Kamati Kuu CCM yakutana Ikulu, Dar

Kamati Kuu CCM yakutana Ikulu, Dar

Informer

Platinum Member
Joined
Jul 29, 2006
Posts
1,629
Reaction score
6,812
Wakuu,

Taarifa toka chanzo chetu Magogoni ni kuwa Kamati Kuu ya CCM ninapoandika wapo Ikulu na inahisiwa watajadili hali ya kisiasa nchini (UKAWA, Bunge la Katiba na Mtikisiko unaoletwa na 'Wagombea Urais') na kuandaa Agenda za Kikao cha NEC kitakachofanyika Mbeya hivi karibuni.

Zaidi, tegeni masikio

==========

UPDATE:

attachment.php

Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongoza kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM jijini Dar es salaam leo
 

Attachments

  • Kikao-CCM-Ikulu.jpg
    Kikao-CCM-Ikulu.jpg
    75.8 KB · Views: 6,918
Masuala madimu sana kwa CCM - UKAWA imewakaba kooni balaa!!.
 
Kikao anachoingia Nape huwa hakina jambo la maana sana litakaloamuliwa..ajenda ya mtoto wa rais kutaja majina 11 ya wanaofaa kuwa ma rais haitajadiliwa?
 
Tatizo tunasahau sana wabongo!!
kwani ndio mara ya kwanza hicho kitu kufanyika Ikulu??

Je ni sahihi???!!!!
Ndio haya haya awamu hii mtoto wa raisi anataja idadi ya wagombea uraisi wapi wanafaa na wapi hawafai!! Soon first lady atakuwa anaendesha baraza la mawaziri maana kashaanza kupokea ripoti mikoani!!!!!
 
chama cha watu makini kinajadili ajenda makini na muhimu..ukawa sio ajenda ya CCM na haitakuwa ajenda kamwe.
 
Wakuu,

Taarifa toka chanzo chetu Magogoni ni kuwa Kamati Kuu ya CCM ninapoandika wapo Ikulu na inahisiwa watajadili hali ya kisiasa nchini (UKAWA, Bunge la Katiba na Mtikisiko unaoletwa na 'Wagombea Urais') na kuandaa Agenda za Kikao cha NEC kitakachofanyika Mbeya hivi karibuni.

Hawana jipya,jana aliyoyasema dr slaa yamewastua wamezoea kutumia ubabe kumbebesha punda mzigo,sasa punda ameanza kuchoka na ameshaanza kugoma pia kuwekewa mzigo,sasa kinachofuata ni nini...........................kitegueni hicho kitendawili
Zaidi, tegeni masikio
 
Serikali inayoendekeza ''groupthink'' ni hatari sana kwa wananchi wake. Nachelea kusema kwamba hicho kikao wajumbe wote wataenda kupewa misimamo na kazi yao ni kuconform tu. what a shame.!!
 
Back
Top Bottom