RUGAHIMBILA E R
Member
- Mar 5, 2009
- 95
- 32
Kamati ya Mpito inayosimamia Msikiti wa Ijumaa Jijini Mwanza imekuwa ikiwatapeli mamilioni ya fedha wafanyabiashara wa hapa kwa kuwalipisha pesa na kuwapa mikataba ya kupanga vyumba ambavyo tayari vinao wapangaji. Ajabu unakuta chumba kimoja kimelipishwa watu zaidi ya watano na wote wamepewa risiti na mikataba halali. Mhasibu Bwana Mansoor Maruzuku ndiye anapokea hizi pesa. Wafanyabiashara wamemdai pesa anajibu kwa jeuri kwamba hakuna wa kumfanya lolote nchi hii na ajabu bado anaendelea kutapeli watu wengine kwa kuwapangisha vyumba hi to hivyo hewa.
Wafanyabiashara wamejaribu kushtaki kwenye vyombo husika ikiwa pamoja na kuambatanisha vidhibiti vyote lakini hakuna linalofanyiwa kazi. Pamoja na kupeleka malalamiko RITA ambao ndio wasimamizi wao lakini nao wameamua kukaa kimya wakiacha hali hii iendelee.
Je hawa jamaa wako nyuma ya nani anayewafanya wafanye huu wizi waziwazi bila woga wala aibu yoyote?
Je wataendelea kuwaibia watu pesa zao mpaka lini
Tafadhali vyombo husika mulikeni hawa jamaa.
Taarifa na nyaraka zote ziko kwenye vyombo husika na ziko wazi.
Angalizo: Hii haihusiani na migogoro inayoendelea ndani ya msikiti huo.
Wafanyabiashara wamejaribu kushtaki kwenye vyombo husika ikiwa pamoja na kuambatanisha vidhibiti vyote lakini hakuna linalofanyiwa kazi. Pamoja na kupeleka malalamiko RITA ambao ndio wasimamizi wao lakini nao wameamua kukaa kimya wakiacha hali hii iendelee.
Je hawa jamaa wako nyuma ya nani anayewafanya wafanye huu wizi waziwazi bila woga wala aibu yoyote?
Je wataendelea kuwaibia watu pesa zao mpaka lini
Tafadhali vyombo husika mulikeni hawa jamaa.
Taarifa na nyaraka zote ziko kwenye vyombo husika na ziko wazi.
Angalizo: Hii haihusiani na migogoro inayoendelea ndani ya msikiti huo.