi yake iheshimiwe just simple like that ila wenye minguvu kama ya samson wao wanataka tumia nguvu tu hata sehemu isiyohitajika nguvu bali akili na maarifa tu
Acha wakaandike katiba ya ccm,katiba ya watanzania tutaipata in future

Inshaallaah
 
Back
Top Bottom