Kamanda Mpinga tunaomba ufafanuzi

Kamanda Mpinga tunaomba ufafanuzi

Tunajenga uwanja wa ndege mkubwa wa kimataifa ktk jiji la Chato,,
Hebu changieni pesa wananchi kwa njia hii ya kulipa faini kidogo tu ya 30,000/= kwann hampendi maendeleo ya jamhuri nyie watanganyika mmekalia kulalamika tu
 
Mkuu ni maelekezo toka juu ili zipatikane hela za kujenga viwanda,nilivyomuelewa kamanda taa zilizokuja na gari hazina Shida ila zile za kuongeza kwa kununua mtaa wa Lumumba ndo Shida,ila kwa sababu wanaojua wao na maelekezo toka juu zaidi wanafanya kila liwalo wa meet target
Kama ni hivyo basi kazi tunayo, wakimaliza suala la taa watabuni kingine, sijui watasema magari yote tufunge tairi nyeupe, aah ni shida.....
 
With a serious note nakubaliana na hoja.
1.Kuna taa ndogo zinawaka moja kwa moja kusaidia aliye mbele kuona gari jana wamenikomalia
2.Tinted zipi zimezuiwa
 
Sidhani kama polisisiem wana uwezo wa kutofautisha fog light na sportslight,wewe walipe hela la kujenga uwanja wa ndege kule CHATU.
 
Hivi kwenye Road trafic act hayo mambo yapo? Au unapigwa faini kwa maneno ya mtu alielala akayawaza na kuja kuyaongea?
 
Mmmmh wenye magar nyofoen taa zote msijekumbwa na fani aiseee hii serikali yetu kudadasadeki ....nimeshaanza kaprocess kakuagiza kagar kangu sasa inabid niache tuu nicijemtemea MTU mate usoni inakera etiiiii
 
Shida hapa ni lugha iliyotumika na sio dhamira. TAA ZILIZOKUJA NA GARI ndio neno linalochanganya watu hapa.

Labda na tuanze na KUJA KUTOKA WAPI? Agizo la Kamanda linalenga kuziacha TAA ZILE ZILIZOWEKWA NA MANUFACTURER TU na si vinginevyo. Gari lako la mtumba kama limetoka Japan au India, na huko lilikokuwa likitumika awali ndiko walikokuwa wameongeza taa zaidi ya zile ambazo manufacturer aliweka...zitoe kabla 30 haijakuhusu.

Taa zote zaidi ya zile alizoweka muundaji wa gari lako zinahusika na zoezi hilo...watch out.
Foglights mkuu maelezo ya awali hayakukaa sawa
 
Niligoma kutoa hela ya ku brashi viatu vya trafiki juzi baada ya kunisimamisha kwa sababu gari yangu ina vioo vya tinted madirishani.... ikanibidi mi ndo nimweleweshwe yeye kwamba tinted inayokatazwa ni ya kioo cha mbele na sio madirishani.
 
Nchi ya matamko hii,Baada ya Taa mtaskia watu watoe Sports Rim maana hatari sana!
 
Ningeandika kwa kiswahili hakuna mtu angeshangaa lakini kwa vile ni kimalkia kila mtu anajitahidi kuonesha kuwa ni mzuri kimalkia. Hongera sana mkuu
Hapana umeandika sawa kabisa na maana inaeleweka it's from born day yani haijaongezwa na watu mtaani hasa wa tz .. me nimekupata kabisa hata me ningeelezea hivyo hivyo kuwa na amani
 
Hapana umeandika sawa kabisa na maana inaeleweka it's from born day yani haijaongezwa na watu mtaani hasa wa tz .. me nimekupata kabisa hata me ningeelezea hivyo hivyo kuwa na amani
Mkuu inaoneka walimu wako hawakupata shida sn, kimombo ni kipana sn hasa sisi tulisoma sekondari za kata kuelewa inakuwa ni vigumu sana.
 
Back
Top Bottom