Kamati ya Sitta kuiundia zengwe UKAWA

Kamati ya Sitta kuiundia zengwe UKAWA

Tukumbuke katiba ni ya taifa zima,tumwombe mungu atupe hekima ya kulimaliza hili kwa utashi na uzalendo,mungu ibariki tz
 
mlisema ukawa ndio chanzo cha vurugu sasa inakuwaje mlazimishe watu mliodai ndio chanzo cha matatizo warudi? Ukawa tumejiridhisha kuwa nyie ni watetezi wetu hampo hapo kwaajili ya posho.

hivii ile posho ya laki saba imepitishwaa au ilikuwa ni kivutio cha kuwavuta ukawa warudi mjengoni?
 
Tume ya Warioba ilifanya kazi iliyotukuka na kwa mTZ yeyote mwenye kufikiri na kuona mbali ile Rasimu ni nzuri sana kwa vizazi vijavyo! Kura yangu ya maoni napiga kwa Rasimu ya Katiba Mpya ya Tume ya Warioba.
 
Kwa mwendo huu Wa CCM naona soon Tanzania ikiingia kwenye Machafuko makubwa sana ya kisiasa. Na hii yote ni Sababu ya huyu Mcheza ngoma Mzaramo a.k.a ------.
 
CCM wanawalazimisha UKAWA kurudi kwenye bunge la Katiba bila kueleza ni Rasimu ipi inaenda kujadiliwa pale, hili ni jambo la ajabu sana, ni vema maoni ya wananchi wengi(democracy of majority) iheshimiwe siyo matakwa ya CCM maana hapa hatufanyi mchakato wa kuandika katiba ya CCM kama ingelikuwa hivyo sisi ambao ni non-CCM tusingepiga kelele na kukemea jambo hili, Katiba ya JMT ni ya wananchi wa JMT siyo ya chama chochote cha siasa hivyo CCM waache kulazimisha mambo as if tunatunga katiba ya CCM
 
Hapo kwenye red, huo ndio utumbo wa mnyama gani? Ulitaka kusema "simple" au hayo ndiyo matokeo ya shule za kata ambapo kiingereza chako kimekomea hapo?

Nafikiri ni matokea ya huyu mdudu anayeitwa "Bigi Rizalti Nau"
 
Tukumbuke katiba ni ya taifa zima,tumwombe mungu atupe hekima ya kulimaliza hili kwa utashi na uzalendo,mungu ibariki tz

Kuna wakati mwingine tunamsingizia Mungu kwa ujinga wetu wenyewe. Do You mean tumuombe Mungu aishawishi ccm iache rasimu yake na ifuate ya tume? Kwanini tusiwaambie ccm wenyewe moja kwa moja? Si ndio hawa hawa tunakula nao, tunaongea nao, tunapanda nao daladala, tunaongea nao hata humu kwenye huu uzi wapo kibao, tunashinda nao nk!!!!??
Mwacheni Mungu aitwe Mungu na afanye kazi yake.
 
Gharama za unafiki wa bunge la katiba na mabilion yaliyotumika ni EPA nyingine....shangilieni tu
 
UKAWA mnajikaanga kwa mafuta yenu wenyewe. wananchi wanawashangaa.

Hivi niwatanzania gani wanaowashangaa Ukawa kutoludi bungeni,mkuu bado unafikili watanzania waleo bado ni wale wa zama za mawe? Pole sana,mmebaki watz wachache sana wanaotumia nywele kufikili kama wewe.
 
Ukawa ni viherehere sana hakuna lolote njaa tuu na tamaa ya madaraka bunge litaendelea na katiba mpya itapatikana walie tuuu na mwakani tunawanyima kura tuone kama mtafurukuta bila ruzuku
 
Sita anazidi kujivurugia ndoto zake za kugombea urais.
 
Back
Top Bottom