Kamanda mwandamizi wa Boko Haram aitwae Amir Adamu Rugu Rugu ajisalimisha kwa majeshi ya Nigeria akiwa na wake zake watatu na watoto

Richard

JF-Expert Member
Oct 23, 2006
14,939
20,400
Mmoja wa makamanda wa juu kabisa wa kikundi cha ugaidi cha Boko Haram aitwae Amir Adamu Rugu Rugu amejisalimisha siku ya Alhamisi jioni kwa majeshi ya Nigeria.

Rugu Rugu alijisalimisha akiwa na wake zake watatu na watoto katika mji wa Gwoza ndani ya jimbo la Bono ambako ndipo vikosi vya jeshi la Nigeria vyaendesha operesheni iitwayo Hadin Kai.

Kamanda huyo ambae anasifika kwa ukatili na mauaji ya wananchi kadhaa katika maeneo ya milima ya Mandara na msitu mnene wa Sambisa aliamua kujitokeza baada ya mashambulizi ya anga na ardhini ya majeshi ya Nigeria.

Katika operesheni hiyo ya Hadin Kai majeshi ya Nigeria yalikazania kushambulia sehemu ya kaskazini ilipo misitu hiyo ya Sambisa na milima ya Mandara mfululizo.

Mpaka sasa magaidi wa Boko Haram wapatao 1000 na familia zao wamejisalimisha, 51 wamekamatwa na wananchi wapatao 29 wameokolewa na majeshi hayo.

Katika operesheni hiyo pia idadi ya majambazi 13 wakiwemo waporaji wa kutumia silaha pamoja na magaidi wamekamatwa.

Operesheni hiyo inahusisha majeshi ya Nigeria na vikosi mbalimbali vya usalama.

Chanzo:

Vyombo mbalimbali vya habari vya Nigeria likiwemo jarida la Vangard.
 
Mmoja wa makamanda wa juu kabisa wa kikundi cha ugaidi cha Boko Haram aitwae Amir Adamu Rugu Rugu amejisalimisha siku ya Alhamisi jioni kwa majeshi ya Nigeria.

Rugu Rugu alijisalimisha akiwa na wake zake watatu na watoto katika mji wa Gwoza ndani ya jimbo la Bono ambako ndipo vikosi vya jeshi la Nigeria vyaendesha operesheni iitwayo Hadin Kai.

Kamanda huyo ambae anasifika kwa ukatili na mauaji ya wananchi kadhaa katika maeneo ya milima ya Mandara na msitu mnene wa Sambisa aliamua kujitokeza baada ya mashambulizi ya anga na ardhini ya majeshi ya Nigeria.

Katika operesheni hiyo ya Hadin Kai majeshi ya Nigeria yalikazania kushambulia sehemu ya kaskazini ilipo misitu hiyo ya Sambisa na milima ya Mandara mfululizo.

Mpaka sasa magaidi wa Boko Haram wapatao 1000 na familia zao wamejisalimisha, 51 wamekamatwa na wananchi wapatao 29 wameokolewa na majeshi hayo.

Katika operesheni hiyo pia idadi ya majambazi 13 wakiwemo waporaji wa kutumia silaha pamoja na magaidi wamekamatwa.

Operesheni hiyo inahusisha majeshi ya Nigeria na vikosi mbalimbali vya usalama.

Chanzo:

Vyombo mbalimbali vya habari vya Nigeria likiwemo jarida la Vangard.
Boko Haram wenyewe washazidiwa nguvu na kikundi kingine ndiyo maana Shekau aliuawa na hicho kikundi
 
Yap!... kikundi kipya cha 'Iswap'
Yah, islamic state west africa province, yaani hicho no kifaranga cha IS,kikiachwa kikomae kitakuwa hatari si tu kwa nigeria na cameroon,bali kwa afrika nzima,ndiyo maana inafaa amani ya afrika iwe jukumu la nchi zote za afrika,siyo kuacha hadi nchi moja ielemewe ndiyo na magaidi wasambae nchi nyingine ndiyo majirani waanze kuburuza miguu kusaidia,jumuia ya afrika ni mbwa koko.
 
Back
Top Bottom